Hii ndiyo sababu yangu Kuu kwanini nimerudi Kuiabudu Mizimu na Kuwachoka Wahubiri wengi wa Kiroho na Matapeli waliopo sasa Tanzania

GENTAMYCINE

JF-Expert Member
Jul 13, 2013
56,054
107,538
Hakuna ambaye kila ' akihubiri ' anakusisitiza Ushike neno na uamini katika Mungu Baba bali wanatulazimisha tuwaamini wao tena 100% utadhani ndiyo Wameniumba GENTAMYCINE wakati kumbe aliyeniumba ni Mungu wa Ibrahim, Isaka na Yakobo.

Sasa kama tu 100% ya Wahubiri wa Kiroho ambao ni ' Matapeli ' watupu wanatutaka tuwaamini na Kuwaabudu wao huku tukiwapelekea Chumvi, Udongo, Mende, Mijusi na Panya waliopo katika Makazi yetu tukawape Sifa na Umaarufu kwanini tu nisirejee katika ' Mizimu ' yetu ambayo nadhani ina Msaada mkubwa Kwangu?

Kuna Mtafiti Mmoja wa Mambo ya Kale na Mila amewahi kuniambia GENTAMYCINE kuwa laiti Waafrika wote tungeendelea Kuiamini ile ' Mizimu ' yetu leo hii Bara la Afrika lingekuwa mbali Kimaendeleo, Magonjwa yangedhibitiwa, Maadili yangeimarika, Vita visingekuwepo, Amani ingetawala na Watu wangekuwa na Upendo wa Kidhati kabisa na siyo kama huu wa Kinafiki ulioko sasa.

Bora tu sasa GENTAMYCINE niiamini ' Mizimu ' yangu mizuri na mema ya Kizanaki, Kisimbiti, Kimakuwa na Kitutsi kuliko Kuwaanini ' Matapeli ' wa Kawe, Mwenge, Ubungo, SalaSala, Kimara Temboni na Mikocheni ambao wanachokifanya hakina tofauti sana na Waganga wa Kienyeji na tena huenda hata wakawa wanawazidi vile vile.

Kulitaja Jina la Mungu Baba na Mwana Mkombozi Yesu Kristo kila Mara ' Madhabahuni ' wakati Matendo yako kwa 100% ni ya ' Kishirikina ' tupu ni Kujiandalia Kuni zako za Kuchomewa Mbinguni huku ' Ukiwaponza ' na wale Wote unaowahadaa ( unaowadanganya ) Kutwa.

Wenye 'Akili' turudini Kuiamini Mizimu.
 
Hakuna ambaye kila ' akihubiri ' anakusisitiza Ushike neno na uamini katika Mungu Baba bali wanatulazimisha tuwaamini wao tena 100% utadhani ndiyo Wameniumba GENTAMYCINE wakati kumbe aliyeniumba ni Mungu wa Ibrahim, Isaka na Yakobo.
Mkuu wewe utakuwa umechoka na kukata tamaa kwa kuwa pengine yale uloyaomba imechukua muda kupata majibu, yapo makanisa kibao tu hapa town na nchi nzima yanaomuabudu Mungu Katika roho na kweli, unasikiliza watu baada ya kumsikiliza Mungu embu utafute ule wimbo wa Christopher Muhangile usikilize tena uenda utakuinua tena imani yako,kumbuka hao panya,mijusi na n. k ni sehemu ya ushuhuda Katika ibada ili wengine wasoamini wapate kuamini.

Siidhani kama baada ya kipengele cha ushuhuda ibada uishia hapo lazima kuna kuwa na neno apo ndipo wewe pa kupazingatia ujue neno linasemaje uishi sawasawa nalo Mungu akufungulie milango yako, kusema waendesha ibada wanaishia kujipamba wao tu wakati hata mtu ashuhudie halafu aseme kwa mfano nakushukuru mtume Mwamposa, Mwamposa lazima haraka atajua huyo mtu bado ajakua kiimani yeye lazima aseme sifa na Utukufu ni Kwa Bwana.

Mwisho tusiwe watu wa kwenda makanisani Sunday to Sunday tujitahidi kuhudhuria vipindi vya Kati Kati ya wiki kwani humo kuna wasaa mzuri mwingi wa kujifunza neno
 
Hakuna ambaye kila ' akihubiri ' anakusisitiza Ushike neno na uamini katika Mungu Baba bali wanatulazimisha tuwaamini wao tena 100% utadhani ndiyo Wameniumba GENTAMYCINE wakati kumbe aliyeniumba ni Mungu wa Ibrahim, Isaka na Yakobo.

