Mwanamkiwi
JF-Expert Member
- Mar 7, 2019
- 2,023
- 2,399
Jamii chache zilijua kuvuma nguo, lakini wa jumla nguo ziliagizwa kutoka nje. Biashara ya misafara kutoka pwani kwenda bara ilipeleka idadi kubwa za nguo katika maeneo yote yaliyokuwa karibu na njia za misafara. Bidhaa kuu zilizoingizwa zilikuwa nguo, waya, lule za kioo, pamoja na bunduki, baruti (na pombe kali kidogo kwa machifu). Msafara uliweza kuwa na wapagazi 1000 hadi 2000.1844 tulikuwa tunatoa wapi nguo.
Njia kuu za misafara zilikuwa 1) bonde la Pagani kwenye kaskazini kuelekea ziwani Viktoria, 2) Bagamoyo / Saadani kwenda Tabora - Ujiji, 3) Kilwa kufuata Rovuma hadi Ziwa Nyasa.
Viwanda vya nguo huko Uhindi, Marekani na Ulaya vilizalisha kwa ajili ya soko la Afrika. Ilhali hawakuwa na pesa, futi kadhaa za kitambaa zilikuwa bei ya kununulia pembde za ndovu na watumwa, waliorudishwa tena pwani.
Kwa hiyo nguo zilipatikana tu, angalau karibu na njia za misafara.