mawazo mbishi
Member
- Apr 1, 2012
- 20
- 23
Tz ina Madaktari wa upasuaji wa mfumo wa fahamu (neuro surgeons)-3
Madaktari wa moyo ( cardiologists)-5
Madaktari wa figo (nephrologists)-3
Madaktari wa mfumo wa fahamu (neurologists)-2
Nchi nzima ina machine 7 za Hemodialysis za kusafisha figo kwa watu wenye renal failure, na zinazofanya kazi ni 4 na hizo nne zinatumiwa na watu watatu au wanne tu. Nchi yetu inakadiriwa kuwa na wagonjwa zaidi ya laki moja wanaohitaji dialysis...maana yake ukipata tu renal failure maana yake we umeshakufa...
leo hii ukipata renal failure, ambayo wengi wanapata kuafanyiwa dialysis mara moja tu ni sh 200,000 na unahitaji kufanyiwa mara tatu kwa wiki...!!!!
Hospitali zote za mikoa hazina madaktari bingwa na zile ambazo wapo ni mmoja mmoja, nao ni viongozi hawatibu watu.
Hebu niambieni hawa watanzania milioni 40 wanapata wapi hizi huduma, hivi tuna justification viongozi wetu kutembea na VX..!!!!!
Inasikitisha kuona bado tuna mazingira kama haya, na tunatumia mamilioni ya pesa kuwapeleka vigogo wetu wakatibiwe nje ya nchi kwa hela zetu za kodi. Nadhani madaktari waliposema pamoja na mabo mengine wanapinga wagonjwa kupelekwa nje ya nchi walikuwa sahihi hasa ukizingatia wanaopata nafasi kwa kipaumbele ni viongozi wakifuatiwa na ndugu na jamaa zao, na wale wanaoweza kuilainisha machine nadhani hapa naeleweka, ila wewe mlalahoi ukiugua basi ndugu zako waanze tu taraibu za kukuaga....!!!
Naona aibu kwamba tuna miaka 50 tangu uhuru..na tuna rasilimali nyingi kama Taifa...!!!!nimetafakari kwa kina taarifa hizi na nikaona wataalamu wetu walikuwa na hoja ya msingi walipoamua kuingia katika mgomo
Madaktari wa moyo ( cardiologists)-5
Madaktari wa figo (nephrologists)-3
Madaktari wa mfumo wa fahamu (neurologists)-2
Nchi nzima ina machine 7 za Hemodialysis za kusafisha figo kwa watu wenye renal failure, na zinazofanya kazi ni 4 na hizo nne zinatumiwa na watu watatu au wanne tu. Nchi yetu inakadiriwa kuwa na wagonjwa zaidi ya laki moja wanaohitaji dialysis...maana yake ukipata tu renal failure maana yake we umeshakufa...
leo hii ukipata renal failure, ambayo wengi wanapata kuafanyiwa dialysis mara moja tu ni sh 200,000 na unahitaji kufanyiwa mara tatu kwa wiki...!!!!
Hospitali zote za mikoa hazina madaktari bingwa na zile ambazo wapo ni mmoja mmoja, nao ni viongozi hawatibu watu.
Hebu niambieni hawa watanzania milioni 40 wanapata wapi hizi huduma, hivi tuna justification viongozi wetu kutembea na VX..!!!!!
Inasikitisha kuona bado tuna mazingira kama haya, na tunatumia mamilioni ya pesa kuwapeleka vigogo wetu wakatibiwe nje ya nchi kwa hela zetu za kodi. Nadhani madaktari waliposema pamoja na mabo mengine wanapinga wagonjwa kupelekwa nje ya nchi walikuwa sahihi hasa ukizingatia wanaopata nafasi kwa kipaumbele ni viongozi wakifuatiwa na ndugu na jamaa zao, na wale wanaoweza kuilainisha machine nadhani hapa naeleweka, ila wewe mlalahoi ukiugua basi ndugu zako waanze tu taraibu za kukuaga....!!!
Naona aibu kwamba tuna miaka 50 tangu uhuru..na tuna rasilimali nyingi kama Taifa...!!!!nimetafakari kwa kina taarifa hizi na nikaona wataalamu wetu walikuwa na hoja ya msingi walipoamua kuingia katika mgomo