Hii ni ya muhimu sana

WISE 2012

JF-Expert Member
Mar 13, 2012
634
460
Tumia dakika chache kufanya uamuzi na siku nyingi kufanya utafiti.Wanaume wengi wanaongoza kwa kuhonga huwa na mkono mfupi wa kuhudumia familia zao pamoja na kuwajali wazazi wao.

Ni kazi rahisi kumkuta mwanaume anakunywa pombe bar ya Tsh 200,000/- kwa usiku mmoja na mama yake mzazi ana pair mbili za kitenge bila kusahau wazazi hawana uwezo hata wa kununua Kg ya nyama,ila ni kazi rahisi sana kumpangia mwanamke kimada chumba na kumnunulia gari kimada wakati familia yako inalalia mihogo ama viporo

Nitajie mtu anayemtolea Mungu fungu la kumi ambaye hana mafanikio katika maisha yake ? Nionyeshe kijana yeyote ambaye huwatumia wazazi wake pesa za matumizi ya nyumbani ambaye hajastawi katika maisha bora na yenye tija ?Kila palipo na baraka ya wazazi pana hazina ya mafanikio daima.

Jitahidi mara nyingi kuwapa wazazi faraja ili wakunenee maneno yenye baraka na hazina ya furaha yako katika maisha yako.Manung'uniko huleta laana katika maisha ya mwandamu na maneno ya baraka huleta mafanikio katika maisha .Ni wakati sahihi wa kuwapa faraja wazazi wetu kwa upendo na asilimia chache ya tukipatacho ili maisha yetu yawe na baraka.

Mama unaweza ukamtumia doti mbili za khanga na akakuombea dua na baraka kwa mwenyezi Mungu ila unaweza kumnunulia kimada wako Iphone 6 na akakuomba tena umnunulie na airtime pamoja na Brazilian Wig,sababu wamejaa laana na ndio wanaovunja ndoa za watu kila uchwao.

Kama upo kwenye ndoa basi hakikisha unapata baraka toka kwa mwanamke bora ambaye ni mkeo sababu yeye ndio kila kitu katika maisha yako kisha unapata baraka za wazazi sababu ndio nguzo bora ya maisha yako.

One of the greatest titles in the world is parent, and one of the biggest blessings in the world is to have parents to call mom and dad
 
Ujumbe mzuri Sana,ila kiukweli ukiwajali wazazi wako,huwi na maisha ya dhiki
 
Mm furaha yangu ni kuwasaidia wazazi wangu....nlipokuwa chuo nlimuomba sana Mungu anipe kazi hata km ina mshahara mdogo ... ili tu niwasaidie wazazi wangu ambao wamenisomesha kwa tabu sana. Nlikua naumia sana nkifikiria kuajiriwa angalao uwe na refa naumia sana....mpaka ikanibidi niwe naweka sehemu ya boom langu kwenye investment fund (umoja fund-UTT) ili kusudi hata wasiponiajiri niwe na pakuanzia. Haya yote nlikua nikiyafanya ili tu mwisho wa siku niwasaidie wazazi wangu... nlipoanza kuwekeza nlipata confidence kwmb ntajiajiri kwa mtaji huo. Wakati huohuo nikisoma kwa bidii ili pia katika degree yangu nayosoma niwe knowledgeable na si bora degree...huku pia nikihakikisha GPA yangu inasoma vizuri. ... kitu ambacho nlijihisi ni UNIQUE kwangu ni Kwamba nlijisemea moyoni kuliko kumpa demu pesa zangu bora nimtumie BI MKUBWA ili nae ajione ana mtoto anaejielewa. Mungu si athumani baada tu ya kumaliza chuo....kutokana na matokeo yangu kuwa mazuri na kuwa knowledgeable kwenye degree nliyosomea kwangu mm kuitwa kwenye INTERVIEWS ilikua OBVIOUS. Kati ya interviews nlizofanya sehem 4 tofauti nliitiwa kazi sehem 3. So nlifanya tu kuchagua wapi pananifaa. Cha ajabu pia nlipata kazi ambayo mshahara wake ni MKUBWA sawa na mtu mwenye experience au hata zaidi (kwa level yangu )...vitu vyote ambavyo nlitamani kuwafanyia wazazi wangu nlifanya bila kuchelewa...nikiwa na miezi miwili kazini. .. ninachotaka kasema hapa sio kujisema mimi wala kujisifia ila nataka mjue kuwa SIKU ZOTE UKIWA NA NIA NJEMA KWA WAZAZI WAKO MUNGU HACHELEWI KUKUFUNGULIA MILANGO YA MAFANIKIO...naamini mtakua mmenipata vzur.
 
