Hii ni dharau kubwa kwa wizara ya mambo ya ndani


Mkurugenzi Mkuu wa Kampuni ya ulinzi ya Knight Support,David Sutton akitishia kuondoka kikaoni kwa ghadhabu baada ya Kamishna Mkuu wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji,Jenerali Matwani Kapamba (kushoto)kumueleza Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi,Shamsi Vuai Nahodha (Mwenye suti aliyeketi ambaye pia ni Mbunge wa kuteuliwa na Waziri Kiongozi Mstaafu SMZ)kuhusu kampuni yake,wakati waziri huyo alipotembelea kampuni hiyo ikiwa ni sehemu yake ya ziara kwa kampuni mbalimbali binafsi za ulinzi na uokoaji,Dar es Salaam.Picha na Fadhili Akida

Verdict:
Du! Kweli sikitiko eeh sikitiko limetupata Watanzania, kuwa sasa mambo yamefikia hivi! kudadeki! siamini macho! hata wageni wanaona kila kitu kipo shaghalabaga! kiasi wanaweza leta zogo 'high-table' mbele ya 'kadamnasi', maana tunajua mambo yalikuwa yanafanyika kwa kificho kati ya serikali na wawekezaji lakini sasa mambo hadharani! Watanzania 2015 lazima kubadili chama na mfumo mzima kama tunataka kujinasua kutoka 'janga hili'.
 
Nafikiri suala hili linapaswa kukemewa kwa nguvu kubwa sana na iiwezekana huyu jamaa aadhibiwe kwa hata kuondolewa hapa nchini. Haiwezekani kwa namna yeyote ile huyu mgeni kuidharau serikali yetu kiasi hiki na bado wanaruhusiwa kutengeneza faida kutoka kwenye mifuko ya Watanzania! Halivumiliki hili, kwa namna yeyote ile kama hii kampuni haikuweza kukubaliana na yale waliyosemwa basi angeiweka bayana na kutafuta mwafaka na sio kuvunjiana heshima mbele ya vyombo vya habari, ikumbukwe alifuatwa kwake na aliwakaribisha kama hawakuwa wakielewana asingewaruhusu kuja kwake.
 
Na hicho kikwapa cha huyu Mdhungu inamaana ndio muda huu huu katoka kuzima moto mahala??

Kama wizara yetu ya mambo ya ndani huwa wanavu kwao zile fedha za wazee basi salaam mla rushwa toka kwa wenzetu wadhungu ndio huwaga ni hivo hivo. Wazungu wanachukia sana rushwa na kumdharau sana mwenye kuiendekeza hata kama ana cheo gani serikalini.

Na kwa kuwa picha zima imetokea mbele ya waziri mwenyewe huku akionekana amenyea kama vile kanyeshewa basi ukatafute tu jibu lako kichwani.
 
View attachment 19274

Mkurugenzi Mkuu wa Kampuni ya ulinzi ya Knight Support,David Sutton akitishia kuondoka kikaoni kwa ghadhabu baada ya Kamishna Mkuu wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji,Jenerali Matwani Kapamba (kushoto)kumueleza Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi,Shamsi Vuai Nahodha(wa pili kulia)kuhusu kampuni yake,wakati waziri huyo alipotembelea kampuni hiyo ikiwa ni sehemu yake ya ziara kwa kampuni mbalimbali binafsi za ulinzi na uokoaji,Dar es Salaam
Wanajamii forum kweli misaada kutoka nje ina tudhalilisha sana. We need to stand for our dignity and our nation

Mbona Polisi Mkuu anachekelea kama anaomba radhi vile? Au naye yupo kwenye pay roll ya kaburu?
 
Hivi tujiulize hawa makaburu wanavyokua na kiburi hivi ndani ya nchi yetu je haya makampuni waliyowekeza yapo kwa ajili ya msaada au pia na wao wanapata faida? Maana naona kama hapo labda anamwambia waziri kama hutaki mi nafunga kampuni yangu. Kwani hakuna watanzania wenye uwezo wa kuendesha makampuni kama haya? Wapi WAITARA, wapi MBOMA, wapi TIBAIGANA? Hawa ndo watu wangetakiwa waachane na mambo ya siasa na kusaidia nchi yetu kumiliki kampuni za ulinzi kama hizi maana kidogo wana uzoefu.
TANZANIA TUMEKUA WATULIVU KIASI KWAMBA SASA TWAJIZALILISHA NA KUJIFANYA WATUMWA DHIDI YA WATU FULANI NDANI YA NCHI YETU
Kashfa zote kubwa za rushwa zinazotafuna nchi yetu na kuendelea kutuongezea garama za maisha zinashirikisha watu kutoka nje kwa asilimia kubwa. Si maanishi tuwafukuze wageni ndani ya nchi yetu but lazima tujifunze namna ya kuishi na hawa watu.
 
Hivi mwenye nyumba hua hizi taarifa anazipata kweli?
Huu ni uwekezaji wa aina gani wa kutufanya watanzania watumwa wa nchi yetu kila sekta?.... Hii type ya wazungu nahisi inatokea south africa maana ndo hua hawana nidhamu kwa black people hua wanatuona kama wanyama pori. Na ndo maana ubaguzi bado south africa unaendelea.
Sidhani kama kuna mzungu anatoka nchi za ulaya au amerca anaweza kua na nidhamu ya namna hii.
Iam loosing confidence to my country.

Akizipata atafanya nn, Zile Elkopter na garama za uchaguzi unajua alizozichangia? unajua wana hisa wa hizo kampuni? wacha kabisa hio maneno sisi nio mabwege and we should accept that.....
 
Wewe unamuona huyo tu tena anatoa huduma kwa jamii japo ya kulipia. Matusi tunayotukanwa na Rostam, Somaiya + our brothers EL etc ni madogo?
 
Mbona hata wao (mambo ya nje/polisi) wanatudharau wananchi hata kufikia kupiga wabunge/mbunge wetu?
wao wakidharauliwa mi kwangu poa. siku hizi hata sipendi kuwaona wakikatisha mbele yangu.
 
Akizipata atafanya nn, Zile Elkopter na garama za uchaguzi unajua alizozichangia? unajua wana hisa wa hizo kampuni? wacha kabisa hio maneno sisi nio mabwege and we should accept that.....

Hapa kaka kweli umenikumbusha kitu.
 
Mbona hii imekaa kiudaku na uchochezi? Huyu mzungu kwenye picha anaonyesha akitowa point na hawa maafisa wetu wanaonyesha wamefurahi wanacheka (chekelea). Sasa hapo ni wapi anapotishia kuondoka?

Hii habari, sijui?

Watu huwa wanachekelea point??? Omba source kwanza badala ya kuanza kusema inaelekea anatoa point na jamaa wanachekelea. Hao jamaa wapo kazini siyo kwenye kahawa na kashata.
 
Back
Top Bottom