Albedo
JF-Expert Member
- Feb 24, 2008
- 5,559
- 1,452
Source: K I D A UCHADEMA WAVAA MAGWANDA DARASANI.
Wanachama sugu na viongozi wa chadema tawi la Chuo kikuu cha Mt.Augustine(SAUT) Mwanza leo wametinga madarasani kuhudhuria mihadhara(lectures) wakiwa ndani ya sare(uniform) za chama chao. Wanachama hao na wapenzi wafuasi wa chadema wameonekana chuoni hapo na mavazi yao huku wanachuo wengine wakibakia kushangaa. Baada ya kufuatiliwa nyendo zao na kuhojiwa walisema hiyo ni njia moja wapo ya kuhamasisha watu kuwaunga mkono katika maandamano yatakayofanyika kesho jijini hapa.Maandamano hayo imefahamika rasmi kuwa yataanza saa saba mchana,na yakianzia Standi ya mabasi ya Buzuruga hadi viwanja vya wazi vya Furahisha maeneo ya Kiruba jijini Mwanza.Lakini baadhi ya watu wameonesha kuwa na wasiwasi wa kushiriki maandamano hayo kwa kuhofia kupigwa mabomu na risasi za moto. Pia wengine wamedai kua kesho ni siku ya kazi hivyo muda huo watakuwa wako kazini hivyo wao walipendelea ingekuwa Jumamosi au Jumapili.Mmoja wa viongozi wa tawi la chuo cha SAUT aliulizwa juu ya hofu ya mabomu alisema"tunajua wazi kuwa mabomu yatakuwepo ila sio yale ya Mbagala na Gongo la Mboto hivyo tutaandamana,lakini kwa amani".