Mm furaha yangu ni kuwasaidia wazazi wangu....nlipokuwa chuo nlimuomba sana Mungu anipe kazi hata km ina mshahara mdogo ... ili tu niwasaidie wazazi wangu ambao wamenisomesha kwa tabu sana. Nlikua naumia sana nkifikiria kuajiriwa angalao uwe na refa naumia sana....mpaka ikanibidi niwe naweka sehemu ya boom langu kwenye investment fund (umoja fund-UTT) ili kusudi hata wasiponiajiri niwe na pakuanzia. Haya yote nlikua nikiyafanya ili tu mwisho wa siku niwasaidie wazazi wangu... nlipoanza kuwekeza nlipata confidence kwmb ntajiajiri kwa mtaji huo. Wakati huohuo nikisoma kwa bidii ili pia katika degree yangu nayosoma niwe knowledgeable na si bora degree...huku pia nikihakikisha GPA yangu inasoma vizuri. ... kitu ambacho nlijihisi ni UNIQUE kwangu ni Kwamba nlijisemea moyoni kuliko kumpa demu pesa zangu bora nimtumie BI MKUBWA ili nae ajione ana mtoto anaejielewa. Mungu si athumani baada tu ya kumaliza chuo....kutokana na matokeo yangu kuwa mazuri na kuwa knowledgeable kwenye degree nliyosomea kwangu mm kuitwa kwenye INTERVIEWS ilikua OBVIOUS. Kati ya interviews nlizofanya sehem 4 tofauti nliitiwa kazi sehem 3. So nlifanya tu kuchagua wapi pananifaa. Cha ajabu pia nlipata kazi ambayo mshahara wake ni MKUBWA sawa na mtu mwenye experience au hata zaidi (kwa level yangu )...vitu vyote ambavyo nlitamani kuwafanyia wazazi wangu nlifanya bila kuchelewa...nikiwa na miezi miwili kazini. .. ninachotaka kasema hapa sio kujisema mimi wala kujisifia ila nataka mjue kuwa SIKU ZOTE UKIWA NA NIA NJEMA KWA WAZAZI WAKO MUNGU HACHELEWI KUKUFUNGULIA MILANGO YA MAFANIKIO...naamini mtakua mmenipata vzur.

ubarikiwe mkuu, najifunza sana kutoka kwako. nami pia nataka niwatendee wema wazazi wangu kwa kila liwezekanalo.
 
Tumia dakika chache kufanya uamuzi na siku nyingi kufanya utafiti.Wanaume wengi wanaongoza kwa kuhonga huwa na mkono mfupi wa kuhudumia familia zao pamoja na kuwajali wazazi wao.

Ni kazi rahisi kumkuta mwanaume anakunywa pombe bar ya Tsh 200,000/- kwa usiku mmoja na mama yake mzazi ana pair mbili za kitenge bila kusahau wazazi hawana uwezo hata wa kununua Kg ya nyama,ila ni kazi rahisi sana kumpangia mwanamke kimada chumba na kumnunulia gari kimada wakati familia yako inalalia mihogo ama viporo

Nitajie mtu anayemtolea Mungu fungu la kumi ambaye hana mafanikio katika maisha yake ? Nionyeshe kijana yeyote ambaye huwatumia wazazi wake pesa za matumizi ya nyumbani ambaye hajastawi katika maisha bora na yenye tija ?Kila palipo na baraka ya wazazi pana hazina ya mafanikio daima.

Jitahidi mara nyingi kuwapa wazazi faraja ili wakunenee maneno yenye baraka na hazina ya furaha yako katika maisha yako.Manung'uniko huleta laana katika maisha ya mwandamu na maneno ya baraka huleta mafanikio katika maisha .Ni wakati sahihi wa kuwapa faraja wazazi wetu kwa upendo na asilimia chache ya tukipatacho ili maisha yetu yawe na baraka.

Mama unaweza ukamtumia doti mbili za khanga na akakuombea dua na baraka kwa mwenyezi Mungu ila unaweza kumnunulia kimada wako Iphone 6 na akakuomba tena umnunulie na airtime pamoja na Brazilian Wig,sababu wamejaa laana na ndio wanaovunja ndoa za watu kila uchwao.

Kama upo kwenye ndoa basi hakikisha unapata baraka toka kwa mwanamke bora ambaye ni mkeo sababu yeye ndio kila kitu katika maisha yako kisha unapata baraka za wazazi sababu ndio nguzo bora ya maisha yako.

One of the greatest titles in the world is parent, and one of the biggest blessings in the world is to have parents to call mom and dad
ubarikiwe mkuu.
 
Back
Top Bottom