Hii ndiyo kampuni ya Arab Contractors itakayojenga bwawa la Stiegler's Gorge

Kanungila Karim

JF-Expert Member
Apr 29, 2016
20,744
25,445

Disemba 12 2018 Serikali ya Tanzania chini ya utawala wa Dkt John Pombe Magufuli na kampuni ya Arab Contractors ya nchini Misri zilitilia saini mkataba wa ujenzi wa mradi wa kuzalisha umeme lkatika mto Rujifi (Stiegler's Gorge) utakaotekelezwa kwa muda wa miezi 42 kuanzia sasa.

Katika halfa hiyo ya kutia saini iliyohudhuriwa na Rais wa Tanzania Mhe.John Pombe Magufuli na Waziri Mkuu wa Misri Dkt. Mustafa Madbouly,kwa upande wa Tanzania aliyetia aini ni Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la umeme Tanzania(TANESCO) Dkt. Tito Mwinuka huku upande wa Misri ukiwakilishwa na Mwenyekkiti wa kampuni ya Arabs Contractors Bwana Mohamed Mohsen Salaheldin na Mtendaji Mkuu wa kampuni ya Elsewedy Bwana Ahmed Sadek Elsewedy.

Kampuni ya Arab Contractors iliyoshinda zabuni ya ujenzi wa mradi huo mkubwa utakaozalisha megawati 2,115 utakapokamilika ni kampuni ya ujenzi kutoka Misri iliyoanzishwa mwaka 1955 yenye makao yake makuu jijini Cairo.

Mwanzilishi wa kampuni hiyo ni Bwana Osman Ahmed Osman ambaye aloikuwa ni mjasiriamali na mwanasiasa nchini humo na pia aliwahi kuwa Waziri wa Makzi wa Misri chini ya utawala wa Rais kipenzi cha watu Anwar Saadat aliyeongoza kuanza 1971 hadi 1980.

Osman Ahmed Osman alifahamika zaidi kama El-mo;alim alifariki Mei Mosi 1999 jijini Cairo.

Kampuni hiyo ilitaifishwa na kuwa mali ya serikali baada ya kutokea mapinduzi nchini humo.

Kampuni hiyo pia ilishiriki katika ujenzi wa bwawa kubwa la kufua umeme nchini humo la Aswan ambalo lilionekana na njia ya kuleta mapinduzi ya Viwanda nchini humo kutokana na uwezo wake mkubwa wa kuzalisha umeme.

Ujenzi wa bwaa la Awan ulianza mwaka 1960 na kufungulia rasmi mwaka 1970 yaani miaka 10 baadae.Bwawa hilo lina urefu wa kina cha futi 364 urefu wa kilometa 3.83 na upana wa mita 980.


Kampuni hiyo pia imehusika na ujenzi wa majengo mbalimbali ya nchini humo na nje ya nchi.Hadi sasa kampuni hiyo ya Arab Contractors ina miradi katika nchi 29 duniani kote.

Mbali na ujenzi kampuni hiyo inamiliki klabu ya mpira wa miguu ya El Mokawloon SC inayoshiriki ligi kuu ya nchini Misri.

Katika michuano ya klabu bingwa ya Afrika mwaka 1996 klabu hiyo inayomilikiwa na kampuni hii ilikutana na Simba SC ya Tanzania katika mzunguko wa pili ambapo katika mchezo wa kwanza klabu ya El Mokawloon SC ilikubali kipigo cha 3-1 kutoka kwa Simba SC.Na katika marudiano klabu ya Simba SC ilifungwa 2-0 na hivyo klabu ya El Mokawloon iliingia robo fainali kwa faida ya goli la ugenini.

Katika fainali hizo klabu ya El Mokawloon ilifanikiwa kutinga fainali kwa kuifunga klabu ya Sodigraf ya Jamhuri Ya Kidemokrasia Ya Kongo(DRC) kwa magoli 4-0 na kufanikiwa kutwaa taji la Klabu Bingwa Afrika.

Hapo chini ni baadhi ya miradi iliyowahi kutekelezwa na kampuni hiyo



Bibliotheca Alexandrina


Uwanja wa mpira wa Borg El Arab


Bwawa la Aswan



Cairo Regional Ring Road


Uwanja wa ndee wa kimataifa wa Luxor
 
Naishauri serikali wakati Wamisri wanajenga bwawa hilo waitumie fursa hiyo kuzungumza nao watuletee ujuzi wa kilimo cha irrigation. Wamisri ni mabingwa wa irrigation duniani.
Kwa upande wa irrigation wapo vizuri Sana tatizo ni kuwa Serikali yetu haijaweka kipaumbele kwenye kilimo.

Kujenga irrigation system scheme ni gharama kubwa Sana sioni Serikali yetu kuwa inaweza kutoa nafasi ya Kwanza ktk kilimo.

Nimewahi kushiriki utafiti mwaka 2014 kilimo Cha umwagiliaji tunahitaji Trillion shs 35 kujenga scheme katika Kila kata zote Tanzania bara hii ni zaidi ya bajeti na kwa Sasa kata zimeongezeka gharama pia zimeongezeka Bei za vifaa zipo juu.

Serikali itaweza kutoa nafasi ya Kwanza ktk kilimo?
 
Kwa upande wa irrigation wapo vizuri Sana tatizo ni kuwa Serikali yetu haijaweka kipaumbele kwenye kilimo.

Kujenga irrigation system scheme ni gharama kubwa Sana sioni Serikali yetu kuwa inaweza kutoa nafasi ya Kwanza ktk kilimo.

Nimewahi kushiriki utafiti mwaka 2014 kilimo Cha umwagiliaji tunahitaji Trillion shs 35 kujenga scheme katika Kila kata zote Tanzania bara hii ni zaidi ya bajeti na kwa Sasa kata zimeongezeka gharama pia zimeongezeka Bei za vifaa zipo juu.

