mcfm40
JF-Expert Member
- Nov 2, 2010
- 4,452
- 3,150
Jamani mimi ni mwalimu nafundisha Chuo Kikuu cha Dar es Salaam kama Assistant Lecturer.
Kusema kweli hii nchi haijui thamani ya madaktari na professionals wengine kwa ujumla.
Hivi kweli unaweza kulinganisha miaka mitano ya kusomea udaktari na miaka mitatu ya digrii nyingine hizi!?
Nimeshangaa eti daktari anayeanza kazi analipwa laki 9. Huu ni mshahara mdogo kuliko wa Tutorial Assistant aliyesomea digrii yake kwa miaka mitatu tu tena digirii laini (nimesoma mimi Arts) usinitolee mimacho! Ni laini tu huwezi kulinganisha na nondo za udaktari!
Kusema ukweli interns wanapaswa kulipwa minimum 2mil. Yaani daktari alipwe sawa na kada nyingine? You are kidding!
Kazi ya udaktari ni habari nyingine jamani tusidanganyane. Kikwete anachofanya ni kujaribu kugombanisha madaktari na wananchi! Unajua watu wa kawaida hawajui nondo za udaktari zilivyo ngumu na ilivyo ngumu kufaulu! Watu mliokimbia chemistry, physics, biology mnajua habari yake, sio mchezo!
Hivi inakuwaje serikali imeanza tabia ya kupuuzia kada nyeti kama udaktari? Kiwete anazungumza kwa kubeza tu, anafikiri ni rahisi kama alivyodesa na uchumi wake pale ya Mlimani!? Madaktari pambaneni mtambulikane kama kada maalumu na muwe na commission yenu maalumu ya mishahara.
Ni kichekesho kwamba mganga wa kienyeji na wenzake wa darasa la saba pale bungeni anakula milioni 7, professionals wanadhihakiwa. What are our priorities?
Kwa mtindo huu tutaweza kuzuia madaktari wetu kutimkia nje kwenye greener pastures? Na nin nani atapenda hiyo kazi ya udaktari ya kuteseka kusoma mavitu magumu halafu hata hudhaminiwi kwa nini nisichukue kozi laini laini si mshahara ni huo huo?
Serikali inapaswa kujitathmini upya na kujua vipaumbele vyake. Kazi ya Udakatari haithaminiwi Tanzania! Hatutafika namana hii! Hii ni kazi inayohusisha uhai wa watu lazima tuinvest vya kutosha hapa bial visingizio vyovyote. Kwa hiyo mkishawalazimisha kurudi kazini kwa manunguniko ndiyo watatibia watu kwa juhudi?
Serikali mnaweka maisha ya wananchi hatarini! Let us be serious. Sidhani kama kuna dakatri analazimisha milioni 3.5; lengo ni kiwango kifikie walau mahali reasonable! Hii inawezekana kabisa, na si kweli kwamba lazima mshahara wa madaktari ukibadilika na kada nyingine zote ubadilike!
Kama nilivyosema kazi ya udaktari habari nyingine kabisaa! Kuanzia kusomea hadi kazi yenyewe yataka moyo sio sawa na kufundisha darasani!
Kusema kweli hii nchi haijui thamani ya madaktari na professionals wengine kwa ujumla.
Hivi kweli unaweza kulinganisha miaka mitano ya kusomea udaktari na miaka mitatu ya digrii nyingine hizi!?
Nimeshangaa eti daktari anayeanza kazi analipwa laki 9. Huu ni mshahara mdogo kuliko wa Tutorial Assistant aliyesomea digrii yake kwa miaka mitatu tu tena digirii laini (nimesoma mimi Arts) usinitolee mimacho! Ni laini tu huwezi kulinganisha na nondo za udaktari!
Kusema ukweli interns wanapaswa kulipwa minimum 2mil. Yaani daktari alipwe sawa na kada nyingine? You are kidding!
Kazi ya udaktari ni habari nyingine jamani tusidanganyane. Kikwete anachofanya ni kujaribu kugombanisha madaktari na wananchi! Unajua watu wa kawaida hawajui nondo za udaktari zilivyo ngumu na ilivyo ngumu kufaulu! Watu mliokimbia chemistry, physics, biology mnajua habari yake, sio mchezo!
Hivi inakuwaje serikali imeanza tabia ya kupuuzia kada nyeti kama udaktari? Kiwete anazungumza kwa kubeza tu, anafikiri ni rahisi kama alivyodesa na uchumi wake pale ya Mlimani!? Madaktari pambaneni mtambulikane kama kada maalumu na muwe na commission yenu maalumu ya mishahara.
Ni kichekesho kwamba mganga wa kienyeji na wenzake wa darasa la saba pale bungeni anakula milioni 7, professionals wanadhihakiwa. What are our priorities?
Kwa mtindo huu tutaweza kuzuia madaktari wetu kutimkia nje kwenye greener pastures? Na nin nani atapenda hiyo kazi ya udaktari ya kuteseka kusoma mavitu magumu halafu hata hudhaminiwi kwa nini nisichukue kozi laini laini si mshahara ni huo huo?
Serikali inapaswa kujitathmini upya na kujua vipaumbele vyake. Kazi ya Udakatari haithaminiwi Tanzania! Hatutafika namana hii! Hii ni kazi inayohusisha uhai wa watu lazima tuinvest vya kutosha hapa bial visingizio vyovyote. Kwa hiyo mkishawalazimisha kurudi kazini kwa manunguniko ndiyo watatibia watu kwa juhudi?
Serikali mnaweka maisha ya wananchi hatarini! Let us be serious. Sidhani kama kuna dakatri analazimisha milioni 3.5; lengo ni kiwango kifikie walau mahali reasonable! Hii inawezekana kabisa, na si kweli kwamba lazima mshahara wa madaktari ukibadilika na kada nyingine zote ubadilike!
Kama nilivyosema kazi ya udaktari habari nyingine kabisaa! Kuanzia kusomea hadi kazi yenyewe yataka moyo sio sawa na kufundisha darasani!