HumbleBoy98
JF-Expert Member
- Aug 30, 2020
- 386
- 392
Habari zenu wakuu, natumai mko Salama na mnaendelea vyema na majukumu ya ujenzi wa taifa.
Niende Moja kwa Moja kwenye mada.
Mimi HumbleBoy98 nimekuwa na tatizo la usikivu kwa takribani miaka 9 sasa, sikuzaliwa hivi nilikuwa mzima kabisa Ila ilipofika mwaka 2011 nilianza kuhisi Hali ya tofauti katika usikivu wangu.
Ni kwamba mtu anapoongea namsikia sauti yake vizuri tu, ila tatizo ni kwamba Yale matamshi siyaelewi yanapotamkwa Yani nakuwa sisiikii baadhi ya herufi zinapotamkwa hivyo mtu anapoongea naona Kama anamung'unya tu maneno hivi na anachokiongea nakuwa sikielewi.
Tatizo hili halikuanza na dalili zozote sikuwahi hisi maumivu masikioni, Wala kutoa usaha, Wala Nini na nilishaenda hospitali Fulani pale maeneo ya magomeni mikumi inaitwa "EKENYWA", Pale wakaniingizia kifaa fulani kilichokuwa na kamera sikioni ila hawakuona uvimbe Wala tatizo lolote lile masikioni mwangu!
Hali hii imenifanya nishindwe kuelewa hili tatizo limetokana na nini sababu halikuanza na dalili zozote Yani Ni ghafla tu nimejikuta mtu anapoongea namsikia lakini simuelewi.
Sasa nimekuwa nikijaribu kuperuzi mtandaoni ili kuona Kama nitakutana na maelezo yatakayoendana na hili tatizo langu, na katika kuperuzi kwangu ndipo nilipokutana na kitu kinaitwa "High frequency hearing loss"
Kwa mujibu wa maelezo niliyosoma katika mtandao Ni kwamba hii "High frequency hearing loss" Ni Hali ambayo mtu anashindwa kusikia sauti au matamshi ambayo utamkwaji wake unatoa frequency za juu sana mfano herufi "s", "f", na "ch" anakuwa hawezi kuzisikia zinapotamkwa hivyo Basi kuhisi Kama mtu anamung'unya maneno na kutoelewa kinachoongelewa.
Niliposoma hayo nikahisi labda na Mimi Nina hii "High frequency hearing loss" maana yaliyoelezwa Hapo ndiyo hasa yanayonikabili, Ila nilikuja kupata sintofahamu baada ya kusoma vyanzo ama visababishi vya tatizo hili na kugundua hakuna hate kimoja ambacho kinahusiana nami.
Kwa mujibu wa maelezo hayo niliyosoma mtandaoni wanasema kwamba high frequency hearing loss inasababishwa na aidha kukaa sehemu yenye kelele nyingi kupita kiasi kwa muda mrefu au umri kuwa mkubwa (uzee).
Sasa kunachnichanganya ni kwamba haya yote mawili kwangu hayahusiki katika kumbu kumbu zangu sikumbuki kabisa Kama niliwahi kukaa sehemu yenye kelele nyingi kupita kiasi kwa muda mrefu kiasi Cha kuweza kusababisha madhara masikioni mwangu. Na hili la pili kuhusu umri kuwa mkubwa ndiyo kabisa halihusiani nami, umri wangu Ni miaka 22 tu!
Sasa wakuu ambao Ni wataalamu wa haya mambo naomba mnisaidie hili linaweza kuwa tatizo gani?? Inawezeoana ikawa ni hiyo high frequency hearing loss?? Mbona hivyo vyanzo tajwa havishabihiani kabisa na Mimi?
Nahitaji msaada kwakweli sababu Hali hii inanipa tabu Sana nashindwa kuwasiliana na niwapendao kwa raha, hapa nilipo Mimi Ni mwanachuo ila kwa 90% facilitator wangu ni Mimi mwenyewe sababu mwalimu anapoingia darasani kufundisha nakuwa sielewi chochote Ni mpaka mida ya prepo nianze kukaa na kujifundisha mwenyewe mpaka nielewe, ninaposikiliza muziki nasikia mdundo wa beat tu maneno yanayoimbwa siyaelewi, ninapotazama movie ni mpaka iwe na 'subtitle'ndo nitaielewa hata ikiwa ya kiswahili, tunapokuwa tumekaa watu wengi naonaga tu wenzangu wanapiga story wanacheka ila Mimi hata sielewi wanaongea Nini nasikia makelele tu! Hali hii inanifanya muda mwingi niwe napendelea kukaa peke yangu na kujitenga na watu.
Nilishauriwa kutumia zile 'hearing aid' ila na zenyewe nilitumia kwa muda mchache tu nikaamua kuachana nazo maana zinaongeza tu sauti ila Bado matamshi siyaelewi nikaona zitaniharibu zaidi saahizi sitaki hata kusikia habari za hearing aid!
