Hii ndiyo Mizigo TISA ambayo JK alijibebesha

Gembe

JF-Expert Member
Sep 25, 2007
2,483
159
wakati Rais Kikwete anaingia madarakani alijibebesha mizigo tisa,Je ni ipi kati ya aliyojibebesha wakati anazindua bunge la Jamhuri ya muungano pale Dodoma ambao ameweza kuufikisha panapotakiwa
Ifuatayo ni mizigo hiyo tisa

Mzigo wa kwanza alioamua kukijitwisha ni ule wa kukiri na kueleza bayana kwamba tatizo la kuwapo kwa rushwa kubwa (grand corruption) ni jambo ambalo atakabiliana nalo kwa nguvu zake zote, akianzia na hatua ya kupitia mikataba yote ambayo serikali inaingia na taasisi za kigeni.

Kwa kukiri kwake kwamba, rushwa kubwa inayohusisha viongozi ni tatizo ambalo halina budi kushughulikiwa kikamilifu, Kikwete alihitimisha hoja ambazo zimekuwa zikitolewa na wananchi na asasi mbalimbali za ndani na nje kuhusu kuwapo kwa rushwa hiyo ambayo serikali ya awamu ya tatu haikuwahi kuiweka bayana na kukubali kuwapo kwake.

Katika hilo, aliwatadharisha viongozi wote katika serikali yake kuwa waaminifu na kutojiingiza katika mtego wa kupokea rushwa kubwa kwa tamaa ya kupata utajiri wa haraka haraka na akahitimisha kwa kusema; "Tusijekulaumiana mbele ya safari".

Mzigo wa pili ambao aliahidi kuubeba kwa kufikia hata hatua ya kuitisha mdahalo au mjadala wa kitaifa ulikuwa ni ule alioupa jina la Mpasuko wa Zanzibar wa kati ya Wapemba na Waunguja, hoja ambayo Mwalimu Nyerere katika ile hotuba yake ya mwaka 1995 aliugusia.

Mzigo wa tatu unaoelekeana na huo alioahidi kuushughulikia pia ni ule wa matatizo yaliyopo katika Muungano wa Tanganyika na Zanzibar uliozaa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ambao alifikia hatua ya kuahidi kuunda wizara itakayokuwa Ofisi ya Makamu wa Rais itakayopitia masuala yote yanayoleta chokochoko na kuzusha malalamiko kutoka pande zote mbili.

Mzigo wa nne ni ule wa mmomonyoko wa maadili ya kitaifa, umoja na mshikamano wetu ambao huo aliamua kurejea katika falsafa zilizobuniwa na Serikali ya Awamu ya Kwanza katika kuupatia ufumbuzi kabla haujawa tatizo kubwa.

Katika hilo, Kikwete alieleza haja ya kurejeshwa tena kwa Shule za Sekondari za Kitaifa moja katika kila wilaya au mkoa ambazo zitakuwa zikichukua wanafunzi kutoka mikoa yote ya Tanzania na pia akarejea umuhimu wa kurejeshwa kwa Jeshi la Kujenga Taifa mambo ambayo kimsingi yalisaidia sana katika kujenga misingi ya umoja na utaifa wa Tanzania.

Kikwete alijitwika mzigo wa sita wa kukabiliana na tatizo la udini ambalo pia limeanza kulinyemelea taifa kama alivyowahi kuonyesha Baba wa Taifa pia. Katika hilo, Rais alilielezea hilo kwa tahadhari kwa kuzitaka shule zinazoanzisha na mashirika ya dini (zisizo za seminari) kujenga utaratibu wa kuwachukua wanafunzi wenye imani tofauti lengo likiwa kutoa fursa sawa ya Watanzania wote kielimu.

