GENTAMYCINE
JF-Expert Member
- Jul 13, 2013
- 56,054
- 107,538
Hakuna ambaye kila ' akihubiri ' anakusisitiza Ushike neno na uamini katika Mungu Baba bali wanatulazimisha tuwaamini wao tena 100% utadhani ndiyo Wameniumba GENTAMYCINE wakati kumbe aliyeniumba ni Mungu wa Ibrahim, Isaka na Yakobo.
Sasa kama tu 100% ya Wahubiri wa Kiroho ambao ni ' Matapeli ' watupu wanatutaka tuwaamini na Kuwaabudu wao huku tukiwapelekea Chumvi, Udongo, Mende, Mijusi na Panya waliopo katika Makazi yetu tukawape Sifa na Umaarufu kwanini tu nisirejee katika ' Mizimu ' yetu ambayo nadhani ina Msaada mkubwa Kwangu?
Kuna Mtafiti Mmoja wa Mambo ya Kale na Mila amewahi kuniambia GENTAMYCINE kuwa laiti Waafrika wote tungeendelea Kuiamini ile ' Mizimu ' yetu leo hii Bara la Afrika lingekuwa mbali Kimaendeleo, Magonjwa yangedhibitiwa, Maadili yangeimarika, Vita visingekuwepo, Amani ingetawala na Watu wangekuwa na Upendo wa Kidhati kabisa na siyo kama huu wa Kinafiki ulioko sasa.
Bora tu sasa GENTAMYCINE niiamini ' Mizimu ' yangu mizuri na mema ya Kizanaki, Kisimbiti, Kimakuwa na Kitutsi kuliko Kuwaanini ' Matapeli ' wa Kawe, Mwenge, Ubungo, SalaSala, Kimara Temboni na Mikocheni ambao wanachokifanya hakina tofauti sana na Waganga wa Kienyeji na tena huenda hata wakawa wanawazidi vile vile.
Kulitaja Jina la Mungu Baba na Mwana Mkombozi Yesu Kristo kila Mara ' Madhabahuni ' wakati Matendo yako kwa 100% ni ya ' Kishirikina ' tupu ni Kujiandalia Kuni zako za Kuchomewa Mbinguni huku ' Ukiwaponza ' na wale Wote unaowahadaa ( unaowadanganya ) Kutwa.
Wenye 'Akili' turudini Kuiamini Mizimu.
Sasa kama tu 100% ya Wahubiri wa Kiroho ambao ni ' Matapeli ' watupu wanatutaka tuwaamini na Kuwaabudu wao huku tukiwapelekea Chumvi, Udongo, Mende, Mijusi na Panya waliopo katika Makazi yetu tukawape Sifa na Umaarufu kwanini tu nisirejee katika ' Mizimu ' yetu ambayo nadhani ina Msaada mkubwa Kwangu?
Kuna Mtafiti Mmoja wa Mambo ya Kale na Mila amewahi kuniambia GENTAMYCINE kuwa laiti Waafrika wote tungeendelea Kuiamini ile ' Mizimu ' yetu leo hii Bara la Afrika lingekuwa mbali Kimaendeleo, Magonjwa yangedhibitiwa, Maadili yangeimarika, Vita visingekuwepo, Amani ingetawala na Watu wangekuwa na Upendo wa Kidhati kabisa na siyo kama huu wa Kinafiki ulioko sasa.
Bora tu sasa GENTAMYCINE niiamini ' Mizimu ' yangu mizuri na mema ya Kizanaki, Kisimbiti, Kimakuwa na Kitutsi kuliko Kuwaanini ' Matapeli ' wa Kawe, Mwenge, Ubungo, SalaSala, Kimara Temboni na Mikocheni ambao wanachokifanya hakina tofauti sana na Waganga wa Kienyeji na tena huenda hata wakawa wanawazidi vile vile.
Kulitaja Jina la Mungu Baba na Mwana Mkombozi Yesu Kristo kila Mara ' Madhabahuni ' wakati Matendo yako kwa 100% ni ya ' Kishirikina ' tupu ni Kujiandalia Kuni zako za Kuchomewa Mbinguni huku ' Ukiwaponza ' na wale Wote unaowahadaa ( unaowadanganya ) Kutwa.
Wenye 'Akili' turudini Kuiamini Mizimu.