Sasa kama tu 100% ya Wahubiri wa Kiroho ambao ni ' Matapeli ' watupu wanatutaka tuwaamini na Kuwaabudu
Hapa Kiranga lazima akuunge mkono
 
Mkuu wewe utakuwa umechoka na kukata tamaa kwa kuwa pengine yale uloyaomba imechukua muda kupata majibu,yapo makanisa kibao tu hapa town na nchi nzima yanaomuabudu Mungu Katika roho na kweli, unasikiliza
Bado 'hujanishawishi' Mkuu jaribu tena.
 
Bado 'hujanishawishi' Mkuu jaribu tena.
Mkuu umenikumbusha kisa cha Yesu alivyowatuma wanafunzi wake kwenda miji mbalimbali kuhubiri injiri, aliwambia miji watayowakataa kun'guteeni miguu tembeeni,sasa kibando chenyewe nimepewa mb 200 naanzaje kwa mfano kukimalizia kwakwo mi nakun'guta miguu natembea 🚶
 
Mkuu umenikumbusha kisa cha Yesu alivyowatuma wanafunzi wake kwenda miji mbalimbali kuhubiri injiri, aliwambia miji watayowakataa kun'guteeni miguu tembeeni,sasa kibando chenyewe nimepewa mb 200 naanzaje kwa mfano kukimalizia kwakwo mi nakun'guta miguu natembea 🚶
'Injiri' ndiyo nini? Mimi ninajua 'Injili' tu.
 
Mkuu umenikumbusha kisa cha Yesu alivyowatuma wanafunzi wake kwenda miji mbalimbali kuhubiri injiri, aliwambia miji watayowakataa kun'guteeni miguu tembeeni,sasa kibando chenyewe nimepewa mb 200 naanzaje kwa mfano kukimalizia kwakwo mi nakun'guta miguu natembea 🚶
😁😁😁
 
Amini Mungu mmoja Muumbaji wa vyote. Yeye Aliyekuwapo, Ambaye yupo na Atakuja kwa Utukufu. Achana na utapeli unaoendelea
 
Kumbe wewe ulikuwa unawaamini wahubiri, huku ukijua ni wahubiri feki....kwa hiyo unajaribu kumshawishi nani akafanye ibada za mizimu, kila mtu apambane na hali yake ya kiroho.
 
Hakuna ambaye kila ' akihubiri ' anakusisitiza Ushike neno na uamini katika Mungu Baba bali wanatulazimisha tuwaamini wao tena 100% utadhani ndiyo Wameniumba GENTAMYCINE wakati kumbe aliyeniumba ni Mungu wa Ibrahim, Isaka na Yakobo.

Sasa kama tu 100% ya Wahubiri wa Kiroho ambao ni ' Matapeli ' watupu wanatutaka tuwaamini na Kuwaabudu wao huku tukiwapelekea Chumvi, Udongo, Mende, Mijusi na Panya waliopo katika Makazi yetu tukawape Sifa na Umaarufu kwanini tu nisirejee katika ' Mizimu ' yetu ambayo nadhani ina Msaada mkubwa Kwangu?

Kuna Mtafiti Mmoja wa Mambo ya Kale na Mila amewahi kuniambia GENTAMYCINE kuwa laiti Waafrika wote tungeendelea Kuiamini ile ' Mizimu ' yetu leo hii Bara la Afrika lingekuwa mbali Kimaendeleo, Magonjwa yangedhibitiwa, Maadili yangeimarika, Vita visingekuwepo, Amani ingetawala na Watu wangekuwa na Upendo wa Kidhati kabisa na siyo kama huu wa Kinafiki ulioko sasa.

Bora tu sasa GENTAMYCINE niiamini ' Mizimu ' yangu mizuri na mema ya Kizanaki, Kisimbiti, Kimakuwa na Kitutsi kuliko Kuwaanini ' Matapeli ' wa Kawe, Mwenge, Ubungo, SalaSala, Kimara Temboni na Mikocheni ambao wanachokifanya hakina tofauti sana na Waganga wa Kienyeji na tena huenda hata wakawa wanawazidi vile vile.

Kulitaja Jina la Mungu Baba na Mwana Mkombozi Yesu Kristo kila Mara ' Madhabahuni ' wakati Matendo yako kwa 100% ni ya ' Kishirikina ' tupu ni Kujiandalia Kuni zako za Kuchomewa Mbinguni huku ' Ukiwaponza ' na wale Wote unaowahadaa ( unaowadanganya ) Kutwa.

Wenye 'Akili' turudini Kuiamini Mizimu.
sijawahi kubali hoja zako ila kwa mada hii nasema sasa umepevuka kiakili. karibu kwenye chama
 
Write your reply...yani kwa haya maombi kidogo tu wanao Fanya hao unao wata matapel ndo unaona duniani tunaendelea kuishi.
 
9 Reactions
Reply
Back
Top Bottom