Mzigo wa saba aliuzungumzia na kutoa maelekezo ya namna atakavyoukabili ni ule unaohusu miiko ya uongozi na hususan ile inayohusiana na kuzingatia maadili ya utendaji na hususan uaminifu. Katika hilo, Kikwete aliahidi kukabiliana ipasavyo na viongozi wote wenye uchu ya kupata utajiri wa haraka haraka hata kufikia hatua ya kuliibia taifa kwa lengo la kujilimbikizia mali, nia ikiwa ni kupata utajiri wa haraka haraka kwa njia zisizo halali.

mzigo wa nane ni wa kuokoa raslimali maji na uhifadhi wa mazingira kwa kuhakikisha kwamba analifanya hilo kama mkakati mahususi kabisa wa kulinusuru taifa hili kukabiliwa na mgogoro mkubwa wa ukosefu wa maji katika kipindi cha miaka 10 ijayo iwapo hatua za dharura na mahususi hazitachukuliwa.

mzigo wa tisa ambao Kikwete aliuzungumzia ulikuwa ni ule wa kukabiliana na pengo kubwa kati ya matajiri na maskini, jambo ambalo limekuwa likipigiwa sana kelele na watu wengi akiwamo Baba wa Taifa Mwalimu Nyerere. Katika hilo, Kikwete alisema serikali yake haitawapokonya mali matajiri, bali itawajengea maskini uwezo wa kujikwamua kimapato.

Naomba kuwasilisha

Kwa hisani ya Fikra Pevu
 
Mzigo wa kwanza alioamua kukijitwisha ni ule wa kukiri na kueleza bayana kwamba tatizo la kuwapo kwa rushwa kubwa (grand corruption) ni jambo ambalo atakabiliana nalo kwa nguvu zake zote, akianzia na hatua ya kupitia mikataba yote ambayo serikali inaingia na taasisi za kigeni.

Kwa kukiri kwake kwamba, rushwa kubwa inayohusisha viongozi ni tatizo ambalo halina budi kushughulikiwa kikamilifu, Kikwete alihitimisha hoja ambazo zimekuwa zikitolewa na wananchi na asasi mbalimbali za ndani na nje kuhusu kuwapo kwa rushwa hiyo ambayo serikali ya awamu ya tatu haikuwahi kuiweka bayana na kukubali kuwapo kwake.

Suala La Mkataba wa Buzwagi na Richmond?Je Muungwana atawachukulia hatua waliohusika kwababu alisema tusije kulaumiana..?
 
Mzigo wa nne ni ule wa mmomonyoko wa maadili ya kitaifa, umoja na mshikamano wetu ambao huo aliamua kurejea katika falsafa zilizobuniwa na Serikali ya Awamu ya Kwanza katika kuupatia ufumbuzi kabla haujawa tatizo kubwa.

Katika hilo, Kikwete alieleza haja ya kurejeshwa tena kwa Shule za Sekondari za Kitaifa moja katika kila wilaya au mkoa ambazo zitakuwa zikichukua wanafunzi kutoka mikoa yote ya Tanzania na pia akarejea umuhimu wa kurejeshwa kwa Jeshi la Kujenga Taifa mambo ambayo kimsingi yalisaidia sana katika kujenga misingi ya umoja na utaifa wa Tanzania.

Naomba kuwasilisha

Mawasilisho yako yamefika.
Mzigo huu namba nne ndio umebeba kila kitu kilichoahidiwa.
Uzalendo ndio kila kitu, kwa mawazo yangu. Kama wewe ni mzalendo huwezi kupokea rushwa, huwezi kuiba, utaipenda nchi yako nk. Akiweza kufanikisha hili, basi mengi yatawezekana. Umoja wa kitaifa ni muhimu sana. Lakini kama anatuita sisi wakosoaji kuwa ni 'Kelele' ambazo hazimsumbui, tayari ashatugawa kwa msingi wa itikadi. Hakuna kitakachoendelea hapo, kwani hatutajisikia wamoja na wale anaofikiri hawampigii kelele.
 
safi sana, hapa umetupa mawazo ya kufikiria. Hii mizigo alibebeshwa au aliibeba yeye mwenyewe? Maana juzi anasema mzigo wa Kadhi haukuanzia kwake na anataka kuutua kiujanja!
 
safi sana, hapa umetupa mawazo ya kufikiria. Hii mizigo alibebeshwa au aliibeba yeye mwenyewe? Maana juzi anasema mzigo wa Kadhi haukuanzia kwake na anataka kuutua kiujanja!

alijebebesha,Kwasababu alikuwa Over ambitious na alidanganywa na kina Kingunge,alifikiri kila jambo unaweza kulifanya peke yako,na ndio maana alichagua mawaziri wengi ili wagawane hii mizigo yote,ila naona sasa amegundua hata hao mawaziri sitini wameshindwa kuibeba hiyo mizigo,
Naamini anakuja na Maamuzi mazito sana hivi karibuni sababu nchi imemuelemea
 
Ama kweli alijitwisha au alitwishwa mizigo mizito,
bahati mbaya sana karibu miaka miwili sasa hakuna mzigo hata mmoja kati ya hiyo ambao kafanikiwa kuutua au hata kuupunguza.

