Hii ndo mistari ya bongo fleva iliyoandikwa na mwanafunzi wakati akifanya mitihani ya kidato cha 4

Imefika wakati sasa kuwe na vibali vya kuwa msanii iwe wa bongo fleva au movie ili wajue ubora wa elimu tena form six kigezo nadhani haya matitizo yatapungua
 
Dogo kalamu hataki, anakipaji cha kurap ebu akuzwe ktk kipaji chake. Kina Jay Z walitokea huku.
 
Wazazi wa siku hizi hawataki kulea watoto wao! Sio wababa wala wamama, kukimbizana na starehe za mjini jumatatu hadi jumatatu!
Kila mtu anavuna alichopanda, I'm sure report cards za mtoto kama huyu zilikuwa kila temu zimeandikwa na kupelekwa kwa mzazi.
Unamuongelea hasa mzazi gani? maana usije ukawajumlisha na wale wa kwetu ambao uwezo wao umeishia kutupeleka shule ya kata, mwalimu mmoja masomo yooote, hakuna kitabu cha kiada wala ziada, hakuna maabara, hakuna madawati. Report card ikija nimfanyeje mtoto sasa?

sekta yetu ya elimu jamani inasikitisha, aseme tu yule ambaye haya madhara hayajamgusa kwa njia moja au nyengine,

Navyoandika hapa namfikiria binti ambaye yuko so eager to learn na mzazi uwezo ndo umeishia shule ya kata, kesho sitashtuka akiandika madudu zaidi ya hayo kwenye majibu yake.
 
Na utashangaa progress reports zake zilikuwa zinaonyesha performance nzuri tu. Mimi ninasikitika kwani ninahisi wengi wetu tumepoteza ile maana halisi ya elimu. Mwalimu anafundisha lililopo kwenye silabasi, mzazi anakagua madaftari kuona kama kile kilichofundishwa kinafundishika ilhali tunasahau kuwahimiza wanafunzi/watoto wetu umuhimu wa yeye kusoma. Nafikiri elimu ya sasa inachukuliwa kama just another stage katika kukua, kwamba ulizaliwa, unatakiwa utambae, utembee, usome uwe mkubwa basi na katu hatuichukulii kama ni nyenzo muhimu kwa mafanikio ya baadae.

Hata huyu mwanafunzi angeelewa umuhimu wa elimu hata kwenye hiyo bongo flava yake asingefanya madudu haya.
Nakubaliana na mdau aliyelihusisha tukio hili na bange oitherwise mwanafunzi ashindwe hata kuandika definition tu!!! kuna tatizo.
 
Mkuu, tukubali tukatae, shule za kata ni janga la Taifa. Nimecheki shule za kata kutoka kwenye wilaya yangu, waliofaulu kwa kiwango cha juu wameanzia division three. Wengi wamefeli! Cha ajabu, shule nyingine katika wilaya hiyo hiyo ( za dini na zile za serikali proper) zimefanya vizuri. Nawasikitikia sana hawa vijana wanaopangiwa shule za kata. Wanapotezewa muda!!
Haswa ni kuwapotezea watoto muda, sijui serikali wanaangalia wapi kwa kweli...
Walitegemea matokeo tofauti na haya btw? I guess not...
 
inasikitisha sana..lakini kama uongozi husika hauta chukua hatua kwa hao watoto itakua ndo mchezo wao maana wanajua hakuna wa kuwaadabisha. Necta wanajua hao watoto ni wa shule gani so wawatoe hadharani kwenye vyombo vya habari ama sivyo na hawa wa form six nao watakuja na verse zao..:hatari:
 
tunashabikia upuuzi tutaishia kuwa na taifa gani hapo baadae uwapo kila kijana anafikiri atatoka kwa muziki tu..no wataalam wa fani tofauti,hivi kweli wewe unayejiita msanii unasema kioo cha jamii utailimishaje jamii wakati wewe mwenyewe hukuelimika?
BASATA ipo wapi wakati under eighteen wanaingia kumbi za starehe na pia studio kurekodi commercial musics?
Hatukatai vijana kukuza vipaji au kushiriki matamasha ya kijamii na sio kushiriki show za burudani huki wakiangaliwa na wenzao kupita luninga kwa vyovyote itawapa hamasa wengine kutozingatia masomo ambayo ni msingi wa maisha
 
Hii ni mbaya kuliko kwani nidhamu ni moja ya vigezo vya mwanafunzi bora hivyo kwa huyo hakuna lolote alilojifunza .Mazingira yanachangia kwani waliondoa mitihani ya form 2 wanapitisha watoto wasio jitambua.Serikali inatakiwa kuwapa huduma za uhakika wananchi wake
 
Tujitizame upya kama taifa! huko tunapo elekea maadili ya wajukuu zetu....itakuwa balaa! kuna mambo mengi yakurekebisha, issue si utandawazi tu! je watanzania wanajitambua? na kunamifumo gani yakuaanda jamii zetu kukabiliana na changamoto za maisha?
 
Inawezekana dogo alikua anajibu kwenye mtihani wa kiswahili, sasa akawa anaandika mashahiri. Inawezekana wasahihishaji hawakufurahishwa na majibu yake lkn mashairi anayo yajua ndo ya kizazi cha sasa ... bongo fleva.

By the way, ninaamini kuna watoto wanapelekwa shule ili wakue kiumri lkn sio ili apate chchote cha maana. Unakumbuka Steve Jobs alisema alishindwa kuendelea na masomo kwa kukosa ada? Baadae akagundua maisha mbadala ya yale ya formal education yalikua more interesting? Sasa inawezekana dogo kipaje chake ni mistrari, na mfumo wa elimu hautoi support ya hiyo kitu ... mi nahisi mziki utamtoa tuu ... ndio anachokijua na kukiweza! Simpingi wala simuungi mkono, ni maoni yangu tuu.
 
Ndugu Zangu Watanzania;

Si jambo geni hili, labda huenda mwaka huu limeongezeka ndio maana wameamua kuliweka wazi, au kutokana na matusi yamewashitua.

:photo::photo: Ninayoipata hapa ni kwamba tatizo hili limetokana na Kuvuja kwa Mitihani,

Hao Baraza wakichunguza vizuri watakuta kuwa hiyo mitihani yenye majibu ya utumbo ni lazima ilikuwa imevuja. Sasa MWanafunzi alipata paper na akalitafutia majibu kabla ya kufika chumba cha mtihani. Akiwa anajiaminisha MIA KWA MIA kufanya vizuri, anafika ndani ya chumba kufunua karatasi anakuta SIYO PAPER ALIYOIONA KABLA!!!!!!! :lol::lol::lol:

Ndipo hapo mtu anakosa jibu na anachanganyikiwa na kufikia kufanya mambo kama hayo.

Katika hili pande zote ni za kulaumiwa (1) Wanafunzi (2) wazazi (3) Walimu (4) Baraza la Mitihani

Wazazi tunachangia kiasi kikubwa kwani tunashiriki katika kuwapa pesa ili wanunue mitihani. Ili tu mtoto afaulu na kujiona ni sifa mtaani. kumbe tunamjengea msingi mbovu na matokeo yake ni haya.

Wanafunzi wanachangia kwa uvivu wa kutojibidisha kimasomo kwa kutegemea kununua mitihani.

Waalimu wanashiriki kiasi kikubwa, kwani kuna baadhi ya shule Walimu wanawatafutia mitihani ili watotot wafaulu wengi na shule ipate sifa kwa kupata alama za juu kitaifa, kumbe tunawaharibu watoto badala ya kuwajenga.

Baraza la Mitihani kuna wafanyakazi ambao siyo waaminifu, kwani wao kwa tamaa ya pesa wanatoa mitihani na kuiuuza.

Hivyo hili tatizo tusimlaumu mtoto peke yake kwani kuna Chain ndefu iliyoshiriki katika hili. Mtoto amefika na kukuta mtihani siyo aliotegemea, Je, tunafikiri atajibu kitu gani na ikiwa alitegemea shwali la kwanza ni Multiple Choice kumbe kufika pale anakuta hakuna Multiple Choice kuna ESSAY tupu mwanzo mwisho.

Kwa nini asiandike matusi yaani kumtukana aliyebadilisha mtihani!!!!!!!

Sote tujirekebishe katika nafasi zetu tulivyoshiriki kumfanya mtoto aandike utumbo huu.

MIZAMBWA
INANIUMA SANA!!!

Mkuu umetoa hoja na kujipinga mwenyewe ... hiyo red na blue haviongei lugha moja. Sasa ni mtihani gani unavuja kama mtahiniwa akiingia kwenye chumba cha mtihani anakuta mtihani tofauti?
 
Mtu mzima anasema waziwazi kuwa Kufeli skonga sio kufeli maisha, sa unafikiri mipoyoyo km hili litafanya nini zaidi ya kufikiri ubongo ulio na fleva utalitoa
 
hivi kama mama yake role model wake ni Madam Ritha

na kipindi cha familia ni bss...mnategemea nini??????
 
1 Reactions
Reply
Back
Top Bottom