Katavi
Platinum Member
- Aug 31, 2009
- 41,983
- 12,700
Kuna jamaa mmoja jana amefanya kituko..........alikuwa kakaa kijiweni na rafiki zake, ghafla kwa mbali akamuona mama wa mkewe akija na njia ile kilipo kijiwe chao. Jamaa akakimbia na kujificha hadi yule mama apite, lakini na yule mkwe wake kumbe nae alimuona jamaa naye akabadili njia. Jamaa aliporejea pale wenzake wakaanza kumtania kwa kuwa muoga mbele ya mkwe wake lakini yeye akajitetea kuwa ile ni heshima..
Hivi hii ni nini maana sehemu nyingine watu wanakimbia kabisa ili kukwepa tu wasikutane na wakwe zao wawapo barabarani......
Hivi hii ni nini maana sehemu nyingine watu wanakimbia kabisa ili kukwepa tu wasikutane na wakwe zao wawapo barabarani......