sky soldier
JF-Expert Member
- Mar 30, 2020
- 5,408
- 19,032
Ni jamii ambayo ilikuwa haijulikani lakini hivi karibuni kutoitambua ni sawa na kusema hakuna kitu kwenye chumba mlichomo na tembo, hata kwa wanaofunga mizigo yao soko kubwa kuliko yote nchini pale kariakoo ni mashuhuda, hawa watu ni kama wameimeza kariakoo, kuimeza kariakoo ni sawa na kuwa mfanyabiashara mkuu wa bidhaa zinazouzwa madukani nchi nzima.
Sio mbinu ya wakinga, wao walichofanya ni kuiga tu, mbinu hii hutumika sanasana na wasomali hasa nchini kenya.
Mbinu ni nyepesi mno na ninahofia endapo kabila kubwa likiiga basi litakuwa mbali sana kimafanikio, mbali sanaaaa!!
Kinachofanyika ni swala la kuwa na umoja unaowaunganisha wakinga waliofanikiwa Dar kuinua wenzao wenye biashara ndogo mikoani waende kufanya biashara kubwa dar.
Kunakuwa na umoja kwa mfano wanakuwa wakinga 500, kinachofanyika ni kwamba kila mwezi kila mtu awe mfanyabashara au kaajiriwa inabidi atoe elf 50, laki, laki 2, n.k kutokana na status yake, hata ukitoa M ni wewe tu.
Hapo kila mwezi huwa inapatikana takribani milioni 50
sasa kitachofanyika hapo, wanamchagua mkinga ambae ana fanya vizuri kwenye biashara yake ndogo huko mikoani walikojazana kama Mbeya, Songwe, Iringa, n.k..wanamchangia mtaji ahamie Dar, ile biashara ndogo huwa tayari wana watu wanaosaidiana ndio ambao wataendeleza yeye akienda kariakoo.
wale waliomchangia tayari huwa wana frem zao kibao pale kariakoo, watampa frem mwanachama mpya na kumshughulikia mambo ya vibali..
Mwanachama mpya ataamua afanye biashara ipi, akishaamua ataletewa mzigo na wakinga wenzake ambao wamejazana kama utitiri kwenye jiji la Guangzhou huko nchini China, hili jiji lina viwanda vya kutengeneza bidhaa, machimbo ya kununua bidhaa, bandari ya kusafirishia, n.k. wakinga ni wamejazana sana huko (kwa waliofika ni mashuhuda), hao ndio huwa wanasaidia kutafuta na kusafirisha bidhaa kwa wenzao, wana kampuni yao kubwa tu ya kusafirisha mizigo inaitwa mapembelo cargo, hilo neno mapembelo ni salamu ya kikinga, ukisalimiwa mapembelo unajibu vavene 😂
Mzigo ukifika bandarini tayari wama connections za kuutoa chap chap unaingia fasta dukani, huko dukani silaha yao kuu ni kuuza kwa bei ndogo kuliko wengine, kufanya hivyo inabidi wauze kwa faida ndogo, kitu ambacho kinauzwa kwa faida ya elf 30 wao wapo radhi wauze kwa faida ya elf 5, hii ndio tabia iliyowafanya hata wachaga na wapemba wanaouza bidhaa zilezile kama wanazouza wakinga wapakimbie hapo kariakoo.
Sasa ukijumlisha kuuza kwa faida ndogo, kulipa marejesho, kuwa wanachama wapya wanaotakiwa kuchangia mchango wa kuinuana, n.k hapa inabidi wajibane haswaa kwenye matumizi, hapa ndio utakuta ni kawaida yao kubeba chakula walichipikia nyumbani kwenye mahotpot.
Zamani wakinga waliokuwa wanaletwa kariakoo walikuwa wamekulia kijijini kwa muda mrefu sana na umri umenda kidogo ni ngumu kibadilika, ilikuwa ni kawaida sana kukuta mkinga kashazoea kuvaa ndala zake na koti lake, yani kama yupo kijijini na ndio kashazoea, kwa siku hizi zama zimebadilika, hata ukienda kariakoo utawakuta vijana watanashati tu ambao wanaendana na mda.
Kuhusu uchawi kiukweli hili jambo nimelisikia mda mrefu ila nakwambia biashara ni kuwa na bidhaa au huduma sahihi, jua soko linataka nini lete kile soko linataka, ukiuza kwa bei rafiki watu tutakutafuta tu popote
sasa sipati picha kabila kama wasukuma, wachaga, wanyakyusa, wahaya, hawa wenye idadi ya watu milioni 2 na zaidi, kabila moja wapo wajikusanye wawe na umoja wa watu hata elf 10 tu wawe wanachangiana hata elf 50 kila mwezi,
watu elf 10 x shilingi 50,000 = milioni 500 pesa taslimu
ni kiasi kikubwa sana hicho kinaweza kisiishie kuinuana kwa mitaji bali hata kielimu na kuendeleza makwao.
