Hii ni kwa wale tunaokumbayia ajira.

Hewa mkaa

JF-Expert Member
Sep 3, 2012
742
377
Kwa wafanyakazi tulio wengi, hiki kibwagizo tumekutana nacho sana. Ama kutoka kwenye vinywa vya viongozi wetu kazini au kwa wafanyakazi wenzetu wasio na maono. Kwa ufupi ujumbe wa mara kwa mara ni "kuheshimu ajira".

Wengi tumekuwa waoga kuthubutu kuacha ajira. Visingizio tunavyotumia mara kwa mara:-
1)Bado watoto wanasoma
2)Mi umri wa kustaafu bado
3)Bado sijajenga
4)Bado sijamaliza mkopo
5)Aliyenitafutia kazi atanielewaje
6)n.k
Sababu hizi zote zimeyufanya kuwa waoga na kushindwa kuanza maisha ya kujitegemea.

Lakini kwa wale waliofumba macho na kufanya maamuzi ya kujiajiri, kauki hizi hazipo tena vinywani mwao. Kauli mbiu zao ni:-
1)Mtaji mdogo
2)Riba za benki ni kubwa
3)Mikopo inasumbua
4)n.k
Kwa ufupi ukijiajiri unaachana na woga kujibembeleza kwa bosi, unajiamini na kujipangia ratiba zako we mwenyewe.

Hakuna aliyewahi kuwa tajiri kwa kutegemea mshahara na posho. Hata kama unasubiri kiinua mgongo kikubwa ni bure tu kwa sababu umri huo uwezo wa kupanga mambo kwa umakini ni mdogo.

Shime tuchangamke mapema. Achana na kazi ukiwa bado na nguvu zako. Jifunze kupanga shughuli zako za binafsi ambazo ni muhimu kuliko kazi za kuajiriwa.

Kumbuka kuwa hata kama umeajiriwa kinachomata ni "unamiliki nini cha kwako" siyo "umewahi kufanya kazi gani". Unapoumwa au kufa jamaa zako watarithi kile ulicho nacho lakini mwajiri wako atawaza namna ya kujaza nafasi yako. WASALAAM
IMG_20190226_141332.JPG


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kila mmoja ana njia yake ya kutoka kimaisha, siyo lazima wote tuchague njia uliyoifuata wewe. Akili ni nywele kila mtu anazo zake.
 
Kaka usilazimishe watu waache ajira,asilimia kubwa ya middle class ni waajiriwa hao ndio wanategemewa sana na serikali Kwani ni kundi muhimu sana katika uchumi

Angalia sera Za mataifa yote duniani ni kuondoka katika kipato cha chini sio kua matajiri maana Yake nn...Muajiriwa hajazuiwa kufanya mambo yake binafsi lahasha,
Ningekuona wamaana kama ungetoa elimu vitu vingine by kufanya bila kuacha ajira yako au ajira ipi inakufaa ili uweze kufanya na mambo yako mengine...

Wengi wenu mnaohamasisha watu waache ajira mna maisha ya kubangaiza Hamna lolote la maana

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Una maana gani unaposema hakuna mtu aliyewahi kuwa tajiri kwa kutegemea posho na ajira? Unataka kusema akina Ronaldo na Messi sio matajiri au umesahau kuwa na wao wameajiriwa?
 
Una maana gani unaposema hakuna mtu aliyewahi kuwa tajiri kwa kutegemea posho na ajira? Unataka kusema akina Ronaldo na Messi sio matajiri au umesahau kuwa na wao wameajiriwa?
Hao ni wajasiriamali. Wanauza skill zao wala siyo ajira. Ndiyo maana wanaweza wakauzwa au wakawekwa mnadani.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kujiajiri sio kazi rahisi kama inavyohubiriwa hata kama una mtaji wa milioni 50.

Kujiajiri ni kipaji Sio kila mtu anacho
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom