Synthesizer
JF-Expert Member
- Feb 15, 2010
- 11,143
- 18,774
Nimeshitushwa sana na kauli iliyotolewa na Mwenyekiti wa Bunge, Sylivester Mabumba aliyekuwa akiendesha Bunge jana jioni. Baada ya Mbunge wa Viti Maalumu (CCM) Stella Manyanya kuwatuhumu Chadema kwa kuchochea mgomo na kudai kwamba walihusika na kumteka na kumjeruhi Dk Ulimboka, Mbunge wa Ubungo (Chadema), alikuja juu baada ya kauli hiyo akimtaka Mwenyekiti amtake Manyanya kuthibitisha au kufuta kauli yake.
Katika suala ambalo liko wazi sana kwamba Manyanya hakupaswa kuwashutumu Chadema kwa namna hii, Mabumba alionyesha wazi kuendesha kikao kwa njia ambayo ni ya kishabiki, kibaguzi na kitoto pale alipomjibu Manyika yeye Mnyika ndiye athibitishe kwamba Chadema hakihusiki.
Mie si mwanachama wa chama chochote cha kisiasa, lakini kwa kweli nimekerwa mno na jibu hili la Mabumba. Huu ni ushabiki, ubaguzi na utoto ambao haustahili kabisa katika kiongozi wa Bunge letu. Mabumba anapaswa kukumbushwa kwamba hili Bunge ni la Watanzania. Viongozi wa Bunge wamekuwa wakiwadai wabunge wa upinzani kutoa ushahidi hata katika mambo ambayo eidha si ya msingi au yako wazi kabisa. Huu ni ukandamizaji dhahiri wa wawakilishi wa Watanzania ambao hata sisi tusio wanachama wa vyama vya siasa tunaona unatia kichefuchefu.
Niko tayari kumpa simu yangu Mabumba ili ikiwezekana tukutane ana kwa ana nimweleze dukuduku langu kwa jibu lake hili linaloonyesha upungufu mkubwa katika masuala ya uongozi wa Bunge. Kama kuna mtu mwenye email ya Mabumba aiweke hapa ili tulio na hasira na jambo hili tumwandikie kutoridhishwa kwetu na kile alichokifanya.
03/07/2012
Baada ya kupewa email yake, nimemwandikia email Mbunge Mabumba, iko chini hapa kwenye hii thread.
Update: 04/07/2012:
Mnyika ataka ufafanuzi juu ya wabunge kudhalilishwa
Mbunge wa Ubungo, (Chadema) John Mnyika, ameomba mwongozo wa Spika, akitaka aelezwe hatua gani atahuchukuliwa Mwenyekiti wa Bunge, Sylivester Mabumba, kwa kitendo cha kuwadhalilisha wabunge wawili alipokuwa akiendesha kikao juzi jioni.
Mnyika aliomba mwongozo huo kwa Mwenyekiti wa Bunge, Jenister Mhagama, mara baada ya kipindi cha maswali na majibu mjini Dodoma jana.
Akitumia kanuni ya tano (1) kwamba juzi katika mkutano wa Bunge, Mwenyekiti wa Bunge, Mabumba (Mbunge wa Dole-CCM), alitoa maneno ya kuwadhalilisha wabunge wawili.
Alimtaja Mbunge wa Kasulu Mjini (NCCR-Mageuzi), Moses Machali, ambaye aliambiwa kuwa anadandia hoja na anajitafutia umaarufu.
Alisema pia Mabumba, alitoa maneno kuwa yeye (Mnyika), ameshindwa kujibu taarifa, jambo ambalo halikuwa ni kweli kwasababu hakupewa nafasi ya kujibu.
Alisema jambo jingine, Mabumba alimwambia kuwa `anawashwa washwa', na kwamba hayo maneno yameleta hasira sana kutoka kwa wananchi wake wa jimbo la Ubungo kwa kuwa wameona kuwa wamekashfiwa wao.
Alisema na wananchi wa Kasulu Mjini, nao wanaona kuwa wamekashfiwa wao kwa kitendo cha Mbunge wao kutolewa maneno ya udhalilishaji.
Alisema kanuni 64 (2) inatoa nafasi kutoa utaratibu kwa mambo yanayomhusu mbunge mwingine. Mnyika alisema pia maneno hayo yanakiuka ibara ya sita ya sheria ya maadili ya umma. Aliomba mwongozo wa Spika, wabunge hao wachukue hatua gani kwa jambo kama hilo.
