Hii ni kwa wana CCM tu

Mlangaja

JF-Expert Member
Nov 2, 2010
579
218
Nataka niwepe ushauri wanaccm wenzangu. Kuna mambo mengi sana ya kipuuzi ambayo yanaendelea kufanywa na serikali yetu kwa sasa. Mambo haya yatatufanya tukose kura mwaka 2015 hasa sehemu zile ambazo chama chetu kimeweka ngome.

Mfano hapa Dodoma, kuna ujenzi wa barabara ambao unaendelea, kweli mtoto wangu ana miaka minne na miezi mitatu. Leo tukiwa kwenye pikipiki tulipokuwa tunapita maeneo ya Chamwino kaniambia, "Baba nani kaharibu bara bara?"

Kuna ujenzi wa barabara wa kipuuzi unaoendelea katika manispaaa ya Dodoma. Kwa hakika kwa ujenzi huu hatuna la kuwaambia wananchi siku zijazo. Mfano katika kata ya Changʼombe kuna diwani wa chama chetu alifariki siku za hivi karibuni. Naamini uchaguzi utakapoitishwa hatuna la kuwaambia wananchi.

Hivi ndiyo kusema tumeshindwa kabisa kuisimamia serikali? Hivi hata viongozi wa chama mnapopita na kuona ugoigoi huu unaendelea mnawaambia nini hawa wakurugenzi wa mkoa, wilaya na watendaji wa kata? Hivi kweli watendaji wa serikali wanawajibika kwenu? Au ndo mnakula nao? Hakika kwa utaratibu huu tutapoteza kila kitu kwani hatuna jema tena.

Hebu tuamke jamani, Angalieni jinsi fedha ya wananchi inavyohujumiwa. Mfano barabara ya kwenda st Gema, ule ni upuuzi umefanyika pale. Kifusi kimemwagwa halafu greda likasawazisha bila kushindia. Huu ni ugoigoi. Hebu tuamke bwana.
 
Ww huwezi kuwa mwana ccm hata siku moja , waonekana kama vile unawatumikia ma bwana 2
 
Nataka niwepe ushauri wanaccm wenzangu. Kuna mambo mengi sana ya kipuuzi ambayo yanaendelea kufanywa na serikali yetu kwa sasa.
kijana unasema serikali yetu ni ya kipuuzi siyo!!! yaani imefikia hatua uansema haya wazi wazi bila kufanya utafiti?

Kama sisi ni wapuuzi kwa nini tumeshinda igunga tena kwa kishindo? kijana kama umekosa cha kuandika logout nenda nyumbani ukapumzike - kwanza wewe si mwana CCM hai kama unavyodai - nakuonya tena usirudie kuandika habari hizi za uchochezi na kuvuruga amani ya nchi. Utulivu tulionao inatakiwa tuudumishe hasa katika kipindi hiki ambacho tunaelekea kusherehekia miaka 50 ya uhuru wetu.

Mungu ibariki Tanzania - wananchi oyeeee!!!!! -- Uhuru oyeeeeee!!!!!! -
 
Ww huwezi kuwa mwana ccm hata siku moja , waonekana kama vile unawatumikia ma bwana 2

Hakika wewe ndio mwana-CCM kweli......

maana nilikuwa nashangaa huyu jamaa mwana CCM gani ambae hajui kuwa chama chake sasa ni sikio la kufa halisikii dawa yoyote....

Careless whispers................
 
kijana unasema serikali yetu ni ya kipuuzi siyo!!! yaani imefikia hatua uansema haya wazi wazi bila kufanya utafiti?

Kama sisi ni wapuuzi kwa nini tumeshinda igunga tena kwa kishindo? kijana kama umekosa cha kuandika logout nenda nyumbani ukapumzike - kwanza wewe si mwana CCM hai kama unavyodai - nakuonya tena usirudie kuandika habari hizi za uchochezi na kuvuruga amani ya nchi. Utulivu tulionao inatakiwa tuudumishe hasa katika kipindi hiki ambacho tunaelekea kusherehekia miaka 50 ya uhuru wetu.

Mungu ibariki Tanzania - wananchi oyeeee!!!!! -- Uhuru oyeeeeee!!!!!! -

Aha ha ha ha ha ha Jamaa unajifanya kama intelejensia vile biti kubwa kumbe hakuna kitu...jamaa kawapa ukweli manaleta hoja uharo hapa...
 
wana ccm hawapo bado wanasherehekea ushindi wa (kishindo?) igunga. Kuhusu wakati wa uchaguzi usijali watu watagawiwa fedha, chakula, na tshirt mtapata tu watanzania hicho ndicho wanachohitaji.
 
Aha ha ha ha ha ha Jamaa unajifanya kama intelejensia vile biti kubwa kumbe hakuna kitu...jamaa kawapa ukweli manaleta hoja uharo hapa...

hahahh..umeonae...biti la jamaa ni kama anamfaham mpaka chumba anacholala...eti anavuruga amani ya nchi
 
Ww huwezi kuwa mwana ccm hata siku moja , waonekana kama vile unawatumikia ma bwana 2
Akitoa ushauri basi anapoteza uhalali wa kuwa mwana CCM?????????? Mbona Prof Bana hujamtoa UCCM alivyo toa tathimini ya kuisha kwa CCM????????Brain Zero mwizi mkubwa wa maghamba!!!!!!!!!
 
Usiogope ndugu yangu lazima tushinde.Usijali sana mambo ya mabarabara sijui mahospitali na maelimu hayo ni maneno ya wapinzani.
Sisi CCM mambo yetu ni makofia,matisheti,maubwabwa na mangoma.
We unaongelea sana mabarabara au we ni CHADEMA umetumwa?
TUACHE NA RAHA ZETU SIE.
 