Wakuu ambao mnaweza kuwa na uelewa na tatizo hili na wataalamu pia naombeni ushauri wenu tafadhali
Nawasilisha
Niende Moja kwa Moja kwenye mada.
Mimi HumbleBoy98 nimekuwa na tatizo la usikivu kwa takribani miaka 9 sasa, sikuzaliwa hivi nilikuwa mzima kabisa Ila ilipofika mwaka 2011 nilianza kuhisi Hali ya tofauti katika usikivu wangu.
Ni kwamba mtu anapoongea namsikia sauti yake vizuri tu, ila tatizo ni kwamba Yale matamshi siyaelewi yanapotamkwa Yani nakuwa sisiikii baadhi ya herufi zinapotamkwa hivyo mtu anapoongea naona Kama anamung'unya tu maneno hivi na anachokiongea nakuwa sikielewi.
Tatizo hili halikuanza na dalili zozote sikuwahi hisi maumivu masikioni, Wala kutoa usaha, Wala Nini na nilishaenda hospitali Fulani pale maeneo ya magomeni mikumi inaitwa "EKENYWA", Pale wakaniingizia kifaa fulani kilichokuwa na kamera sikioni ila hawakuona uvimbe Wala tatizo lolote lile masikioni mwangu!
Hali hii imenifanya nishindwe kuelewa hili tatizo limetokana na nini sababu halikuanza na dalili zozote Yani Ni ghafla tu nimejikuta mtu anapoongea namsikia lakini simuelewi.
Sasa nimekuwa nikijaribu kuperuzi mtandaoni ili kuona Kama nitakutana na maelezo yatakayoendana na hili tatizo langu, na katika kuperuzi kwangu ndipo nilipokutana na kitu kinaitwa "High frequency hearing loss"
Kwa mujibu wa maelezo niliyosoma katika mtandao Ni kwamba hii "High frequency hearing loss" Ni Hali ambayo mtu anashindwa kusikia sauti au matamshi ambayo utamkwaji wake unatoa frequency za juu sana mfano herufi "s", "f", na "ch" anakuwa hawezi kuzisikia zinapotamkwa hivyo Basi kuhisi Kama mtu anamung'unya maneno na kutoelewa kinachoongelewa.
Niliposoma hayo nikahisi labda na Mimi Nina hii "High frequency hearing loss" maana yaliyoelezwa Hapo ndiyo hasa yanayonikabili, Ila nilikuja kupata sintofahamu baada ya kusoma vyanzo ama visababishi vya tatizo hili na kugundua hakuna hate kimoja ambacho kinahusiana nami.
Kwa mujibu wa maelezo hayo niliyosoma mtandaoni wanasema kwamba high frequency hearing loss inasababishwa na aidha kukaa sehemu yenye kelele nyingi kupita kiasi kwa muda mrefu au umri kuwa mkubwa (uzee).
Sasa kunachnichanganya ni kwamba haya yote mawili kwangu hayahusiki katika kumbu kumbu zangu sikumbuki kabisa Kama niliwahi kukaa sehemu yenye kelele nyingi kupita kiasi kwa muda mrefu kiasi Cha kuweza kusababisha madhara masikioni mwangu. Na hili la pili kuhusu umri kuwa mkubwa ndiyo kabisa halihusiani nami, umri wangu Ni miaka 22 tu!
Sasa wakuu ambao Ni wataalamu wa haya mambo naomba mnisaidie hili linaweza kuwa tatizo gani?? Inawezeoana ikawa ni hiyo high frequency hearing loss?? Mbona hivyo vyanzo tajwa havishabihiani kabisa na Mimi?
Nahitaji msaada kwakweli sababu Hali hii inanipa tabu Sana nashindwa kuwasiliana na niwapendao kwa raha, hapa nilipo Mimi Ni mwanachuo ila kwa 90% facilitator wangu ni Mimi mwenyewe sababu mwalimu anapoingia darasani kufundisha nakuwa sielewi chochote Ni mpaka mida ya prepo nianze kukaa na kujifundisha mwenyewe mpaka nielewe, ninaposikiliza muziki nasikia mdundo wa beat tu maneno yanayoimbwa siyaelewi, ninapotazama movie ni mpaka iwe na 'subtitle'ndo nitaielewa hata ikiwa ya kiswahili, tunapokuwa tumekaa watu wengi naonaga tu wenzangu wanapiga story wanacheka ila Mimi hata sielewi wanaongea Nini nasikia makelele tu! Hali hii inanifanya muda mwingi niwe napendelea kukaa peke yangu na kujitenga na watu.
Nilishauriwa kutumia zile 'hearing aid' ila na zenyewe nilitumia kwa muda mchache tu nikaamua kuachana nazo maana zinaongeza tu sauti ila Bado matamshi siyaelewi nikaona zitaniharibu zaidi saahizi sitaki hata kusikia habari za hearing aid!
Wakuu ambao mnaweza kuwa na uelewa na tatizo hili na wataalamu pia naombeni ushauri wenu tafadhali
Nawasilisha