Hii ni Dharau kwa Fani ya Udaktari!

mcfm40

JF-Expert Member
Nov 2, 2010
4,452
3,150
Jamani mimi ni mwalimu nafundisha Chuo Kikuu cha Dar es Salaam kama Assistant Lecturer.

Kusema kweli hii nchi haijui thamani ya madaktari na professionals wengine kwa ujumla.

Hivi kweli unaweza kulinganisha miaka mitano ya kusomea udaktari na miaka mitatu ya digrii nyingine hizi!?

Nimeshangaa eti daktari anayeanza kazi analipwa laki 9. Huu ni mshahara mdogo kuliko wa Tutorial Assistant aliyesomea digrii yake kwa miaka mitatu tu tena digirii laini (nimesoma mimi Arts) usinitolee mimacho! Ni laini tu huwezi kulinganisha na nondo za udaktari!

Kusema ukweli interns wanapaswa kulipwa minimum 2mil. Yaani daktari alipwe sawa na kada nyingine? You are kidding!

Kazi ya udaktari ni habari nyingine jamani tusidanganyane. Kikwete anachofanya ni kujaribu kugombanisha madaktari na wananchi! Unajua watu wa kawaida hawajui nondo za udaktari zilivyo ngumu na ilivyo ngumu kufaulu! Watu mliokimbia chemistry, physics, biology mnajua habari yake, sio mchezo!

Hivi inakuwaje serikali imeanza tabia ya kupuuzia kada nyeti kama udaktari? Kiwete anazungumza kwa kubeza tu, anafikiri ni rahisi kama alivyodesa na uchumi wake pale ya Mlimani!? Madaktari pambaneni mtambulikane kama kada maalumu na muwe na commission yenu maalumu ya mishahara.

Ni kichekesho kwamba mganga wa kienyeji na wenzake wa darasa la saba pale bungeni anakula milioni 7, professionals wanadhihakiwa. What are our priorities?

Kwa mtindo huu tutaweza kuzuia madaktari wetu kutimkia nje kwenye greener pastures? Na nin nani atapenda hiyo kazi ya udaktari ya kuteseka kusoma mavitu magumu halafu hata hudhaminiwi kwa nini nisichukue kozi laini laini si mshahara ni huo huo?

Serikali inapaswa kujitathmini upya na kujua vipaumbele vyake. Kazi ya Udakatari haithaminiwi Tanzania! Hatutafika namana hii! Hii ni kazi inayohusisha uhai wa watu lazima tuinvest vya kutosha hapa bial visingizio vyovyote. Kwa hiyo mkishawalazimisha kurudi kazini kwa manunguniko ndiyo watatibia watu kwa juhudi?

Serikali mnaweka maisha ya wananchi hatarini! Let us be serious. Sidhani kama kuna dakatri analazimisha milioni 3.5; lengo ni kiwango kifikie walau mahali reasonable! Hii inawezekana kabisa, na si kweli kwamba lazima mshahara wa madaktari ukibadilika na kada nyingine zote ubadilike!

Kama nilivyosema kazi ya udaktari habari nyingine kabisaa! Kuanzia kusomea hadi kazi yenyewe yataka moyo sio sawa na kufundisha darasani!
 
Hapo UDSM unafundisha school gani vile? Mimi tu kuuliza.

Acha kupotosha kwamba uko UDSM wewe kwasababu huwezi kuja bila data. TA hapo UDSM anapokea bei gani? Ass. Lecturer naye anaanzia bei gani? Je, ni sifa zipi zinamfanya mtu awe Ass. Lecturer? Ni hiyo miaka mitatu au? Wewe kama ni Ass. Lecturer, una muda gani kazini na unapata mshahara (basic) bei gani? Na mbali na mshahara wako wewe kama Ass. Lecturer, TA na Lecturers, je kuna benefits zozote anazopata huyo mwalimu? Ungekuwa Ass. Lecturer ungefahamu ni kwanini waalimu wengi wa Vyuo vikuu vya Serikali wanapiga deiwaka.