Kuhusu suala la Mnyika, Mhagama alisema suala hilo atalitolea maamuzi baadaye ama siku atakayoona inafaa.
CHANZO: NIPASHE
Katika suala ambalo liko wazi sana kwamba Manyanya hakupaswa kuwashutumu Chadema kwa namna hii, Mabumba alionyesha wazi kuendesha kikao kwa njia ambayo ni ya kishabiki, kibaguzi na kitoto pale alipomjibu Manyika yeye Mnyika ndiye athibitishe kwamba Chadema hakihusiki.
Mie si mwanachama wa chama chochote cha kisiasa, lakini kwa kweli nimekerwa mno na jibu hili la Mabumba. Huu ni ushabiki, ubaguzi na utoto ambao haustahili kabisa katika kiongozi wa Bunge letu. Mabumba anapaswa kukumbushwa kwamba hili Bunge ni la Watanzania. Viongozi wa Bunge wamekuwa wakiwadai wabunge wa upinzani kutoa ushahidi hata katika mambo ambayo eidha si ya msingi au yako wazi kabisa. Huu ni ukandamizaji dhahiri wa wawakilishi wa Watanzania ambao hata sisi tusio wanachama wa vyama vya siasa tunaona unatia kichefuchefu.
Niko tayari kumpa simu yangu Mabumba ili ikiwezekana tukutane ana kwa ana nimweleze dukuduku langu kwa jibu lake hili linaloonyesha upungufu mkubwa katika masuala ya uongozi wa Bunge. Kama kuna mtu mwenye email ya Mabumba aiweke hapa ili tulio na hasira na jambo hili tumwandikie kutoridhishwa kwetu na kile alichokifanya.
03/07/2012
Baada ya kupewa email yake, nimemwandikia email Mbunge Mabumba, iko chini hapa kwenye hii thread.
Update: 04/07/2012:
Mnyika ataka ufafanuzi juu ya wabunge kudhalilishwa
Mbunge wa Ubungo, (Chadema) John Mnyika, ameomba mwongozo wa Spika, akitaka aelezwe hatua gani atahuchukuliwa Mwenyekiti wa Bunge, Sylivester Mabumba, kwa kitendo cha kuwadhalilisha wabunge wawili alipokuwa akiendesha kikao juzi jioni.
Mnyika aliomba mwongozo huo kwa Mwenyekiti wa Bunge, Jenister Mhagama, mara baada ya kipindi cha maswali na majibu mjini Dodoma jana.
Akitumia kanuni ya tano (1) kwamba juzi katika mkutano wa Bunge, Mwenyekiti wa Bunge, Mabumba (Mbunge wa Dole-CCM), alitoa maneno ya kuwadhalilisha wabunge wawili.
Alimtaja Mbunge wa Kasulu Mjini (NCCR-Mageuzi), Moses Machali, ambaye aliambiwa kuwa anadandia hoja na anajitafutia umaarufu.
Alisema pia Mabumba, alitoa maneno kuwa yeye (Mnyika), ameshindwa kujibu taarifa, jambo ambalo halikuwa ni kweli kwasababu hakupewa nafasi ya kujibu.
Alisema jambo jingine, Mabumba alimwambia kuwa `anawashwa washwa', na kwamba hayo maneno yameleta hasira sana kutoka kwa wananchi wake wa jimbo la Ubungo kwa kuwa wameona kuwa wamekashfiwa wao.
Alisema na wananchi wa Kasulu Mjini, nao wanaona kuwa wamekashfiwa wao kwa kitendo cha Mbunge wao kutolewa maneno ya udhalilishaji.
Alisema kanuni 64 (2) inatoa nafasi kutoa utaratibu kwa mambo yanayomhusu mbunge mwingine. Mnyika alisema pia maneno hayo yanakiuka ibara ya sita ya sheria ya maadili ya umma. Aliomba mwongozo wa Spika, wabunge hao wachukue hatua gani kwa jambo kama hilo.
Kuhusu suala la Mnyika, Mhagama alisema suala hilo atalitolea maamuzi baadaye ama siku atakayoona inafaa.
CHANZO: NIPASHE