Aombe msaada, kwani yeye unaelekea kumshinda!
 
""""""""Mzigo wa kwanza alioamua kukijitwisha ni ule wa kukiri na kueleza bayana kwamba tatizo la kuwapo kwa rushwa kubwa (grand corruption) ni jambo ambalo atakabiliana nalo kwa nguvu zake zote, akianzia na hatua ya kupitia mikataba yote ambayo serikali inaingia na taasisi za kigeni""""""""""""


KWA MTAZAMO WANGU NAONA KESHAANZA NA MZIGO WA KWANZA, SASA SINA UHAKIKA KAMA ATAUTUA.NADHANI WOTE TUNAFAHAMU KUWA KATEUWA KAMATI YA KUPITIA MIKATABA YOTE, SASA SIJUI KAMA ITAMSAIDIA KUTUA MZIGO HUU. PILI SINA UHAKIKA KAMA ATAWEZA KUWAWAJIBISHA WAPAMBE WAKE KAMA WATAORODHESHWA NA KAMATI KUWA NI MAFISADI KATIKA MIKATABA WALIYOFANYA
 
safi sana, hapa umetupa mawazo ya kufikiria. Hii mizigo alibebeshwa au aliibeba yeye mwenyewe? Maana juzi anasema mzigo wa Kadhi haukuanzia kwake na anataka kuutua kiujanja!


Mzigo wa mahakama ya kadhi umekuwa mzito..
 
Unfortunately watu wetu hawajui kutathmini utendaji wa Kikwete kulingana na malengo aliyojiwekea; wataangalia pilao, pombe, shilingi elfu mbili, fulana na baseball hats tu.

Ifuatayo ni tathmini yangu kuhus adadi au mizigo hiyo tisa

Mzigo wa kwanza alioamua kukijitwisha ni ule wa kukiri na kueleza bayana kwamba tatizo la kuwapo kwa rushwa kubwa (grand corruption) ni jambo ambalo atakabiliana nalo kwa nguvu zake zote, akianzia na hatua ya kupitia mikataba yote ambayo serikali inaingia na taasisi za kigeni.

Kwa kukiri kwake kwamba, rushwa kubwa inayohusisha viongozi ni tatizo ambalo halina budi kushughulikiwa kikamilifu, Kikwete alihitimisha hoja ambazo zimekuwa zikitolewa na wananchi na asasi mbalimbali za ndani na nje kuhusu kuwapo kwa rushwa hiyo ambayo serikali ya awamu ya tatu haikuwahi kuiweka bayana na kukubali kuwapo kwake.

Katika hilo, aliwatadharisha viongozi wote katika serikali yake kuwa waaminifu na kutojiingiza katika mtego wa kupokea rushwa kubwa kwa tamaa ya kupata utajiri wa haraka haraka na akahitimisha kwa kusema; "Tusijekulaumiana mbele ya safari".
Hapa ni F ndogo au D kubwa kwa sababu ingawa kuna waliojiuzulu kutokana na skendo zile, walifanya hivyo kwa sababu ya shinikizo la bunge wala siyo la Kikwete mwenyewe, ingawa yeye aliridhia. Kuna mafisadi wengine wengi walioiba mali za umma, wanaendelea kupeta. Mikataba aliyoahidi kurudia haikufanyiwa mabadiliko yoyote ya maana kwa vile aliunda tume lakini hakuwa mfuatiliaji wa karibu ili kuyafanya makampuni husika yaone kuwa mzee yuko siriasi. Badala yake makapuni yalipiga chenga na hadi leo mikataba ile haikufanyiwa marekebisho yoyote ya maana.

