Mlangaja
JF-Expert Member
- Nov 2, 2010
- 579
- 218
Nataka niwepe ushauri wanaccm wenzangu. Kuna mambo mengi sana ya kipuuzi ambayo yanaendelea kufanywa na serikali yetu kwa sasa. Mambo haya yatatufanya tukose kura mwaka 2015 hasa sehemu zile ambazo chama chetu kimeweka ngome.
Mfano hapa Dodoma, kuna ujenzi wa barabara ambao unaendelea, kweli mtoto wangu ana miaka minne na miezi mitatu. Leo tukiwa kwenye pikipiki tulipokuwa tunapita maeneo ya Chamwino kaniambia, "Baba nani kaharibu bara bara?"
Kuna ujenzi wa barabara wa kipuuzi unaoendelea katika manispaaa ya Dodoma. Kwa hakika kwa ujenzi huu hatuna la kuwaambia wananchi siku zijazo. Mfano katika kata ya Changʼombe kuna diwani wa chama chetu alifariki siku za hivi karibuni. Naamini uchaguzi utakapoitishwa hatuna la kuwaambia wananchi.
Hivi ndiyo kusema tumeshindwa kabisa kuisimamia serikali? Hivi hata viongozi wa chama mnapopita na kuona ugoigoi huu unaendelea mnawaambia nini hawa wakurugenzi wa mkoa, wilaya na watendaji wa kata? Hivi kweli watendaji wa serikali wanawajibika kwenu? Au ndo mnakula nao? Hakika kwa utaratibu huu tutapoteza kila kitu kwani hatuna jema tena.
Hebu tuamke jamani, Angalieni jinsi fedha ya wananchi inavyohujumiwa. Mfano barabara ya kwenda st Gema, ule ni upuuzi umefanyika pale. Kifusi kimemwagwa halafu greda likasawazisha bila kushindia. Huu ni ugoigoi. Hebu tuamke bwana.
Mfano hapa Dodoma, kuna ujenzi wa barabara ambao unaendelea, kweli mtoto wangu ana miaka minne na miezi mitatu. Leo tukiwa kwenye pikipiki tulipokuwa tunapita maeneo ya Chamwino kaniambia, "Baba nani kaharibu bara bara?"
Kuna ujenzi wa barabara wa kipuuzi unaoendelea katika manispaaa ya Dodoma. Kwa hakika kwa ujenzi huu hatuna la kuwaambia wananchi siku zijazo. Mfano katika kata ya Changʼombe kuna diwani wa chama chetu alifariki siku za hivi karibuni. Naamini uchaguzi utakapoitishwa hatuna la kuwaambia wananchi.
Hivi ndiyo kusema tumeshindwa kabisa kuisimamia serikali? Hivi hata viongozi wa chama mnapopita na kuona ugoigoi huu unaendelea mnawaambia nini hawa wakurugenzi wa mkoa, wilaya na watendaji wa kata? Hivi kweli watendaji wa serikali wanawajibika kwenu? Au ndo mnakula nao? Hakika kwa utaratibu huu tutapoteza kila kitu kwani hatuna jema tena.
Hebu tuamke jamani, Angalieni jinsi fedha ya wananchi inavyohujumiwa. Mfano barabara ya kwenda st Gema, ule ni upuuzi umefanyika pale. Kifusi kimemwagwa halafu greda likasawazisha bila kushindia. Huu ni ugoigoi. Hebu tuamke bwana.