Tatizo kuu wengi hawataki waendelee ili wao wawe juu kuliko wenzao, hiki ndicho kinawapa raha.
Sio mbinu ya wakinga, wao walichofanya ni kuiga tu, mbinu hii hutumika sanasana na wasomali hasa nchini kenya.
Mbinu ni nyepesi mno na ninahofia endapo kabila kubwa likiiga basi litakuwa mbali sana kimafanikio, mbali sanaaaa!!
Kinachofanyika ni swala la kuwa na umoja unaowaunganisha wakinga waliofanikiwa Dar kuinua wenzao wenye biashara ndogo mikoani waende kufanya biashara kubwa dar.
Kunakuwa na umoja kwa mfano wanakuwa wakinga 500, kinachofanyika ni kwamba kila mwezi kila mtu awe mfanyabashara au kaajiriwa inabidi atoe elf 50, laki, laki 2, n.k kutokana na status yake, hata ukitoa M ni wewe tu.
Hapo kila mwezi huwa inapatikana takribani milioni 50
sasa kitachofanyika hapo, wanamchagua mkinga ambae ana fanya vizuri kwenye biashara yake ndogo huko mikoani walikojazana kama Mbeya, Songwe, Iringa, n.k..wanamchangia mtaji ahamie Dar, ile biashara ndogo huwa tayari wana watu wanaosaidiana ndio ambao wataendeleza yeye akienda kariakoo.
wale waliomchangia tayari huwa wana frem zao kibao pale kariakoo, watampa frem mwanachama mpya na kumshughulikia mambo ya vibali..
Mwanachama mpya ataamua afanye biashara ipi, akishaamua ataletewa mzigo na wakinga wenzake ambao wamejazana kama utitiri kwenye jiji la Guangzhou huko nchini China, hili jiji lina viwanda vya kutengeneza bidhaa, machimbo ya kununua bidhaa, bandari ya kusafirishia, n.k. wakinga ni wamejazana sana huko (kwa waliofika ni mashuhuda), hao ndio huwa wanasaidia kutafuta na kusafirisha bidhaa kwa wenzao, wana kampuni yao kubwa tu ya kusafirisha mizigo inaitwa mapembelo cargo, hilo neno mapembelo ni salamu ya kikinga, ukisalimiwa mapembelo unajibu vavene 😂
Mzigo ukifika bandarini tayari wama connections za kuutoa chap chap unaingia fasta dukani, huko dukani silaha yao kuu ni kuuza kwa bei ndogo kuliko wengine, kufanya hivyo inabidi wauze kwa faida ndogo, kitu ambacho kinauzwa kwa faida ya elf 30 wao wapo radhi wauze kwa faida ya elf 5, hii ndio tabia iliyowafanya hata wachaga na wapemba wanaouza bidhaa zilezile kama wanazouza wakinga wapakimbie hapo kariakoo.
Sasa ukijumlisha kuuza kwa faida ndogo, kulipa marejesho, kuwa wanachama wapya wanaotakiwa kuchangia mchango wa kuinuana, n.k hapa inabidi wajibane haswaa kwenye matumizi, hapa ndio utakuta ni kawaida yao kubeba chakula walichipikia nyumbani kwenye mahotpot.
Zamani wakinga waliokuwa wanaletwa kariakoo walikuwa wamekulia kijijini kwa muda mrefu sana na umri umenda kidogo ni ngumu kibadilika, ilikuwa ni kawaida sana kukuta mkinga kashazoea kuvaa ndala zake na koti lake, yani kama yupo kijijini na ndio kashazoea, kwa siku hizi zama zimebadilika, hata ukienda kariakoo utawakuta vijana watanashati tu ambao wanaendana na mda.
Kuhusu uchawi kiukweli hili jambo nimelisikia mda mrefu ila nakwambia biashara ni kuwa na bidhaa au huduma sahihi, jua soko linataka nini lete kile soko linataka, ukiuza kwa bei rafiki watu tutakutafuta tu popote
sasa sipati picha kabila kama wasukuma, wachaga, wanyakyusa, wahaya, hawa wenye idadi ya watu milioni 2 na zaidi, kabila moja wapo wajikusanye wawe na umoja wa watu hata elf 10 tu wawe wanachangiana hata elf 50 kila mwezi,
watu elf 10 x shilingi 50,000 = milioni 500 pesa taslimu
ni kiasi kikubwa sana hicho kinaweza kisiishie kuinuana kwa mitaji bali hata kielimu na kuendeleza makwao.
Tatizo kuu wengi hawataki waendelee ili wao wawe juu kuliko wenzao, hiki ndicho kinawapa raha.