Nataka niwepe ushauri wanaccm wenzangu. Kuna mambo mengi sana ya kipuuzi ambayo yanaendelea kufanywa na serikali yetu kwa sasa. Mambo haya yatatufanya tukose kura mwaka 2015 hasa sehemu zile ambazo chama chetu kimeweka ngome.

Mfano hapa Dodoma, kuna ujenzi wa barabara ambao unaendelea, kweli mtoto wangu ana miaka minne na miezi mitatu. Leo tukiwa kwenye pikipiki tulipokuwa tunapita maeneo ya Chamwino kaniambia, "Baba nani kaharibu bara bara?"

Kuna ujenzi wa barabara wa kipuuzi unaoendelea katika manispaaa ya Dodoma. Kwa hakika kwa ujenzi huu hatuna la kuwaambia wananchi siku zijazo. Mfano katika kata ya Changʼombe kuna diwani wa chama chetu alifariki siku za hivi karibuni. Naamini uchaguzi utakapoitishwa hatuna la kuwaambia wananchi.

Hivi ndiyo kusema tumeshindwa kabisa kuisimamia serikali? Hivi hata viongozi wa chama mnapopita na kuona ugoigoi huu unaendelea mnawaambia nini hawa wakurugenzi wa mkoa, wilaya na watendaji wa kata? Hivi kweli watendaji wa serikali wanawajibika kwenu? Au ndo mnakula nao? Hakika kwa utaratibu huu tutapoteza kila kitu kwani hatuna jema tena.

Hebu tuamke jamani, Angalieni jinsi fedha ya wananchi inavyohujumiwa. Mfano barabara ya kwenda st Gema, ule ni upuuzi umefanyika pale. Kifusi kimemwagwa halafu greda likasawazisha bila kushindia. Huu ni ugoigoi. Hebu tuamke bwana.

Kijana epuka kutumia mimea korofi
 
Mtoa mada umejionea mwenyewe majibu ya chama chako dhidi ya upuuzi wanaoufanya tena umetoa hadi mfano hai wa barabara husika lakini bado wamekukana, pole sana Mkuu.
 
Majibu yenu ya kibabe ndiyo sababu za kushuka kwa mvuto wa chama. Sitasema sana, ila kuna msemo usemao, "Chungu kipikacho mifupa, hupasuliwa na mifupa."
 
Kwa vile nafahamu wanachama wenzangu tupo kwa wingi sana katika mtandao huu ni vizuri niseme tena suala la ujenzi wa barabara unaoendelea hapa Dodoma. Mkikumbuka nilisema kuhusu ujenzi usiokidhi uliofanywa miezi kama mitatu hivi iliyopita. Barabara zote sasa hivi ni makorongo. Ni jambo la ajabu sana, wapo walionijibu kwa kashfa.
Hivi leo kuna barabara ya area C ambayo inafanyiwa ukarabati. Mifereji inayochimbwa inahuzunisha. Kweli wana CCM wenzangu tumeshindwa kuisimamia serikali. Piteni barabara ya Hombolo hapo area C mtajionea. Hivi kwa uchimbaji huu kweli kuna malipo yatafanywa kwa kampuni hii au ni volunteers tu hawa. Hivi kweli tunajali fedha za wananchi. Where is the value of money? Where are we going? Do we want to kill these people. Who will then pay the tax? Lazima tumwogope Mungu.
Nina hakika viongozi wangu ni wasikivu mtalifanyia kazi hili.
Hata hivyo nimeandika barua mara nyingi sana kwa mkurugenzi na kwa kweli sijawahi pata jibu. Nawahakikishieni, kama hii bara bara haitarekebishwa, nitaondoka rasmi katika chama, na nina hakika nitaanguka na kundi la watu and one day you will pay for that.
 
Kwa vile nafahamu wanachama wenzangu tupo kwa wingi sana katika mtandao huu ni vizuri niseme tena suala la ujenzi wa barabara unaoendelea hapa Dodoma. Mkikumbuka nilisema kuhusu ujenzi usiokidhi uliofanywa miezi kama mitatu hivi iliyopita. Barabara zote sasa hivi ni makorongo. Ni jambo la ajabu sana, wapo walionijibu kwa kashfa.
Hivi leo kuna barabara ya area C ambayo inafanyiwa ukarabati. Mifereji inayochimbwa inahuzunisha. Kweli wana CCM wenzangu tumeshindwa kuisimamia serikali. Piteni barabara ya Hombolo hapo area C mtajionea. Hivi kwa uchimbaji huu kweli kuna malipo yatafanywa kwa kampuni hii au ni volunteers tu hawa. Hivi kweli tunajali fedha za wananchi. Where is the value of money? Where are we going? Do we want to kill these people. Who will then pay the tax? Lazima tumwogope Mungu.
Nina hakika viongozi wangu ni wasikivu mtalifanyia kazi hili.
Hata hivyo nimeandika barua mara nyingi sana kwa mkurugenzi na kwa kweli sijawahi pata jibu. Nawahakikishieni, kama hii bara bara haitarekebishwa, nitaondoka rasmi katika chama, na nina hakika nitaanguka na kundi la watu and one day you will pay for that.

Usiwe kibaraka wa Chadema, masuala ya CCM yanamalizwa kiofisi, njoo makao makuu ya chama chetu KIPENZI CHA WATANZANIA, utoe dukuduku lako na utekelezaji utafuata. Hao Chadema wamekalia majungu tu
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom