Hii ni siku ambayo nilidhalilishwa sana kwenye Kadamnasi. Sikuwahi isahau

Hicho kilinge kipo wapi Tukalipize kisasi....Sie wengine Tushakoswa risasi unasema Ndoo tuu.
 
Huu mchezo kwanza unachezwa kwa maneno. Sababu ni wa kutumia akili, maneno hutumika kumfedhehesha opponent.
 
Wewe kilichokufunga sio kwamba hujui bali yale maneno ya shombo,na kwakua alikua tayari kashakutoa kwenye mchezo kweli angekupiga super
 
Hahahaha mkuu kwenye mabewe lugha ya matusi ni kawaida sana na hua na enjoy sana kuangalia pambano ambalo magwiji wakicheza halafu wawe na maneno ya shombo

Kuna siku nilienda kijiweni nikakuta kadogo kanawafunga wazee halafu kanachezea draft mkono wa kushoto. Nilipofika tu nikakuta kuna mzee ndio anatolewa nje baada ya kufungwa na hicho kidogo.

Mzee wakati ananyanyuka dogo akamuambia mzee hizo goli nilizokupiga hutakiwi kukaa hapa kanawe kwanza ndio uje tena

Daah wakati nastaajabu kuona mtoto akimtolea maneno ya shombo mdingi, kuna mzee mwingine akaingia, yule mzee aliyetoka akawa anampa kete kwa kumpisha mzee mwenzake ili aendelee kucheza na yule dogo ambaye anawasumbua, yule mzee akamjibu mzee mwenzake kua weka kete chini usinipe mkononi usije ukaniambukiza gono ulilopewa na huyo mtoto

Mzee akaendelea kucheza, yule dogo akampiga force kingi mzee halafu dogo akamuambia yule mzee "hebu visha hiyo kingi kabisa maana maradhi ni mengi"
nimecheka sanaaaaa hii aiseeeh.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Nimecheka sana ,Ila wadau jifunzeni kupuuzia maneno ambayo hayakupunguzii uhai,izo ni technique tu za mpinzani wako kukuogopesha ushindwe ,relax and keep play...😂😂😂
 
Nlishawahi kuona jamaa kamng'ang'ania mtu shingo watu wanapambana kumwachanisha....nakuja ambiwa chanzo ni draft jamaa aliambiwa anapenda sana kufumuliwa malinda maana anapigwa mabao hakati tamaa anategesha tena makalio kama anavyofanyaga mkewe...hapo jamaa alishindwa vumilia.maana mshindi alikuwa anasema mimi ndo dume la mbegu ntawapanda familia yako yote ....mkeo na leo wewe nakuona ulivyo mtamu. Hapo jamaa alimrukia jamaa shingoni....
😂😂Kwa kwel hapa lazima tuzichape...
 
Sio draft tu, kwenye sports nyingi unaweza kucheza na psychology ya mtu ukamtoa mchezoni.

Hata kwenye boxing maneno huwa yapo sana ya kukera na yanamfanya mtu ana panic anaishia kupigwa.

Unakumbuka Zidane na Materazzi kwenye fainali ya World Cup 2006? Ndio mifano kama hiyo. Maneno ya chinichini yakamtoa Zidane mchezoni akamlamba mwenzake kwicha, kapewa red Ufaransa wamebaki pungufu mwisho wa siku wakapoteza fainali.
 
Mkuu hakuna michezo yenye ku hitaji uvumilivu kama huo, na kupotezea watu, hasa kiringe kikiwa na Wazee wa swahili waweza jitafutia murder case.

Sent using Jamii Forums mobile app
Pale nje ya Shule ya Sekondari Kambangwa karibu na mahakama ya Kinondoni, kuna kijiwe cha kahawa cha Msisiri. 2002 nilijichanganya kukalia benchi nitest viwango vyangu nikaona na wa upande wa pili naye kainuka, hataki kucheza na mimi. Wenzake (kisanii, maana najua wanaujua mchezo wao) wakamuuliza, vipi bingwa mbona unainuka, akawajibu maishani mwake hajawahi kucheza disco toto, yaani mimi sio size yake.

Basi wakamuita mtoto mdogo mpita njia eti ndio akae acheze na mimi. Njoo cheza na mwenzako :D :D, dah. Ile kamecheza tu kete ya kwanza, nikasikia wooote kwa pamoja wanasema "heko", nikicheza mimi utasikia "mmmh, bora ulivyosimama...ulikuwa na kesi ya mauaji. Yule dogo alinifunga asee, maana si kwa mbeleko zile
 
Nliacha kabisa kucheza draft.kipindi cha nyuma uncle wangu mmoja alinifundisha draft nikawa vizuri sana.kiukweli niliweza kuwagonga gonga baadhi ya watu kiroho mbaya.

