Hii ni Kweli Utamaduni wa Zanzibar ni kwa Waislam? Kanisa ni Ukafiri? Elimu kubaguana

nngu007

JF-Expert Member
Aug 2, 2010
15,862
5,797
Habari za Mzalendo huko Visiwani wanaona kuwa na Kanisa ni Sawa Sawa na kuwa na Bar na Clubs na wanaita ni Ukafiri. Sasa Huku Bara Tuna Utamaduni wetu na Dini Zetu, Kuna Msukuma ambaye ni Mkristo na ambaye in Mwislamu na wote Utamaduni wao ni Wa Kisukuma Dini ndio Tofauti...

Wao Wazanzibari Utamaduni Wao Ndio Dini Yao UISLAMU kweli tutafika?
Soma tahariri yao hapa chini;

"Asilimia kubwa Zanzibar 99% ni waislamu, na ukiangalia utamaduni wetu ni wakislamu,na tumeona kuwa kwamba wazanzibar hawataki kabisa kuona mambo ya kikafiri ambayo yanaweza kupotoa maadili yetu na dini kama vile bar na makanisa na club.
Lakini mimi nitaelezea ufahamu wangu wa maadili ya kislamu ambayo tukiacha bar makanisa na clubs ambazo hapa Zanzibar zinaweza kuharibu maadili yetu ya dini na kiutamaduni,kwa mfano mfumo wetu kwa mfano katika elimu kazi mikusanyiko ya watu kama harusi n.k . Tunafahamu kuwa dini yetu ya kislamu inakataza sehemu kukusanyika gender mbili ambazo ni male and female kuwa pamoja,labda kwa zarura.
Leo nitadokezea Mfumo tunaotumia katika maskuli yetu Zanzibar sio mfumo mzuri kwa waislamu, katika maskuli yetu kumekuwa na mchanganyiko wa gender mbili male and female,tena wanasoma hadi kubalekh wakiwa katika mchanganyiko huo,jee hatuoni kuwa kwa dini yetu ya kislamu sio vizuri hili ?
Hatuoni yakuwa mchanganyiko huku ndio kunakuwa na vishawishi ambavyo vitawafanya waingie katika vitendo viovu ? Dini yetu ya kislamu imesema tusome hata uwende china hata iwe elimu ya dunia lakini soma,jee katika mfumo huu kwa waislamu ni right ?
Pia katika maadili yetu ya Zanzibar na tamaduni Watanganyika/Watanzania bara wanasema kuwa zinawakosesha wanawake kupata fursa katika sula la elimu hii inachangia kuzoefesha maendeleo yetu zanzibar,mi kwa kuangalia ni hasa pale wanapomalizikia form 2 au 4 au 6,hawapewi fursa ya kuendelea kutoka na hofu za wazee watoto kuja kuharibikiwa ukubwani wakati wanaona washa balekh lakini hawaoni yakuwa huko walikotoka ni sawa na huko wanakotaka kuenda mix gender jee wazee hawaoni hili ? Na serikali kwa ujumla jee limechukua hatua ?
Katika sehemu za kazi,usafiri ,sehemu za biashara zote hizi ni mchanganyiko wa wanawake na wanaume,dini yetu ya kislamu inaruhusu m/ke na m/ke kuwa sehemu moja katika mchanganyiko ? Kwa kweli ni masuala ya kujiuliza na kuangalia hizo situation tulizonazo kwa mfumo wetu wa dini kama ni haki na ni sawa kulinda utamaduni wa kizanzibari pamoja na kuheshimu na kufata dini yetu ya kislam.
Pia kwa walimu wa skuli,pamoja na madarasat ukiangalia pia wanafunzi wanapofanya makosa wanapokuwa darasani wakiwa hali yakuwa wana funzi hao ni wari kabisa balekh,na mwalimu wa kiume tena kijana anakamata nguo zake hadi ile ya ndani na kuishika bara bara na kumchapa fimbo jee hii ni sawa kwa utamaduni wetu na dini yetu ya kislamu ?
Hivi hatuwezi kuwafunza watoto wetu bila ya kutumia fimbo na hasa motto ambaye ni mkubwa asiyepungua miaka kumi tano ? Inamaana kuwa mototo hawezi kusoma bila ya fimbo kumchapa nayo makalioni ? kweli haya ndio tamaduni zetu jamani kwa makosa kama haya ?
Skuli zetu kuweka jinsia mbili tofauti,wanawake na wanaume jee ni sawa ? Vyuo vikuu pia mix gender ni sawa? Katika sehemu za kazi ni sawa ? Na kama sio sawa kwa mfumo huu na tukiangalia dini yetu ya kislamu jee munaishauri vipi jamii pamona na viongozi ? Pengine mimi upeo wangu mdogo,hebu nichambulieni."
 
Habari za Mzalendo huko Visiwani wanaona kuwa na Kanisa ni Sawa Sawa na kuwa na Bar na Clubs na wanaita ni Ukafiri. Sasa Huku Bara Tuna Utamaduni wetu na Dini Zetu, Kuna Msukuma ambaye ni Mkristo na ambaye in Mwislamu na wote Utamaduni wao ni Wa Kisukuma Dini ndio Tofauti...

