Hii ni kazi inayopaswa kufanywa na Jaji au Mahakimu wa Mahakama ya Mwanzo?

kifupi kirefu

JF-Expert Member
Oct 29, 2018
539
3,507
Jaji ni mtu mkubwa na mwenye hadhi ya juu Sana katika mfumo wa Mahakama. Majaji pamoja na kuwa na hadhi ya juu pia ni watu ambao wanamajukumu mahususi na wanapaswa kufuatilia mambo nyeti kwenye kesi zinazofikishwa mbele yao. Hili kuweka heshima ya Mahakama na kuzuia Mahakama kuchezewa Jaji anapobaini Kuna watu wanafika mbele yake kwa lengo yakuidanganya Mahakama anapaswa kuchukua hatua hili watu wengine wanapofika mahakamani wawe na nidhamu na waeleze facts za ukweli kulingana na mazingira ya kile wanachokijua.

Inatia huruma na naamini majaji serious wakifuatilia kinachofanywa n Jamhuri kwenye upelekaji wa mashahidi mahakamani na ukimya wa jaji wanaumia Sana. Mahakama wakati mwingine zinapaswa kuilinda Serikali ila Serikali pamoja na kulindwa inapaswa kuonyesha kwamba ipo serious na jinai kweli ilitendeka.

Nimesikiliza maelezo ya mashahidi wa tatu na wanne waliyoandika Polisi yansikitisha. Siyo melezo ya shahidi kwenda kusomwa kwa jaji Bali yanapaswa kuishia Mahakama za Mwanzo. Lakini kwanini mashahidi wamekuw na kiburi n kwanini DPP na Polisi wameshindwa kufanya kazi yao ya kitaaluma? Ni kwasababu Wana uhakika 100% Jaji awezi kufanya chochote. Ukali n hadhi ya ujaji havionekani mahakamani. Uwezi kutofautisha kazi ya hakimu na Jaji, hakuna sehemu Jaji anasimamia standard za ujaji, hakuna professionalism Mahakama imebaki kucheka hata inapodanganywa wazi.

Nadhani Ni muda Sasa kesi hizi zirejeshwe Mahakama ya chini maana hakuna ladha ya kesi hizi kusikilizwa Mahakama kuu au Mahakama y mafisadi.

Shahidi Hana facts, hakuna muunganiko wa ushahidi, hakuna analosema la ukweli, dakika chache anasema hiki baada ya muda anajisemea mengine n hakuna kukemeana. Hizi siyo Mahakama, tunajidhalilisha Sana. Jaji asipoonyesha ukali wa kiti kwa mashahidi Mahakama zitaendwlea kuchezewa na kuwa sehemu ya majaribio.

Polisi awapo serious, DPP yupo tu mradi analipwa salary na Jaji naye katulia tu kulinda haki ya shahidi. Tunachezea Sana mhimili huu. Ukiona wakili wa utetezi anafika mahali anamwambia Jaji tushauriane tukurahisishie kuandika hukumu basi wakili wa utetezi ameona wazi anadhalilisha taaluma yake Bora wakayazungumze gizani huko labda Mahakama utafumbua macho
 
Ni ukweli usiofichika kuwa kesi hii ya kuchonga yenye nia ovu ya kumfunga Mh. Mbowe kwa gharama yoyote imeiumbua Serikali hii na vyombo vyake hasa jeshi la Polisi.

Na pia kesi hii imeacha doa kuuuubwa sana kwa mhimili wa Mahakama kwani ni dhahiri hukumu imeshaandikwa huko Ikulu kinachofanyika ni kuwatumia majaji ambao hata teuzi zao zilikuwa za kimkakati ili kubariki nia hii ovu ya watawala.

Hakika mhimili huu wa Mahakama na taaluma ya sheria imenajisiwa kwani hukumu hii ya kishetani itabaki kwenye rekodi na itaweza kutumika kama rejea katika kesi nyingine huko mbele ya safari.
 
Yule Jaji aliesikiliza kesi ya Zuma hiyo kesi angeifutilia mbali aisee yule jamaa ni kichwa na ana misimamo na anatumia Elimu yake sawa sawa bila upendeleo kwa Jamhuri mtu anakwambia akiandika akiwa amesimama atatoa saini tofauti na akiwa amekaa mahakama kuu wanaendelea kusikiliza hiyo kesi..au kiwango cha Elimu zetu zimeshuka sio bure sasa hiyo ni mahakama kuu huko chini za mwanzo si yapo madudu ya ajabu kabisa..
 
Yule Jaji aliesikiliza kesi ya Zuma hiyo kesi angeifutilia mbali aisee yule jamaa ni kichwa na ana misimamo na anatumia Elimu yake sawa sawa bila upendeleo kwa Jamhuri mtu anakwambia akiandika akiwa amesimama atatoa saini tofauti na akiwa amekaa mahakama kuu wanaendelea kusikiliza hiyo kesi..au kiwango cha Elimu zetu zimeshuka sio bure sasa hiyo ni mahakama kuu huko chini za mwanzo si yapo madudu ya ajabu kabisa..
Inashangaza Sana
 
Nilishangaa Jaji anakubali utetezi wa shahidi eti sahihi zimetofautiana kwa sababu zingine aliandika akiwa amesimama, how come na jaji anaishia kucheka tu.
 
Yaani mpaka leo shahidi wa nne wala huo ugaidi unaosemwa na sirro hatuuoni
Pamoja na elimu yake kamanda Siro napata mashaka sana kama alimuaminisha mh. rais kwa ushahidi huu mpaka kuropoka kwenye vyombo vya vya habari vya kimataifa.
 
Shahidi badala ya kuthibitisha uhusiano wa bastola na mtuhumiwa labda kwa finger prints anakuja kuieleza mahakama kuwa bastola ni nzima huku evidence zingine (risasi) amezitumia.

Kwani bastola kuwa nzima inathibitishaje ugaidi.
Hiki ndio kituko cha mhimili na jaji mhusika kuubali ushahidi wakipumbavu kama huu. Kwahiyo kuthibitisha uzima wa bastola ni nzima ndio waseme ni gaidi ilhali hakuna fujo wala kitendo chochote cha kuashiria ugaidi?!
 
Back
Top Bottom