Mzigo wa pili ambao aliahidi kuubeba kwa kufikia hata hatua ya kuitisha mdahalo au mjadala wa kitaifa ulikuwa ni ule alioupa jina la Mpasuko wa Zanzibar wa kati ya Wapemba na Waunguja, hoja ambayo Mwalimu Nyerere katika ile hotuba yake ya mwaka 1995 aliugusia.
Hapa ninampa kati ya B ndogo na C kubwa kwa sababu mpasuko huo umepungua. Ila nashindwa kumpa credit yoyote Kikwete kwa hili kwa sababu sina uhakika kama kweli alisaidia kuondoa mpasuko huo. Ninadhani yalikuwa ni makubalianoa bain ya Hamadi na Karume tu.

Mzigo wa tatu
unaoelekeana na huo alioahidi kuushughulikia pia ni ule wa matatizo yaliyopo katika Muungano wa Tanganyika na Zanzibar uliozaa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ambao alifikia hatua ya kuahidi kuunda wizara itakayokuwa Ofisi ya Makamu wa Rais itakayopitia masuala yote yanayoleta chokochoko na kuzusha malalamiko kutoka pande zote mbili.

Hapa pia ninampa F kubwa sana kwa sababu mbili: kwanza alikuwa anamuogopa sana Karume kiasi kuwa Karume akawa anaweza kuamua kutohudhuria hata vikao vya muhimu kwa makusudi. Alimwacha Karume akawa anajisemea lolote analotaka la kuudhoofisha Muungano. Pili kitendo cha kumwondoa Shein akagombee Zanzibar badala ya kuendelea kama Makamu wa Rais ambaye angeweza kurithi kiti cha Rais mwaka 2015 hakikuwa na nia ya kuimarisha muungano kabisa.
Mzigo wa nne ni ule wa mmomonyoko wa maadili ya kitaifa, umoja na mshikamano wetu ambao huo aliamua kurejea katika falsafa zilizobuniwa na Serikali ya Awamu ya Kwanza katika kuupatia ufumbuzi kabla haujawa tatizo kubwa.

Katika hilo, Kikwete alieleza haja ya kurejeshwa tena kwa Shule za Sekondari za Kitaifa moja katika kila wilaya au mkoa ambazo zitakuwa zikichukua wanafunzi kutoka mikoa yote ya Tanzania na pia akarejea umuhimu wa kurejeshwa kwa Jeshi la Kujenga Taifa mambo ambayo kimsingi yalisaidia sana katika kujenga misingi ya umoja na utaifa wa Tanzania.
hapa nitampa "F" kubwa sana kwa sababu alianzisha shule za kata ambazo ndizo zilizowatenga zaidi watoto kulingana na uwezo wa kata yenyewe, Shule zilizokuwa katika kata za mjini zilifanikiwa wakati zile za kata za vijijini zikawa hoi zaidi.
Kikwete alijitwika mzigo wa sita wa kukabiliana na tatizo la udini ambalo pia limeanza kulinyemelea taifa kama alivyowahi kuonyesha Baba wa Taifa pia. Katika hilo, Rais alilielezea hilo kwa tahadhari kwa kuzitaka shule zinazoanzisha na mashirika ya dini (zisizo za seminari) kujenga utaratibu wa kuwachukua wanafunzi wenye imani tofauti lengo likiwa kutoa fursa sawa ya Watanzania wote kielimu.
Sijui amefanya nini kuhusu ahadi hiyo kwa sababu migogoro ya kidini imeendelea kuwapo, na kuna shule nyingi za kiislamu zinajiendesha kama vile watoto wote ni waislamu tu kwa kuwataka wavae kiislamu hata kama siyo waislamu, na wala sijasikia Kikwete akizungumzia lolote kuhusu hilo. Hata hivyo ninadhani kuwa pamoja na kuwapo kwa migogoro ya kidini, Kikwete mwenyewe hakuwa shabiki sana wa mambo ya udini ingawa watule wake wengi ni wa dini moja, kwa hiyo nitampa "C" hasa kwa kugomea mambo yoyote yaliyokuwa ya kidini zaidi kuliko ya kitaifa.

