Hii ndoa inanivunja moyo, najuta kwanini nilimuoa huyu mwanamke

Habari wanajamvi, naombeni tumshauri huyu mwenzetu, kanisimulia mkasa wake mimi kama rafiki yake wa karibu sana
Huyu ndio tabia yake, anapenda sana kufuatilia simu yangu. Wakati mwingine anaiba simu yangu anachukua namba, anaanza kuwapigia watu anaoona calls zimeingia sana. Ana wivu wa kitoto sana
Jamaa we mwongo Sema ukweli bibie kakuta unaongea simu na mchepuko maana hata maandishi yako unaonekana ni uwongo.Unabahati umepata mwanamke hana hasira kakuchana na kisu kidogo laiti ningekuwa mimi ningehakikisha nakata kitendea kazi.
 
upo sahihi mkuu, lakini elewa kwamba, mimi najitambua, ningekuwa sijamheshimu ningeongelea hili suala mbele yake kule chumbani. Yeye ndo alinyata kunifuata kunisikiliza naongea nini na nan? lakini hakuwa na subira, angekuwa na busara angesubiri nimueleze pia ningempa aongee na yule dada

Ubongo wa mwanaume na mwanamke unavyofanya kazi ni vitu viwili tofauti kabisa..
Mwanamke hana subira hiyo mkuu inatakiwa uelewe utendaji kazi wa ubongo wao.

Wewe ndio mwanaume unasimama kama mkuu ndio mana ulipewa heshima ya kukojoa huku umesimama kwa ajili ya kuangalia usalama na kesho yake.
Sasa ukikimbia matatizo unazani nani atayatatua..??

Kwenye kikao mwanamke atasema nilimskia anasema nakuja kulala kwako leo
 
Habari wanajamvi, naombeni tumshauri huyu mwenzetu, kanisimulia mkasa wake mimi kama rafiki yake wa karibu sana. Ila nimeona nishare nanyi ili tupate mawazo murua. Nitasimama katika huu uzi kwa niaba yake. Mtanisamehe kwa maelezo haya mengi, ila ili umshauri ni vema usome uzi huu wote.

NB. For great thinkers only, if you are a small thinker stay away from this thread.

ILIPOANZIA JANA 12/09/2019
Alfajiri nimeamka nikakuta sms katika simu yangu. Ujumbe ulisomeka hivi "habari, sorry ukiwa free na ukiiona sms hii naomba unipigie, ni muhimu sana".

Ni dada ambaye ninafahamiana nae sana (long time back). Nikachukua simu, fasta nikaenda sebuleni ili nimpigie nijue kuna tatizo gani. Kumbee! mimi bila kujua, mke wangu kanyata kimya kimya kunifuata nyuma....

Nikampigia simu yule dada, akanambia anaumwa sana, nimkopeshe fedha ili akapate matibabu. Katika kumuuliza sana unaumwa nini!,. akanambia anahisi ni amechezewa na waswahili maana ni miezi miwili mfululizo anableed!

Nikamhoji, kwa nini anahisi kachezewa! akanijibu, anajua fika atakuwa amechezewa maana kuna siku alianika nguo zake nje, mda wa kuja kuzichukua alibaini nguo zake mbili tu za ndani hazipo (zimeibiwa).

Ghafla bin vuu! hata sijamaliza kuongea nae, WIFE kapokonya simu huku kafura kwa hasira na maneno yakimtoka ."malay* mkubwa weeee, yan unaongea na demu wako kuhusu MP huoni hata aibu, mseng* mmoja wee".

Nikamfuata ili nichukue simu niikate(ilikuwa hewani bado) afu nimuelezee hali halisi, akaibamiza chini, PAAAAAH.........Busara niliweka kando, nilimpa kerubu mbili matata,(nakiri sijawahi kumpiga kabla)........Nae akanivamia, nikamsukumia kwenye sofa nikaokota simu kwa hasira nikaenda chumbani kujifungia.

Punde si punde, yupo mlangoni..."KAMA WEWE MWANAUME KWELI FUNGUA MLANGO"...mh, nikaona hii dharau sasa, huyu anajiamini nn!!!!.....Nimeanza kufungua mlango tu, aaahmad!!!!, kabeba mtwangio wa kinu na KISU.