Maeneo flani Kino clan kulikuwa na bench nje ya nyumbani kwa jamaa yangu.siku hiyo nikaona nami ni socialize na wananzengo.walikuwepo wazee na vijana na kakijana kamoja kana ulumbi wa maneno.

Baada ya kumfunga mtu super kakaanza maneno ya shombo "mi sijaona mtu hapa...naona tu mnapuyanga puyanga hakuna anayejua draft"

Wale wengine wakawa wanajiuma uma.nikaomba nikae kwenye bench...kajamaa kakacheka sana...mpaka machozi yakakatoka.tena kwa kebehi.

"Daaah yaani wewe poyoyo ndo unataka kuja kupakaza makamasi na udenda kwenye kete?" Nlikwazika maana kajamaa kenyewe ni namba moja hasa.

Tukaanza, kakanambia nichague kuanza kusukuma kete au kaanze kenyewe.nikasukuma...kakatikisa kichwa kwa huzuni.

"Kweli akili si mwili, unacheza kibwege sana kama ndondocha...we unajua draft kweli?au unasukuma tu kete kama ulivyokuwa unamwona huyo mzee aliyetoka?"

Kalinikwaza sana kajamaa ila nikanyamaza.nikataka sukuma kete flani kakanishika mkono.

" Hiyo usisukume...ntakupiga super" nikakaambia "please dont touch me huku nmekunja sura..."

"Aaah wakusoma usiwe mkali...simba mkali na anazaa utakuwa wewe" hapo kweli kalinila kete mbili.huku kanacheka kwa kebehi.

Nikataka sukuma nyingine kakanambia..."big usisukume hiyo ntakupiga super ujue" nikasukuma.kakanila tatu... Hapo hasira zinakipanda kiasi.maana nikawa sielewi inakuaje nacheza kama boya.

Tumecheza kidogo nikataka sukuma nyingine....kakatikisa kichwa..."kweli nmeamini ukubwa wa mwili si wingi wa akili...yaani nyie wote ndo mmeniletea huyu ndondocha ananuka maziwa aje kucheza na mwanaume?kwa nini mnanikosea heshima?oneni anavyo bong'oa kwa furaha kabisa nifanye yangu"

Hapo sikuvumilia nilimgonga kichwa akaanguka chini akawa kama amezima hivi.jamaa wakaniwahi....nlikuwa natetemeka kwa hasira na ghadhabu.wazee wakanishika na kunisihi niwe mvumilivu. kama dk moja kajamaa kakawa kanakohoa wakakamsha na kukakalisha kwenye kiti...kametoa macho kama ngumi.

"Amenigonga na nini?" Wakaanza kucheka kwa lile swali...mzee mmoja akajibu " ndoo hiyo fala wewe unadhani wote wnapenda maneno ya shombo...tunakwambia kila siku acha shombo huelewi"

Kajamaa kakatikisa kichwa ili ubongo urudi sehemu yake nadhani ulishake kidogo.halafu kakasikilizia kakaona bado ubongo haujakaa sawa.kakatikisa na kugonga gonga pembeni ya kichwa.halafu kakanicheck na kukenua meno.

" Huu mchezo hautaki hasira...unataka akili" hapo jamaa waliniwahi kunikamata...na kuniondoa maana waliniona kabisa naanza kuchemka...

mpaka leo nahisi kale kajamaa kalikuwa kachawi kangeweza nitafutia kesi ya kijinga tu.

Sikuwahi cheza tena draft hadharani. Nmepita sehemu nmekuta watu wanacheza nikasimama tu kutizama nmemkuta mzee ambaye anaweza kuwa baba yake yule jamaa....ana maneno machafu.nmesimama anauliza "na wewe unataka kulawitiwa?" Hawa wengine wote tayari hawana marinda nmewachana chana" niligeuka na kuondoka nisije pata murder case bure.
HAHAHAHAHAHHAHAH HAHAHAHAHAHHA HAHAHAHAHAHHA

DAAAAH, nimecheka sana aisee..
Maana nasoma story hunu navuta picha jinsi tukio lilivyokuwa...
 
Kwa
Nliacha kabisa kucheza draft.kipindi cha nyuma uncle wangu mmoja alinifundisha draft nikawa vizuri sana.kiukweli niliweza kuwagonga gonga baadhi ya watu kiroho mbaya.