Mzigo wa saba aliuzungumzia na kutoa maelekezo ya namna atakavyoukabili ni ule unaohusu miiko ya uongozi na hususan ile inayohusiana na kuzingatia maadili ya utendaji na hususan uaminifu. Katika hilo, Kikwete aliahidi kukabiliana ipasavyo na viongozi wote wenye uchu ya kupata utajiri wa haraka haraka hata kufikia hatua ya kuliibia taifa kwa lengo la kujilimbikizia mali, nia ikiwa ni kupata utajiri wa haraka haraka kwa njia zisizo halali.
Alijitahidi kwa kuwaondoa wafanya biashara mbalimbali kutoka kwenye madaraka ya juu. Hata hivyo aliendelea kuwalea katika nafasi nyingine ambazo wameendelea kujilimbikiza mali kwa kutumia nafasi hizo. Kwa hapa nampa "D"

mzigo wa nane ni wa kuokoa raslimali maji na uhifadhi wa mazingira kwa kuhakikisha kwamba analifanya hilo kama mkakati mahususi kabisa wa kulinusuru taifa hili kukabiliwa na mgogoro mkubwa wa ukosefu wa maji katika kipindi cha miaka 10 ijayo iwapo hatua za dharura na mahususi hazitachukuliwa.
Sikuwahi kumsikia akiliongelea jambo hili tena. Makampuni yote ya uchimbaji wa madini yamevuruga sana mazingira na wala hatujasikia tamko la rais kuhusu swala hilo. Huko Tarime watu wanapata magonjwa ya ajabu kutokana na uharibifu wa mazingira lakini raisi huyo aliruhusu wananchi hao wauawe na wenye machimbo hayo kwa kusaidiwa na polisi wetu. Hapa ninampa gredi ya F ya chini kabisa.

mzigo wa tisa ambao Kikwete aliuzungumzia ulikuwa ni ule wa kukabiliana na pengo kubwa kati ya matajiri na maskini, jambo ambalo limekuwa likipigiwa sana kelele na watu wengi akiwamo Baba wa Taifa Mwalimu Nyerere. Katika hilo, Kikwete alisema serikali yake haitawapokonya mali matajiri, bali itawajengea maskini uwezo wa kujikwamua kimapato.
Kwa kugoma kuongeza kima cha chini na kuruhusu mishahara ya wabunge ipande zaidi, alifeli hapa kwa gredi ya "F"


TOTAL GPA 0.33
 
mizigo hiyo badala ya kupungua uzito mingi yake imezidi kuongezeka..........

mzigo wa maisha bora kwa kila mtanzania sijui nao umeyayukia wapi
 
wakati Rais Kikwete anaingia madarakani alijibebesha mizigo tisa,Je ni ipi kati ya aliyojibebesha wakati anazindua bunge la Jamhuri ya muungano pale Dodoma ambao ameweza kuufikisha panapotakiwa
Ifuatayo ni mizigo hiyo tisa

Mzigo wa kwanza alioamua kukijitwisha ni ule wa kukiri na kueleza bayana kwamba tatizo la kuwapo kwa rushwa kubwa (grand corruption) ni jambo ambalo atakabiliana nalo kwa nguvu zake zote, akianzia na hatua ya kupitia mikataba yote ambayo serikali inaingia na taasisi za kigeni.

Kwa kukiri kwake kwamba, rushwa kubwa inayohusisha viongozi ni tatizo ambalo halina budi kushughulikiwa kikamilifu, Kikwete alihitimisha hoja ambazo zimekuwa zikitolewa na wananchi na asasi mbalimbali za ndani na nje kuhusu kuwapo kwa rushwa hiyo ambayo serikali ya awamu ya tatu haikuwahi kuiweka bayana na kukubali kuwapo kwake.

Katika hilo, aliwatadharisha viongozi wote katika serikali yake kuwa waaminifu na kutojiingiza katika mtego wa kupokea rushwa kubwa kwa tamaa ya kupata utajiri wa haraka haraka na akahitimisha kwa kusema; "Tusijekulaumiana mbele ya safari".