Nikataka nipush mlango ili niubane tena, akanisogezea knife, akanichana kwenye mkono(my arm).

Nilipata hasira sana yani sana.....nikampa kibao kizito cha shavuni, alitoka ndukiii akasahau hadi zana zake....breki ya kwanza jikoni.....

Sikumfuata, fasta nikatafuta leso ili nijifunge jeraha(maana damu ilikuwa inamwagika).


MUDA SI MUDA, karudi tena hadi mlangoni, akanifungia kwa funguo kwa nje. "Leo hutoki kabisa, utakaa humo humo ndani, NI NANI ALIYEKWAMBIA MWANAMKE ANAPIGWAA" . Aliendelea kupayuka pale nje, maneno yote yalimtoka.
Alivyoona simjibu , akaenda nje, akafunga geti, akarudi sebuleni, akajifungia kwa ndani.

Nilikaa takribani nusu saa nikimsihi anifungulie ili nijiandae niwahi kazini, KIMYAA!!!!.

Nikachukua simu yangu ndogo, nikampigia boda boda aje na fundi seremala na zana zote za kuvunjia vitasa. Nikapaki baadhi ya nguo katika begi langu la mgongoni (nilijiapia sirudi home).
Fundi alipofika, nilimpa maelekezo, akaruka uzio. akatindua kitasa.....nikamalizana nae pamoja na boda boda.


Nilijiandaa, nikabeba na begi.. nikazunguka dirishani nikamwambia mke wangu *"NAONDOKA, SITARUDI KWA SABABU UMENISHIKIA KISU UNA LENGO LA KUNIUA".
huyooo, nikaepa..

Muda wa mchana alinipigia simu sikupokea maana ilikuwa kwa fundi inatengenezwa. Akaja kazini kwangu(nimejiajiri) hakunikuta. Akawapa maagizo wafanyakazi wangu nikifika wanipe taarifa kuwa yeye alifika pale kuniulizia. Kwa kweli sikumtafuta kabisa hiyo jana, na home sikurudi, nililala kwenye chumba nilichompangia mfanyakazi wangu wa kiume.


LEO ILIPOFIKIA 13/09/2019
Simu za wana ndugu zimefululiza hapa na sijapokea, nimepokea ya mama tu. Akanambia amepokea malalamiko kuwa nimempiga mwenzangu, na nimehama na nyumba.!!!!!!!
Nimemwomba mama nimpigie badae jioni kwa sababu asubuhi nilikuwa nimetingwa nahudumia wateja(ila pia nilikuwa sijaona nimweleze nini)

MAELEZO YA ZIADA
I. Huyu mke wangu ni reporter sana yaani nahisi hata wanandugu washaanza kumchoka, ugomvi kidogo tu, atasimulia home kwangu na kwao.
Pia ifahamike kwamba yeye pia ni binadamu, huwa ananikosea lakini mimi huwa namchukulia the way alivyo.

II. Huyu ni mke wangu wa ndoa katoliki , ndoa ni ya mwaka mmoja sasa


HAYA WANAJAMVI
ungekuwa wewe ungemshauri nini huyu ndugu?

pia wewe great thinker una maoni gani kuhusu changamoto hii aliyoshare nawe?
Alooh hali si hali!!
 
Mtwangio na kisu...shemeji alipitia jkt nini..

Turudi upande wako unamskia mke wako anaongea na simu na mwanaume alafu mwanaume anamwambia kuwa mboo yake inasimama usiku kucha amkopeshe hela aende hospital ungejiskiaje mkuu ??

Tena wewe ulivyomkorofi nahisi ungemuangushia ukuta ili afe kabisa..
Hapo kuwa mwanaume tumia akili mshape mke wako acha kumsingizia kuwa ni reporter sana hiyo ndio asili yao wanawake hawana koromeo.
Mwanaume hakimbii nyumba rudi nyumbani kaa na mkeo vizuri mpe maneno matamu tamu ye mwenyewe atapiga simu kwa mama ake na kumwambia mama nilikua nakutania.

