Polycarp Mdemu
Senior Member
- Jun 2, 2019
- 165
- 209
HII NI MARA YA PILI BASILIKA LA SOFIA HAGIA KUBADILISHWA KUWA MSIKITI.
Mara ya Kwanza HAGIA SOPHIA lilibadilishwa kuwa msikiti mwaka 1453 na halafu kuwa makumbusho kuanzia mwaka 1934 mpaka mwaka huu tulipojuzwa litakuwa Msikiti tena.
HAGIA SOPHIA ni jina la Kigiriki la kanisa kubwa mjini Istanbul - Konstantinopoli huko Uturuki, Jina linatoka katika Kigiriki " Ἅγια Σοφία" likimaanisha (hekima takatifu) na kwa Kituruki linaitwa "Ayasofya".
Katika Historia ujenzi wa kanisa hili ulianzishwa mwaka 532 B.K na Kaisari Justiniani I aliyekuwa mtawala wa Roma ya Mashariki au tuite tu Ufalme wa Byzanti
Lengo la Jamaa huyu (Kaizari) Alitaka kuwa na kanisa (Jengo) kubwa kuliko yote duniani akafaulu kwa sababu Hagia Sofia ilikuwa ukumbi mkubwa duniani hadi mwaka 1520.
Hagia Sophia lilikamilika tu baada ya miaka mitano na Kaizari Justiniani alipoingia mara ya kwanza ndani Alisema:
"Suleimani nimekushinda", hapa alimlenga mfalme Suleimani wa Israeli ya Kale aliyejenga hekalu la Yerusalemu
Mwaka 1453 Waturuki Waislamu waliteka mji wa Konstantinopoli na kufanya mji mkuu wa Dola la Osmani
Hapo Hagia Sofia likabadilishwa kuwa msikiti na Waturuki wakatamka jina la kigiriki kama "Ayasofya".
Jengo la kanisa likaongezwa minara minne ya mtindo wa Kiislamu
Mwaka 1934 Baada ya anguko la Waosmani katika vita kuu ya kwanza ya dunia kiongozi wa taifa Kemal Atatürk akaamuru jengo liwe makumbusho, Na likawekwa kwenye Orodha ya UNESCO kama moja ya Jengo ambalo ni "Urithi Wa Dunia"
Lakini Hapo Jana Rais wa Uturuki Recep Tayyip Erdogan Aliamuru kwamba Basilica La Hagia Sophia litatumika kama msikiti tena, kufuatia uamuzi kutoka kwa Baraza la Nchi, Na litafunguliwa rasmi kuanza kutumika hapo Tarehe 24 Julai mwaka huu
Mkubwa Au Baba wa Kanisa la Waorthodox, Ambao Ni Wamiliki Halali wa Jengo hili, Aligusia Uamuzi huu wa Serikal .....Patriach Bartholomew Alisema "Hagia Sophia Si tu la wamiliki wa Sasa, Ni kanisa la watu wa Ulimwengu wote, Watu wa Uturuki wana jukumu kubwa na heshima ya kufanya umoja wa jumba hili la ajabu," alisema, na kuongeza kuwa kama jumba la kumbukumbu ni kama "mahali pa ishara pa kukutana, mazungumzo, mshikamano na uelewano kati ya Ukristo na Uislamu"
Pia Patriach wa Waorthodox Wa Jiji La Moscow alisema "Kuibadilisha Hagia Sophia Kuwa Msikiti ni Dharau na Tishio kwa Wakristu"
Pia Papa Francis katika Misa ya Jumapili alisema "Ninafikiria kuhusu Hagia Sophia na nina huzuni sana".........UN pamoja na UNESCO wameonyesha kutounga mkono Mkono maamuzi haya, Lakini Raisi wa Uturuki Amedai asipofuata Maamuzi yao wenyewe inaana wazi hawapo huru juu ya Mali za nchi yao.
Kila Laheri Kwa HAGIA SOPHIA (THE MASTER PIECE) katika kazi yake mpya.... Hakika Hata wanaolitumia, Wanajua nani ni Mmiliki.