Mimi naamini wewe ni Dr., na una ndugu ambaye ni Mwalimu sasa unatafuta mazingira ya kutaka kujustify mahitaji makubwa hasa ya mshahara wa 3.5 Million kwa Drs.; wanaoanza kazi. Sasa nikuulize swali, Je 3.5 Milion ni basic ya level gani kwa chuo kikuu kama siyo Professors. Kwahiyo, unachotaka kujusstify hapa ni kwamba Interns anapaswa alipwe robo tatu ya Full Professor ambaye amekuwa kazini zaidi ya miaka 20?

Mimi madai ya Drs hasa kwenye mshahara wa Drs wanaoanza kazi kuwa 3.5 Milion is too much. Sasa najiuliza swali ,je timu ya Drs ya negotiation ilikuwa imekamilika? nasema hivyo kwasababu, kiutaalamu unapoenda kwenye negotiations, then lazima ujue kwamba huwezi kupata 100 percent ya vitu vyote unavyohitaji. Kuna kitu kinaitwa Fall Back position, ambapo unakuwa na minimum ya kiwango ambacho ikifikiwa unaweza ukakubali. Pia unakuwa na priorities, yaani unasema kama 1,2,3,4 zikikubaliwa kama tunavyohitaji, then 5,6,7 tunaachana navyo au tunapunguza ili kwamba tuweze kufikia makubaliano, na hii ndiyo inaitwa win-win negotiation. Ukienda kwenye negotiations huku ukitaka mahitaji yako yote yapite jinsi yalivyo, then hiyo sasa negotiations bali ni order ili ambayo counterpart wako anatakiwa kupokea na si NEGOTIATIONS. Mimi nilitegemea Drs walikuwa na timu ya wataalamu wa negotiations kwenye kamati yao, lkn baada ya kusoma hotuba ya Rais, nimegundua kwamba hata Drs haikuwa na kamati inayojua nini maana ya negotiations na si kutoa Instructions. Na hili inawezekana, kwani kamati yao ilikuwa na Doctors of Medicine wote kama nitakuwa sahihi, lkn haikuwa na mtu wa negotiation skills. Negotiation skills nayo ni professional, haiji automatically kama baadhi yenu wanavyofikiria.
TELO.

NB:
Siyo busara na wala huitendei haki UDSM unapoamua kujipa jina kwamba wewe ni mwalimu pale tena wa kiwango cha Ass. Lecturer lkn unajichanganya katika kile unachowasilisha hapa na makosa mengi sana. Siyo busara kuichafua UDSM kwa dhana tu kwamba ukijitambulisha uko UDSM basi mchango wako watu watahueshimu hata kama unaadika upuuzi (source: Mnyika). Watu wataheshimu mchango wako kama una mantiki hata kama ungekuwa wazi kwamba wewe ni Dr., jinsi ulivyo.
 
TELO

Umejibuje tena kwa urefu kitu ambacho unaona kimekosewa na hakina mantiki? Umeelewa bila shaka. kwa hiyo unaamini kikwete alichosema ndio ukweli? Na ni kweli madaktari hawataki anything less than 3.5m. Mbona hujajibu hoja ya umuhimu wa kada ya udaktari? Wenzio hatuna mda mrefu wa kukaa na kuhakiki spellings kwa sababu hii sio Proposal ya PHD. Hatujali spelling alimradi ujumbe umefika km ulivokufikia wewe na ukaelewa!
 
Last edited by a moderator:
Daktari anaeanza alipwe 3.5 m, na kama professa ataona kuwa juyo daktari kamsogelea nae adai ongezeko kivyake.
 
Nimenukuu baadhi ya maneno ya JK kwenye hotuba yake.
Yani anaposema kuwa Muajiri hana uwezo wa kukulipa so yanini Dr Kugoma.
Hii kauli inamaaana kuwa hata yale madai ya serikali kuwa wanayafanyia kazi madai yote ya Ma daktari ni Ulaghai na Usanii Mtupu, Hii inamaana kuwa Seikali ilikuwa inainawazuga tu Ma Dr ilhali haikuwa na nia ya dhat ya kutekeleza Baadhi ya Madai ya Ma Dr.