Ungekua daktari na huyo dada ni mgonjwa wako kusingekuwa na shida
Mama nilikuwa nakutania
 
Ndoa nyingi sana sikuhizi ni Ndoano. Wanandoa wamepoteza nyuso za furaha muda wote wana mawazo sana, Wengine hudiriki kusema hadharani najuta kuoa/kuolewa na mtu huyu. Mungu awajaalieni busara za kuziishi ndoa zenu na Akili ya utatuzi wa changamoto mnazopitia.
 
Mkuu! mke anasameheka kwa kila jambo au kosa alifanyalo pasipo kujali chochote maana sisi wanaume huwachukulia kama watoto tu. Ila wasi wasi wangu ni hizo mbinu zake za kujihami siyo nzuri kabsa maana ipo siku kama utani atatoka na utumbo wako, Ogopa sana mtu anayetumia dhana za vita.. Hebu kubali kosa lako mbele ya wazazi wako plus wazazi wake then muulize why alifanya ivo? Uliza kama kwake ni sahihi kusimama mbele yako na hizo dhana? pia hoji kama wew ukizitumia ni sawaa kwake?, Then waachie wazazi wake wamkanye kwa hicho kitendo na uumpe mashariti yako katika nyumba yako mbele ya wazazi wote na mwelekeze haki yake anatakiwa aombe vipi endapo ataona anaonewa. Samehe rudi kuishi na mkeo mpya.
 
Mweleze Ukweli Kuhusu Simu Uliyokuwa unaongea nayo. Muweke Wazi na Umkanye Kwamba sio Kila ugomvi Wenu Lazima aupeleke Kwa ndugu. Mwambie haikukupendeza yeye kukushikia siraha. Jioni Ukirudi mletee kijizawadi Kisichozidi buku, Mwambie Unampenda na Unafanya hivyo Kwa maslahi ya ndoa yenu (huenda Mkeo anakupenda, ana wivu na wewe ila tu hakuamini maana hatujamskiliza na yeye). Mpe mwaka mwingine wa uangalizi.

Mwisho Kabsa,KUWA MWANAUME
 
Jamaa we mwongo Sema ukweli bibie kakuta unaongea simu na mchepuko maana hata maandishi yako unaonekana ni uwongo.Unabahati umepata mwanamke hana hasira kakuchana na kisu kidogo laiti ningekuwa mimi ningehakikisha nakata kitendea kazi.
angekuwa ni mchepuko kweli, nisingeona sababu ya kuficha. Nimuhofu nani huku nipo behind keyboard
 
Ubongo wa mwanaume na mwanamke unavyofanya kazi ni vitu viwili tofauti kabisa..
Mwanamke hana subira hiyo mkuu inatakiwa uelewe utendaji kazi wa ubongo wao.

Wewe ndio mwanaume unasimama kama mkuu ndio mana ulipewa heshima ya kukojoa huku umesimama kwa ajili ya kuangalia usalama na kesho yake.
Sasa ukikimbia matatizo unazani nani atayatatua..??

Kwenye kikao mwanamke atasema nilimskia anasema nakuja kulala kwako leo
Sina mpango wa kukaa kikao, ni kuwapotezea muda ndugu. Ila nitakuwa tayari kwenda ikiwa atalipeleka hili suala ktk neutral platform namaanisha kanisani
 
upo sahihi mkuu, lakini elewa kwamba, mimi najitambua, ningekuwa sijamheshimu ningeongelea hili suala mbele yake kule chumbani. Yeye ndo alinyata kunifuata kunisikiliza naongea nini na nan? lakini hakuwa na subira, angekuwa na busara angesubiri nimueleze pia ningempa aongee na yule dada
Mkuu wala sitaki ujitete hapo uliteleza kumpa confidence huyo mkewe ungeongea mbele yake halafu umpe maelezo kwa ufupi nani amekupigia simu sababu huyo ndo mwandani wako.....pole sana lakini
 
aah mkuu, mimi mwenyewe sikuamini kama angebeba hadi kisu, nikajisemea huyu kama kadiriki kuja na kisu live atashindwaje kuniwekea sumu kwenye chakula
Pole mkuu kumbe ni wewe nilidhani ni rafiki as you said.
 
22 Reactions
Reply
Back
Top Bottom