Wao Wazanzibari Utamaduni Wao Ndio Dini Yao UISLAMU kweli tutafika?
Soma tahariri yao hapa chini;

"Asilimia kubwa Zanzibar 99% ni waislamu, na ukiangalia utamaduni wetu ni wakislamu,na tumeona kuwa kwamba wazanzibar hawataki kabisa kuona mambo ya kikafiri ambayo yanaweza kupotoa maadili yetu na dini kama vile bar na makanisa na club.
Lakini mimi nitaelezea ufahamu wangu wa maadili ya kislamu ambayo tukiacha bar makanisa na clubs ambazo hapa Zanzibar zinaweza kuharibu maadili yetu ya dini na kiutamaduni,kwa mfano mfumo wetu kwa mfano katika elimu kazi mikusanyiko ya watu kama harusi n.k . Tunafahamu kuwa dini yetu ya kislamu inakataza sehemu kukusanyika gender mbili ambazo ni male and female kuwa pamoja,labda kwa zarura.
Leo nitadokezea Mfumo tunaotumia katika maskuli yetu Zanzibar sio mfumo mzuri kwa waislamu, katika maskuli yetu kumekuwa na mchanganyiko wa gender mbili male and female,tena wanasoma hadi kubalekh wakiwa katika mchanganyiko huo,jee hatuoni kuwa kwa dini yetu ya kislamu sio vizuri hili ?

Hatuoni yakuwa mchanganyiko huku ndio kunakuwa na vishawishi ambavyo vitawafanya waingie katika vitendo viovu ? Dini yetu ya kislamu imesema tusome hata uwende china hata iwe elimu ya dunia lakini soma,jee katika mfumo huu kwa waislamu ni right ?
Pia katika maadili yetu ya Zanzibar na tamaduni Watanganyika/Watanzania bara wanasema kuwa zinawakosesha wanawake kupata fursa katika sula la elimu hii inachangia kuzoefesha maendeleo yetu zanzibar,mi kwa kuangalia ni hasa pale wanapomalizikia form 2 au 4 au 6,hawapewi fursa ya kuendelea kutoka na hofu za wazee watoto kuja kuharibikiwa ukubwani wakati wanaona washa balekh lakini hawaoni yakuwa huko walikotoka ni sawa na huko wanakotaka kuenda mix gender jee wazee hawaoni hili ? Na serikali kwa ujumla jee limechukua hatua ?
Katika sehemu za kazi,usafiri ,sehemu za biashara zote hizi ni mchanganyiko wa wanawake na wanaume,dini yetu ya kislamu inaruhusu m/ke na m/ke kuwa sehemu moja katika mchanganyiko ? Kwa kweli ni masuala ya kujiuliza na kuangalia hizo situation tulizonazo kwa mfumo wetu wa dini kama ni haki na ni sawa kulinda utamaduni wa kizanzibari pamoja na kuheshimu na kufata dini yetu ya kislam.
Pia kwa walimu wa skuli,pamoja na madarasat ukiangalia pia wanafunzi wanapofanya makosa wanapokuwa darasani wakiwa hali yakuwa wana funzi hao ni wari kabisa balekh,na mwalimu wa kiume tena kijana anakamata nguo zake hadi ile ya ndani na kuishika bara bara na kumchapa fimbo jee hii ni sawa kwa utamaduni wetu na dini yetu ya kislamu ?
Hivi hatuwezi kuwafunza watoto wetu bila ya kutumia fimbo na hasa motto ambaye ni mkubwa asiyepungua miaka kumi tano ? Inamaana kuwa mototo hawezi kusoma bila ya fimbo kumchapa nayo makalioni ? kweli haya ndio tamaduni zetu jamani kwa makosa kama haya ?
Skuli zetu kuweka jinsia mbili tofauti,wanawake na wanaume jee ni sawa ? Vyuo vikuu pia mix gender ni sawa? Katika sehemu za kazi ni sawa ? Na kama sio sawa kwa mfumo huu na tukiangalia dini yetu ya kislamu jee munaishauri vipi jamii pamona na viongozi ? Pengine mimi upeo wangu mdogo,hebu nichambulieni."
Nadhani ukweli halisi ni huo mstari wa mwisho wa blue, na kama sio basi ni vema utafute utaratibu wa kujenga kadunia kako ambako utaweza ku practice hayo hapo juu yenye red
Kama ndiyo UISLAMU KAZI MNAYO KWELI KWELI
 
Jee 99% ni waislam, sasa wakiristo wanafasi gani ile? lkn mbona huku bara licha ya waislam kuwa wengi lkn ukiangaliwa waajiriw wengi sana, wakuu wa utawala ni wakiristo? wabunge wengi mno wakiristo? jee mfumo huu tuundie tume huru


MS you are out of context. Read it again between the lines and come with your comments. I like to see you commenting within the context maana mchango wako mara zote huwa ni wa muhimu katika kutoa fikra mbadala (mawazo ya upande wa pili) ila hapa soma tena ujadili hili la maada maana umetoa mtazamo mzuri ila nje kabisa la kinachotakiwa kujadiliwa
 
Wazanzibar wengi wanaamini kuwepo kwa watu kutoka bara haswa wakristo wanaweza kuharibu tamaduni zao ambazo wanaziita za Kiislamu; hivi uislamu ni utamaduni au dini? Lakini wapo wamiliki wa night club (Bhaa Style - Bwawani) hawa ni wazanzibari na waislamu; nafikiri wazanzibari wangeshughulika kwanza na hawa wazanzibari wanaoharibu jamii yao.
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom