Consigliere
JF-Expert Member
- Sep 9, 2010
- 12,038
- 24,595
Harusi za kibongo, ni kivutio kingine cha utalii japo zinazidi kutufanya tubaki maskini wa akili na maendeleo.
Hebu tufikirie kwa pamoja, kwa tukio la harusi tu unakusanya watu zaidi ya mia moja, na wote wanapatikana, koz hawana jambo la maana la kufanya (they have a lot of spare time), wanaandamana na maharusiui wanapokwenda kufunga ndoa, iwe nyumbani au kanisani.
Then mnakwenda kupiga picha baharini, mkitoka hapo mnakwenda kupiga picha Mlimani City, munaendelea kutafuta kila eneo na jengo zuri lilopo mjini ili mpige nalo picha, mtawashawishi wazungu na waarabu mpige nao picha, then mnakwenda ukumbini, hapo maharusi munawekwa mbele kama vinyago vya mapambo au kombe siku ya fainali.
Munatekeza millions of money per night achilia mbali zilizokatikia kwenye vikao vya maandalizi. Mbwembwe ni nyingi zinafanya Harusi zionekane ni za kifalme, hata wageni waingiao nchini hujikuta wakishangaa kwa kutojua nini kinatokea na waambiwapo kuwa ni sherehe za harusi, hujikuta wakisikitika sana kwa kudanganywa kuwa Tanzania ni maskini wakati wanachokishuhudia ni tofauti.
Maisha yanaendelea na maharusi wanarudi mitaani au maofisini ambapo utamaduni wetu wa kupigana mizinga unaendelea kama kawaida, mmoja wa maharusi anapoumwa hakuna wa kujitokeza linabaki suala binafsi, Mungu anaibariki ndoa na watoto wanapatikana wakati wa kuwapeleka shule unapofika na uchumi kutokuwa mzuri hakuna mchangiaji anaejitokeza kusaidia wanasema kila mtu na abebe mzigo wake.
Watoto wakifika muda wa kuoa au kuolewa hapo ni suala la ku-report kwenye kamatiza kudumu za harusi zilizoundwa.
Hivi jamani kwa nini kamati hizi za kijamii zisingekuwa kwa ajili ya maendeleo ya kielimu ya vijana wetu, milioni 25 tunazoziteketeza kwa tukio la siku moja unadhani zingesomesha wanafunzi wangapi.
Misaada tunayoipata kutoka kwa nchi wafadhili ieleweke kuwa ni matokeo ya raia wa nchi hizo kuamua kujibana na kubadili mfumo wao wa maisha kimatumizi ili waweze kutusaidia sisi katika mambo mbali mbali ya kijamii. Kwanini sisi tunashindwa kufanya hivyo kwa ajili yetu wenyewe.
Kama kuna kitu kinaitwa kubana na kupunguza matumizi au matumizi yenye nindhamu basi na kianzie kwetu binafsi na ndani ya familia zetu, bila ya hivyo tabia hii itakua , kukomaa na kuwa sugu, na kujikuta na sisi bila ya kujijua tumejiandaa kwa muda mrefu kuwa aina fulani ya wafujaji ambao tunasubiri kugeuka kuwa mafisadi.
Behaviors are only comfortable but behavior change is possible.
Tujiulize na kufanya maamuzi ya busura tungali vijana kwa maendeleo yetu na vizazi vijavyo
Hii ndiyo Tanzania, zaidi ya ile unayoifahamu.
Hebu tufikirie kwa pamoja, kwa tukio la harusi tu unakusanya watu zaidi ya mia moja, na wote wanapatikana, koz hawana jambo la maana la kufanya (they have a lot of spare time), wanaandamana na maharusiui wanapokwenda kufunga ndoa, iwe nyumbani au kanisani.
Then mnakwenda kupiga picha baharini, mkitoka hapo mnakwenda kupiga picha Mlimani City, munaendelea kutafuta kila eneo na jengo zuri lilopo mjini ili mpige nalo picha, mtawashawishi wazungu na waarabu mpige nao picha, then mnakwenda ukumbini, hapo maharusi munawekwa mbele kama vinyago vya mapambo au kombe siku ya fainali.
Munatekeza millions of money per night achilia mbali zilizokatikia kwenye vikao vya maandalizi. Mbwembwe ni nyingi zinafanya Harusi zionekane ni za kifalme, hata wageni waingiao nchini hujikuta wakishangaa kwa kutojua nini kinatokea na waambiwapo kuwa ni sherehe za harusi, hujikuta wakisikitika sana kwa kudanganywa kuwa Tanzania ni maskini wakati wanachokishuhudia ni tofauti.
Maisha yanaendelea na maharusi wanarudi mitaani au maofisini ambapo utamaduni wetu wa kupigana mizinga unaendelea kama kawaida, mmoja wa maharusi anapoumwa hakuna wa kujitokeza linabaki suala binafsi, Mungu anaibariki ndoa na watoto wanapatikana wakati wa kuwapeleka shule unapofika na uchumi kutokuwa mzuri hakuna mchangiaji anaejitokeza kusaidia wanasema kila mtu na abebe mzigo wake.
Watoto wakifika muda wa kuoa au kuolewa hapo ni suala la ku-report kwenye kamatiza kudumu za harusi zilizoundwa.
Hivi jamani kwa nini kamati hizi za kijamii zisingekuwa kwa ajili ya maendeleo ya kielimu ya vijana wetu, milioni 25 tunazoziteketeza kwa tukio la siku moja unadhani zingesomesha wanafunzi wangapi.
Misaada tunayoipata kutoka kwa nchi wafadhili ieleweke kuwa ni matokeo ya raia wa nchi hizo kuamua kujibana na kubadili mfumo wao wa maisha kimatumizi ili waweze kutusaidia sisi katika mambo mbali mbali ya kijamii. Kwanini sisi tunashindwa kufanya hivyo kwa ajili yetu wenyewe.
Kama kuna kitu kinaitwa kubana na kupunguza matumizi au matumizi yenye nindhamu basi na kianzie kwetu binafsi na ndani ya familia zetu, bila ya hivyo tabia hii itakua , kukomaa na kuwa sugu, na kujikuta na sisi bila ya kujijua tumejiandaa kwa muda mrefu kuwa aina fulani ya wafujaji ambao tunasubiri kugeuka kuwa mafisadi.
Behaviors are only comfortable but behavior change is possible.
Tujiulize na kufanya maamuzi ya busura tungali vijana kwa maendeleo yetu na vizazi vijavyo
Hii ndiyo Tanzania, zaidi ya ile unayoifahamu.