Polycarp Mdemu
Mara ya Kwanza HAGIA SOPHIA lilibadilishwa kuwa msikiti mwaka 1453 na halafu kuwa makumbusho kuanzia mwaka 1934 mpaka mwaka huu tulipojuzwa litakuwa Msikiti tena.
HAGIA SOPHIA ni jina la Kigiriki la kanisa kubwa mjini Istanbul - Konstantinopoli huko Uturuki, Jina linatoka katika Kigiriki " Ἅγια Σοφία" likimaanisha (hekima takatifu) na kwa Kituruki linaitwa "Ayasofya".
Katika Historia ujenzi wa kanisa hili ulianzishwa mwaka 532 B.K na Kaisari Justiniani I aliyekuwa mtawala wa Roma ya Mashariki au tuite tu Ufalme wa Byzanti
Lengo la Jamaa huyu (Kaizari) Alitaka kuwa na kanisa (Jengo) kubwa kuliko yote duniani akafaulu kwa sababu Hagia Sofia ilikuwa ukumbi mkubwa duniani hadi mwaka 1520.
Hagia Sophia lilikamilika tu baada ya miaka mitano na Kaizari Justiniani alipoingia mara ya kwanza ndani Alisema:
"Suleimani nimekushinda", hapa alimlenga mfalme Suleimani wa Israeli ya Kale aliyejenga hekalu la Yerusalemu
Mwaka 1453 Waturuki Waislamu waliteka mji wa Konstantinopoli na kufanya mji mkuu wa Dola la Osmani
Hapo Hagia Sofia likabadilishwa kuwa msikiti na Waturuki wakatamka jina la kigiriki kama "Ayasofya".
Jengo la kanisa likaongezwa minara minne ya mtindo wa Kiislamu
Mwaka 1934 Baada ya anguko la Waosmani katika vita kuu ya kwanza ya dunia kiongozi wa taifa Kemal Atatürk akaamuru jengo liwe makumbusho, Na likawekwa kwenye Orodha ya UNESCO kama moja ya Jengo ambalo ni "Urithi Wa Dunia"
Lakini Hapo Jana Rais wa Uturuki Recep Tayyip Erdogan Aliamuru kwamba Basilica La Hagia Sophia litatumika kama msikiti tena, kufuatia uamuzi kutoka kwa Baraza la Nchi, Na litafunguliwa rasmi kuanza kutumika hapo Tarehe 24 Julai mwaka huu
Mkubwa Au Baba wa Kanisa la Waorthodox, Ambao Ni Wamiliki Halali wa Jengo hili, Aligusia Uamuzi huu wa Serikal .....Patriach Bartholomew Alisema "Hagia Sophia Si tu la wamiliki wa Sasa, Ni kanisa la watu wa Ulimwengu wote, Watu wa Uturuki wana jukumu kubwa na heshima ya kufanya umoja wa jumba hili la ajabu," alisema, na kuongeza kuwa kama jumba la kumbukumbu ni kama "mahali pa ishara pa kukutana, mazungumzo, mshikamano na uelewano kati ya Ukristo na Uislamu"
Pia Patriach wa Waorthodox Wa Jiji La Moscow alisema "Kuibadilisha Hagia Sophia Kuwa Msikiti ni Dharau na Tishio kwa Wakristu"
Pia Papa Francis katika Misa ya Jumapili alisema "Ninafikiria kuhusu Hagia Sophia na nina huzuni sana".........UN pamoja na UNESCO wameonyesha kutounga mkono Mkono maamuzi haya, Lakini Raisi wa Uturuki Amedai asipofuata Maamuzi yao wenyewe inaana wazi hawapo huru juu ya Mali za nchi yao.
Kila Laheri Kwa HAGIA SOPHIA (THE MASTER PIECE) katika kazi yake mpya.... Hakika Hata wanaolitumia, Wanajua nani ni Mmiliki.
Polycarp Mdemu