Serikali itaweza kutoa nafasi ya Kwanza ktk kilimo?
Tusianze juu huko.

Tuongee nao watuletee wale falahin (peasants) wa kandokando ya mto Nile waje kutupa ujuzi.
 
Tusianze juu huko.

Tuongee nao watuletee wale falahin (peasants) wa kandokando ya mto Nile waje kutupa ujuzi.
Marehem Mzee Samwel Sitta alipeleka vijana wengi Egypt na Ethiopia kujiifunza kilimo Cha umwagiliaji na miradi mingi iliibuliwa kule ulambo kwenye Jimbo la Sitta nilifanikiwa kupata tenda ya kujenga scheme za umwagiliaji 2
Moja iliishia phase 1
Nyingine phase2

Kwasababu ya pesa kutolewa kidogo kidogo miradi hii ilikuwa ikamilike kwa phase 4 na Sasa imetelekezwa miradi mingi ya umwagiliaji iliyoibuliwa kipindi Cha J.K inakufa hakuna wa kuiendeleza.
 
Marehem Mzee Samwel Sitta alipeleka vijana wengi Egypt na Ethiopia kujiifunza kilimo Cha umwagiliaji na miradi mingi iliibuliwa kule ulambo kwenye Jimbo la Sitta nilifanikiwa kupata tenda ya kujenga scheme za umwagiliaji 2
Moja iliishia phase 1
Nyingine phase2

Kwasababu ya pesa kutolewa kidogo kidogo miradi hii ilikuwa ikamilike kwa phase 4 na Sasa imetelekezwa miradi mingi ya umwagiliaji iliyoibuliwa kipindi Cha J.K inakufa hakuna wa kuiendeleza.
Wizi mtupu.

Hatuhitaji miradi ya umwagiliaji tunahitaji peasants wenye uzoefu waje kuwafundisha peasants wenzao individually.
 
Tusianze juu huko.

Tuongee nao watuletee wale falahin (peasants) wa kandokando ya mto Nile waje kutupa ujuzi.
Hata hao vijana waliopelekwa Egypt na Ethiopia kujiifunza walichorudi nacho hakijatusaidia ñadhani hatujaamua kujikomboa kiuchumi kutoka ktk sekta ya kilimo ambayo imegusa % kubwa ya watanzania na ilituondokane na umaskini lazima kilimo kipate nafasi ya pili ktk vipaumbele vya wizara za Serikali
 
Wizi mtupu.

Hatuhitaji miradi ya umwagiliaji tunahitaji peasants wenye uzoefu waje kuwafundisha peasants wenzao individually.
Sio Kila kitu wizi acha kujenga dhana, potofu hao wakulima wa Egypt hawategemei kilimo Cha mvua isiyo na uhakika Kama kwetu
Nenda mikoa ya kusini Mtwara,Lindi uone ukataji wa mistu kwa wakulima wa ufuta unavyoharibu mazingira utaona miaka 10 ijayo tutakuwa taifa la namna gani?

Bila kilimo Cha kisasa Cha umwagiliaji bado hatutafanikiwa ktk kilimo.

Jiulize hao wakulima wa misri wanategemea mvua isiyokuwa na muda maalum?
 
Hata hao vijana waliopelekwa Egypt na Ethiopia kujiifunza walichorudi nacho hakijatusaidia ñadhani hatujaamua kujikomboa kiuchumi kutoka ktk sekta ya kilimo ambayo imegusa % kubwa ya watanzania na ilituondokane na umaskini lazima kilimo kipate nafasi ya pili ktk vipaumbele vya wizara za Serikali
Walipelekwa Kitanzania.
 
Sio Kila kitu wizi acha kujenga dhana, potofu hao wakulima wa Egypt hawategemei kilimo Cha mvua isiyo na uhakika Kama kwetu
Nenda mikoa ya kusini Mtwara,Lindi uone ukataji wa mistu kwa wakulima wa ufuta unavyoharibu mazingira utaona miaka 10 ijayo tutakuwa taifa la namna gani?
Bila kilimo Cha kisasa Cha umwagiliaji bado hatutafanikiwa ktk kilimo.
Jiulize hao wakulima wa misri wanategemea mvua isiyokuwa na muda maalum?
Nisome tena. Naongelea irrigation. Sipo kwenye hizo porojo zako zingine.
 
Kwa upande wa irrigation wapo vizuri Sana tatizo ni kuwa Serikali yetu haijaweka kipaumbele kwenye kilimo.

Kujenga irrigation system scheme ni gharama kubwa Sana sioni Serikali yetu kuwa inaweza kutoa nafasi ya Kwanza ktk kilimo.

Nimewahi kushiriki utafiti mwaka 2014 kilimo Cha umwagiliaji tunahitaji Trillion shs 35 kujenga scheme katika Kila kata zote Tanzania bara hii ni zaidi ya bajeti na kwa Sasa kata zimeongezeka gharama pia zimeongezeka Bei za vifaa zipo juu.

Serikali itaweza kutoa nafasi ya Kwanza ktk kilimo?
Research nyingine kwa kweli duh! Kwa hiyo mlipata gharama ya kata moja mkazidisha kwa kata zote tz mkapata hayo matrilioni? Kwa hiyo na kata ya gerezani mliiweka humo? Kaazi kwelikweli. Tz ya ajabu sana, kumbe ndio maana hata kwenye majiji na manispaa unakuta kuna maafisa Kilimo na maafisa Nyuki. Ishu ni kupata utaalamu wao na kuwekeza kwenye maeneo yanayofaa kwa irrigation scheme kama kilombero, rufiji nk
 
Back
Top Bottom