My Take
Drs Msirudi Nyuma, JK huyu huyu atakuja kuwapigia Magoti
 
nimechoshwa na kauli eti daktari anapendelewa kwa kulipwa sana
........hebu nisaidieni mishahara ya hawa watu kwa level ya degree wanalipwa ngapi
........tanapa
.........tra
..........bot
........bandari
.......hazina
..........msd
..........nhif
..........kilimo
..........mahakama
.........ubalozini/mambo ya nje
..........etc....etc...
 
mcfm40,

kama chuo cha udsm ndo kina watu kama nyinyi nimepata jibu kwa nini kimepoteza mwelekeo. miaka hiyo sisi tukisoma hapo hakikuwa hivyo.
 
Last edited by a moderator:
Madaktari wa bongo! hiyo hela inawatosha, kagaweni panadol huko...you don't deserve more than curremt salaries; for what?
kamachuo cha udsm ndo kina watu kama nyinyi nimepata jibu kwa nini kimepoteza mwelekeo. miaka hiyo sisi tukisoma hapo hakikuwa hivyo.
 
Kama serikali imeshindwa kuziendesha (au kulipa mishahara ya madaktari wa) hizo hosptali zake.... nafikiri ni bora hizo hospitali wakazibinafsisha. Njia mbadala itafutwe ili watu waendelea kupata huduma kwa gharama ndogo,na katika mazingira mazuri.
 
Nimenukuu baadhi ya maneno ya JK kwenye hotuba yake.
Yani anaposema kuwa Muajiri hana uwezo wa kukulipa so yanini Dr Kugoma.
Hii kauli inamaaana kuwa hata yale madai ya serikali kuwa wanayafanyia kazi madai yote ya Ma daktari ni Ulaghai na Usanii Mtupu, Hii inamaana kuwa Seikali ilikuwa inainawazuga tu Ma Dr ilhali haikuwa na nia ya dhat ya kutekeleza Baadhi ya Madai ya Ma Dr.

My Take
Drs Msirudi Nyuma, JK huyu huyu atakuja kuwapigia Magoti

Wameambiwa kama mshahara hamuutaki yanini kuendelea kumdai muajiri ambae hawezi kuwapa? si nendeni mkaajiriwe mtakopata zaidi? mnangoja nini? anaegoma kazi hana.

Yooote mengine ni maneno yako tu.
 
unajua JK anaongea vitu very cheap...yaani simuelwi kabisa..hivianamfanya nani mtoto hapa...bora akae kimya
 
ANA HAKI YA KUSEMA HIVYO KWAKUWA HATUWEZI INGIA MOYONI MWAKE TUKAUJUA UKWELI WAKE, LAKINI HATA MWIZI MZOEFU AKIULIZWA KUWA KAMA HUWA ANAIBA ATAKATAAA. USHAHIDI WA KIMAZINGIRA UNATHIBITISHA KUHUSIKA KWA SERIKALI KATIKA JAMBO HILO NA KWASABABU HIYO SERIKALI ITAKANA KUHUSIKA KWAKWE LAKINI SYSTEM NDIVYO INFANYAVYO INAHUSIKA MOJA KWA MOJA NA KUFICHA UKWELI KWA NAMNA YA AJABU. jK AMESEMA UONGO NA HAKIKA SERIKALI HII YA MADHALIMU IMEHUSIKA KABISA NA TUKIO HILI.
 
Wameambiwa kama mshahara hamuutaki yanini kuendelea kumdai muajiri ambae hawezi kuwapa? si nendeni mkaajiriwe mtakopata zaidi? mnangoja nini? anaegoma kazi hana.

Yooote mengine ni maneno yako tu.
Ukiona wanaume wameweka post, unaanzwa kuwashwa washwa...
 
Back
Top Bottom