Maeneo flani Kino clan kulikuwa na bench nje ya nyumbani kwa jamaa yangu.siku hiyo nikaona nami ni socialize na wananzengo.walikuwepo wazee na vijana na kakijana kamoja kana ulumbi wa maneno.

Baada ya kumfunga mtu super kakaanza maneno ya shombo "mi sijaona mtu hapa...naona tu mnapuyanga puyanga hakuna anayejua draft"

Wale wengine wakawa wanajiuma uma.nikaomba nikae kwenye bench...kajamaa kakacheka sana...mpaka machozi yakakatoka.tena kwa kebehi.

"Daaah yaani wewe poyoyo ndo unataka kuja kupakaza makamasi na udenda kwenye kete?" Nlikwazika maana kajamaa kenyewe ni namba moja hasa.

Tukaanza, kakanambia nichague kuanza kusukuma kete au kaanze kenyewe.nikasukuma...kakatikisa kichwa kwa huzuni.

"Kweli akili si mwili, unacheza kibwege sana kama ndondocha...we unajua draft kweli?au unasukuma tu kete kama ulivyokuwa unamwona huyo mzee aliyetoka?"

Kalinikwaza sana kajamaa ila nikanyamaza.nikataka sukuma kete flani kakanishika mkono.

" Hiyo usisukume...ntakupiga super" nikakaambia "please dont touch me huku nmekunja sura..."

"Aaah wakusoma usiwe mkali...simba mkali na anazaa utakuwa wewe" hapo kweli kalinila kete mbili.huku kanacheka kwa kebehi.

Nikataka sukuma nyingine kakanambia..."big usisukume hiyo ntakupiga super ujue" nikasukuma.kakanila tatu... Hapo hasira zinakipanda kiasi.maana nikawa sielewi inakuaje nacheza kama boya.

Tumecheza kidogo nikataka sukuma nyingine....kakatikisa kichwa..."kweli nmeamini ukubwa wa mwili si wingi wa akili...yaani nyie wote ndo mmeniletea huyu ndondocha ananuka maziwa aje kucheza na mwanaume?kwa nini mnanikosea heshima?oneni anavyo bong'oa kwa furaha kabisa nifanye yangu"

Hapo sikuvumilia nilimgonga kichwa akaanguka chini akawa kama amezima hivi.jamaa wakaniwahi....nlikuwa natetemeka kwa hasira na ghadhabu.wazee wakanishika na kunisihi niwe mvumilivu. kama dk moja kajamaa kakawa kanakohoa wakakamsha na kukakalisha kwenye kiti...kametoa macho kama ngumi.

"Amenigonga na nini?" Wakaanza kucheka kwa lile swali...mzee mmoja akajibu " ndoo hiyo fala wewe unadhani wote wnapenda maneno ya shombo...tunakwambia kila siku acha shombo huelewi"

Kajamaa kakatikisa kichwa ili ubongo urudi sehemu yake nadhani ulishake kidogo.halafu kakasikilizia kakaona bado ubongo haujakaa sawa.kakatikisa na kugonga gonga pembeni ya kichwa.halafu kakanicheck na kukenua meno.

" Huu mchezo hautaki hasira...unataka akili" hapo jamaa waliniwahi kunikamata...na kuniondoa maana waliniona kabisa naanza kuchemka...

mpaka leo nahisi kale kajamaa kalikuwa kachawi kangeweza nitafutia kesi ya kijinga tu.

Sikuwahi cheza tena draft hadharani. Nmepita sehemu nmekuta watu wanacheza nikasimama tu kutizama nmemkuta mzee ambaye anaweza kuwa baba yake yule jamaa....ana maneno machafu.nmesimama anauliza "na wewe unataka kulawitiwa?" Hawa wengine wote tayari hawana marinda nmewachana chana" niligeuka na kuondoka nisije pata murder case bure.
Kwa kifupi huna roho wala akili ya kuhimili changamoto za kimichezo au za watu wengine. Kule JKT wanatukania hadi mama yako.

Halafu inaonekana una kichwa kikubwa.
 
Sana....wadada wengi husema hivyo....kuwa nina kichwa kikubwa wana enjoy..


Kwa

Kwa kifupi huna roho wala akili ya kuhimili changamoto za kimichezo au za watu wengine. Kule JKT wanatukania hadi mama yako.

Halafu inaonekana una kichwa kikubwa.
 

Similar Discussions

57 Reactions
Reply
Back
Top Bottom