Mzigo wa pili ambao aliahidi kuubeba kwa kufikia hata hatua ya kuitisha mdahalo au mjadala wa kitaifa ulikuwa ni ule alioupa jina la Mpasuko wa Zanzibar wa kati ya Wapemba na Waunguja, hoja ambayo Mwalimu Nyerere katika ile hotuba yake ya mwaka 1995 aliugusia.

Mzigo wa tatu unaoelekeana na huo alioahidi kuushughulikia pia ni ule wa matatizo yaliyopo katika Muungano wa Tanganyika na Zanzibar uliozaa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ambao alifikia hatua ya kuahidi kuunda wizara itakayokuwa Ofisi ya Makamu wa Rais itakayopitia masuala yote yanayoleta chokochoko na kuzusha malalamiko kutoka pande zote mbili.

Mzigo wa nne ni ule wa mmomonyoko wa maadili ya kitaifa, umoja na mshikamano wetu ambao huo aliamua kurejea katika falsafa zilizobuniwa na Serikali ya Awamu ya Kwanza katika kuupatia ufumbuzi kabla haujawa tatizo kubwa.

Katika hilo, Kikwete alieleza haja ya kurejeshwa tena kwa Shule za Sekondari za Kitaifa moja katika kila wilaya au mkoa ambazo zitakuwa zikichukua wanafunzi kutoka mikoa yote ya Tanzania na pia akarejea umuhimu wa kurejeshwa kwa Jeshi la Kujenga Taifa mambo ambayo kimsingi yalisaidia sana katika kujenga misingi ya umoja na utaifa wa Tanzania.

Kikwete alijitwika mzigo wa sita wa kukabiliana na tatizo la udini ambalo pia limeanza kulinyemelea taifa kama alivyowahi kuonyesha Baba wa Taifa pia. Katika hilo, Rais alilielezea hilo kwa tahadhari kwa kuzitaka shule zinazoanzisha na mashirika ya dini (zisizo za seminari) kujenga utaratibu wa kuwachukua wanafunzi wenye imani tofauti lengo likiwa kutoa fursa sawa ya Watanzania wote kielimu.

Mzigo wa saba aliuzungumzia na kutoa maelekezo ya namna atakavyoukabili ni ule unaohusu miiko ya uongozi na hususan ile inayohusiana na kuzingatia maadili ya utendaji na hususan uaminifu. Katika hilo, Kikwete aliahidi kukabiliana ipasavyo na viongozi wote wenye uchu ya kupata utajiri wa haraka haraka hata kufikia hatua ya kuliibia taifa kwa lengo la kujilimbikizia mali, nia ikiwa ni kupata utajiri wa haraka haraka kwa njia zisizo halali.

mzigo wa nane ni wa kuokoa raslimali maji na uhifadhi wa mazingira kwa kuhakikisha kwamba analifanya hilo kama mkakati mahususi kabisa wa kulinusuru taifa hili kukabiliwa na mgogoro mkubwa wa ukosefu wa maji katika kipindi cha miaka 10 ijayo iwapo hatua za dharura na mahususi hazitachukuliwa.

mzigo wa tisa ambao Kikwete aliuzungumzia ulikuwa ni ule wa kukabiliana na pengo kubwa kati ya matajiri na maskini, jambo ambalo limekuwa likipigiwa sana kelele na watu wengi akiwamo Baba wa Taifa Mwalimu Nyerere. Katika hilo, Kikwete alisema serikali yake haitawapokonya mali matajiri, bali itawajengea maskini uwezo wa kujikwamua kimapato.

Naomba kuwasilisha

Kwa hisani ya Fikra Pevu

Wa Kumi LOWASSA
 
Hahahaa kichuguu kwa GPA 0.33 ni kuwa JK amedisco na haqualify kuwa presidaa tena, kajifanya ni mnyamwezi kubeba mizigo mizito wakati yeye ni mkwere, hana lolote zaidi ya kukaa kijiweni akinywa kahawa na kupiga soga.
 
Nasubiri Ilani ya uchaguzi kwa mwaka 2010-2015.

Na ripoti ya utekelezaji wa ser za chama kwa kipindi cha miaka mitano 2005-2010.

Is President Mkapa around in Tanzania?
 
Back
Top Bottom