Pukudu
JF-Expert Member
- Jan 7, 2011
- 3,148
- 2,219
Huwezi jua sababu wewe unaangali mpira kwenye tv timu imesafiri kutoka Mara imeenda Mbeya,hujui gharama zikoje.
Milioni 3 kwa mwezi?? Inasaidia nn sasa
Huwezi jua sababu wewe unaangali mpira kwenye tv timu imesafiri kutoka Mara imeenda Mbeya,hujui gharama zikoje.
yaani hiki kidem kitaua soka la bongo, wait and see
Mkuu wenye ligi yao hadi sasa wamekiri GSM hajatoa hata mia kwa vilabu, sasa hapa sijui unaongelea nini!? Ili mpira wetu uendelee basi mikataba ya kihuni tuungane kuikataa tusipelekwe kishabikiHuwezi jua sababu wewe unaangali mpira kwenye tv timu imesafiri kutoka Mara imeenda Mbeya,hujui gharama zikoje.
Hata mimiMwamedi amefurahishwa sana leo
Kabla jiesiemu adhamini, timu zilitembea kwa miguu? Ama timu hazikusafiri?Huwezi jua sababu wewe unaangali mpira kwenye tv timu imesafiri kutoka Mara imeenda Mbeya,hujui gharama zikoje.
Hongera sanaHata mimi
Hakuna mfanyabiashara atakayepoteza fedha zake kuvidhamini vilabu vingine kama tayari anaidhamini Simba. Mo kwake Simba inamtosha zaidi ya vilabu vingine vyote 15 vilivyobaki. Bakhresa alipanda dau la uwekezaji hadi sh. 25B ili kumpiku Mo, sema tu wanachama walimchomolea. GSM amejaribu kuzunguka ili aipate Simba kupitia vilabu vingine 15, ila ameikosa. Kwa hiyo wafanyabiashara nchini target yao ni kudhamini au kuwekeza Simba. Sasa kwa hali hiyo, kwa nini Mo ahangaike kuidhamini ligi yote wakati Simba anayo tayari?Mwambieni Mudi awe mdhamini sasa.
Mikataba wa NBC na Azam timu zilishirikishwa kiasi gani!?jibu swali. timu kuwa na hali ngumu ndio sababu ya TFF na GSM kutoshirikisha hizo timu ikiwepo baba lao Zimba? 🤣🤣🤣🤣
Acha kuhamisha magoli
Watalipa tff,waliocomitt kwamba timu zote zitavaa,wakashindwa kuilazimisha Simba ivae
[https://res]Kampuni ya GSM imetangaza kujiondoa katika udhamini mwenza wa Ligi Kuu Tanzania Bara, hiyo siyo habari mpya kwa sasa, lakini kilichopo nyuma ya pazia na sababu kubwa ni wapinzani wao wa jadi Simba kugoma kuunga mkono juu ya udhamini huo.
Mara baada ya TFF kutangaza udhamini huo, kisha ikaelezwa kuwa klabu zote shiriki katika ligi hiyo kutakiwa kuvaa jezi zenye nembo ya GSM, Simba wao waliibuka na hoja kadhaa kisha wakagoma kutii maelekezo hayo ya TFF na Bodi ya Ligi.
Moja kati ya hoja za Simba ilikuwa ni kutoshirikishwa wakati wa kusainiwa kwa mkataba huo, GSM kuwa ni mdhamini wa Yanga wakati huohuo kuwa mdhamini mwenza wa Ligi Kuu na nyingine kadhaa.
Barbara ambaye ni Mtendaji Mkuu wa Simba ndiye ambaye alilishikilia bango suala hilo kwa niaba ya klabu na kuiandikia barua TFF, pia klabu yake haikushiriki katika kuvaa jezi zenye nembo ya GSM.
Licha ya kuwa GSM hawajasema wazi kuhusu masharti ya mkataba ambayo wanaona yamekiukwa katika makubalano yao lakini ni wazi kuwa Simba ndiyo sababu hasa ya wao kuamua kujiondoa.
Chanzo kutoka GSM kimeeleza kuwa kitendo cha Simba kugomea kuvaa jezi zenye ‘brand’ ya GSM kisha TFF na Bodi ya Ligi kushindwa kuwachukulia hatua, huku kesi ya udhamini wao ikipelekwa FCC ndiyo sababu ya kuamua kujiondoa.
Kesi hiyo ilifikishwa FCC kwa kuwa serikali iliamua kuingilia kuona kama mchakato wa fair competition ulikuwa katika njia sahihi.