Hii ndo sheria itakayowashughulikia wale wanaopenda kutuma picha chafu mtandaoni

RWANDES

JF-Expert Member
Jun 12, 2019
1,615
3,909
ISOME SHERIA HII UIELEWE KABLA RUNGU HALIJAKUFIKIA
IMG-20190905-WA0002.jpeg
 
Serikali kabla ya kutunga sheria na kuanza kutumika ingekuwa ni vizuri ikaelimisha wananchi kwa kuweka matangazo kwenye Radio na TV.

Kuna wananchi wengi watajikuta wakilipa faini au kufungwa gerezani kwa sababu ya kutenda kosa bila kujua.

Ninajua ujinga sio utetezi lakini serikali lazima itumie hekima na busara kabla ya sheria kuanza kutumika.
 
Serikali kabla ya kutunga sheria na kuanza kutumika ingekuwa ni vizuri ikaelimisha wananchi kwa kuweka matangazo kwenye Radio na TV.

Kuna wananchi wengi watajikuta wakilipa faini au kufungwa gerezani kwa sababu ya kutenda kosa bila kujua.

Ninajua ujinga sio utetezi lakini serikali lazima itumie hekima na busara kabla ya sheria kuanza kutumika.

Ni kweli...kama yule Mtanzania kule Uingereza alijikuta yuko lupango kwa kusambaza picha za wahanga wa tukio la kigaidi...hapa kwetu zile picha za wahanga wa moto wa lori pale Morogoro zilisambazawa kwenye mitandao...Elimu ni muhimu kwa kweli ingawa kama ulivyosema 'ignorancce of the law is no defence'
 
Ni kweli...kama yule Mtanzania kule alijikuta yuko lupango kwa kusambaza picha za wahanga wa tukio la kigaidi...hapa kwetu zile picha za wahanga wa moto wa lori pale Morogoro zilisambazawa kwenye mitandao...Elimu ni muhimu kwa kweli ingawa kama ulivyosema 'ignorancce of the law is no defence'
Kwa sasa ukiongea na watu wengi hasa huku kijijini wanasema siku hizi sheria ni nyingi sana!

Wengi wanadhani sheria nyingi zimetungwa katika utawala wa awamu ya tano bila kujua kuwa hizi sheria zilikuwepo muda mrefu lakini zilikuwa hazisimamiwi kikamilifu.

Nimegundua kunahitajika elimu ya sheria kwa kiwango kikubwa sana hasa vijijini kabla ya kuanza kuitumia.
 
Back
Top Bottom