Jacque George
New Member
- Nov 4, 2010
- 3
- 0
Yaani taifa la Tanzania tunakoelekea siko.matokeo ya uchaguzi yanatumia muda wa wiki moja nzima!hatuna budi kujiuliza ya kwamba kwa nini chaguzi zilizopita zilikuwa zikifanyika kwa muda mfupi tu na matumizi ya kompyuta kwa wakati huo yalikuwa madogo,inakuwaje uchaguzi huu wa 2010 watu wenye elimu zao katika matumizi na kuziganga kompyuta zinapopata maradhi ya kila aina wanashindwa kumaliza kazi kwa wakati? Hivi kuna umuhimu wa kuweka uchaguz wa wabunge wa vyama vingi kama hakuna demokrasia? Kwa uelewa wangu haiwezekani kwamba tathmini za uchaguzi zikaonesha asilimia ndogo za uhuru na uhalali wa zoezi zima la uchaguzi na tume ikayapitisha matokeo ya uchaguzi.Hata wenzetu wahisani wanatushangaa na bado kidogo tu watatuchoka kwa kuendekeza hayo 2nayowakumbatia na kuifanya nchi ni kama ya urithi wao.lazima tukubaliane na tufanyie kazi chanya changamoto zilizopo na si kuendelea na mfumo wa uchaguzi wa kichwa na mwenge!