Hii Ndiyo CHADEMA 1992 - 2013

Filipo Lubua

JF-Expert Member
Nov 18, 2011
339
578
Pamoja na changamoto mbalimbali chaa hiki kilizozipitia, bado kimeendelea kuimarika kila uchao uchwao. Kuna wale wanaobeza kuimarika kwa chama hiki, na kukifananisha na vyama vingine vya CUF na NCCR - Mageuzi, wakidhani kuwa kama ilivyokuwa kwa vyama hivyo, Chadema pia kitaporomoka. Ila watu hawa wanashindwa kuelewa kuwa Chama hiki hakijawahi kupoteza umaarufu wake, na zaidi tu kimekuwa kikiuongeza.

Swala hili linathibitishwa na idadi ya viti vya udiwani na Ubunge ambavyo chama hiki kimekuwa kikivipata katika kila uchaguzi mkuu, tangu 1995. Leo tuangalie tu takwimu fupi za udiwani na ubunge kwa Chama hiki.

MwakaMadiwaniWabunge
1995424
2000755
200510311
201046749

Kwa kuzitazama takwimu hizi rahisi, utajifunza kuwa pamoja na hujuma nyingi, wizi wa kura, na fitina mbalimbali kutoka vyama vingine vya siasa (vikiwemo CCM na CUF), pamoja na serikali kutumia vyombo vya dola kujaribu kukiporomosha, bado Chadema kimekuwa kikiendelea kujinyakulia viti vingi zaidi kila kiingiapo katika uchaguzi mkuuna zaidi sana, ongezeko limekuwa likiongezeka kila uchaguzi. Mfano, mwaka 2000 chadema kiliongeza kiti kimoja tu cha ubunge na mwaka 2005 kiliongeza viti sita vya ubunge na mwaka 2010 kiliongeza viti 38 (ukiongeza na vile vya viti maalum). Kwa mantiki hiyo, chadema kimekuwa kikikubalika zaidi kila miaka isogeapo. Wale wenye ndoto kuwa kitakufa, subirini kama hamtakiona kikiingia ikulu na nyie kubaki mnabung'aabung'aa tu.

Kwa wale mpendao grafu, takwimu hizi zinaweza kuonekana kama ifuatavyo. Chadema songeni mbele, hadi mfanikiwe kulikomboa taifa hili. Matumaini ya Watanzania wengi, hasa nguvu ya taifa (vijana), yako mikononi mwenu. Imarisheni umoja, mshikamano, maelewano na mapambano. Hatimaye mtalifikisha taifa letu pale ambapo CCM wameshindwa kwa zaidi ya miaka 50 sasa (nusu karne).

Chadema 1992 - 2013.jpg
 
Utafiti Mzuri! Pamoja na changamoto zote tunazopata, bado kuna tatizo kubwa sana kwa watanzania ni kutokuwa na mwamko wa kupiga kura. Kura ndio maamuzi ya mwisho kama unataka mabadiliko. ACHA kushabikia tu mtaani na mikutanoni, PIGIA KURA CHADEMA!
 
Mwamko wataupata tu manake shida hazidanganyi. Maisha yamekuwa magimu na kila mtu yukoalert kuwa tumeingia chakani. Wenyewe tutaenda kupanga mstari kupiga kura. JK kaza bolt hizohadi tunyooke!
Utafiti Mzuri! Pamoja na changamoto zote tunazopata, bado kuna tatizo kubwa sana kwa watanzania ni kutokuwa na mwamko wa kupiga kura. Kura ndio maamuzi ya mwisho kama unataka mabadiliko. ACHA kushabikia tu mtaani na mikutanoni, PIGIA KURA CHADEMA!
 
Mwamko wataupata tu manake shida hazidanganyi. Maisha yamekuwa magimu na kila mtu yukoalert kuwa tumeingia chakani. Wenyewe tutaenda kupanga mstari kupiga kura. JK kaza bolt hizohadi tunyooke!

You can't be serious King'asti ... hivi kuna kunyooka zaidi ya hapa tulipofikia!?
 
Last edited by a moderator:
Mungu ibariki tanzania mungu ibariki chadema na watu wake peeeeeeeeeeeople power 2015 ccm tunawazika rasmi
sema mungu ibariki tanganyika.. wacha kututia tia na sisis kwenye hizo biashara zako...zanzibar tuko kivyetu.....
 
Msijidanganye cdm hz takwimu mnapaswa kuzitafakari kwa kina kwani ingawa chama kinaungwa mkono na watanzania wengi lkn chama kama chama bd hakija kuwa, nasema hvy kwa nn? Lazima mlinganishe toka mwaka 1992-2013 ki uchumi chama kikowapi kimepiga hatua gani , idadi ya wanachama halali na waaminifu imeongezeka kiasi gani! Uwezo wa kutengeneza fursa za kiuchumi ki chama imefikia wapi? Ofisi za kueleweks kuanzia Taifa mpaka ngazi ya chama zipo?uongozi endelevu kuanzia Taifa mpaka chini upo?. Nasema hvy maana natambuwa kuwa cdm hakijatekeleza hy ambayo ndi yanayoosha kama chama kimekuwa. Kilichopo sasa ni kuwa cdm kina washabiki tuu ambao ni dkk mojo tuu wanaweza kugeuka na kikiacha chama kama kikombe kilichomaliza kunywewa maji yaani tupu. Jiimalisheni ktk hayo vinginevyo ni sawa na kundi kama la waigizaji tuu ktk democrasia na Siasa hapa Tanzania.
 
Msijidanganye cdm hz takwimu mnapaswa kuzitafakari kwa kina kwani ingawa chama kinaungwa mkono na watanzania wengi lkn chama kama chama bd hakija kuwa, nasema hvy kwa nn? Lazima mlinganishe toka mwaka 1992-2013 ki uchumi chama kikowapi kimepiga hatua gani , idadi ya wanachama halali na waaminifu imeongezeka kiasi gani! Uwezo wa kutengeneza fursa za kiuchumi ki chama imefikia wapi? Ofisi za kueleweks kuanzia Taifa mpaka ngazi ya chama zipo?uongozi endelevu kuanzia Taifa mpaka chini upo?. Nasema hvy maana natambuwa kuwa cdm hakijatekeleza hy ambayo ndi yanayoosha kama chama kimekuwa. Kilichopo sasa ni kuwa cdm kina washabiki tuu ambao ni dkk mojo tuu wanaweza kugeuka na kikiacha chama kama kikombe kilichomaliza kunywewa maji yaani tupu. Jiimalisheni ktk hayo vinginevyo ni sawa na kundi kama la waigizaji tuu ktk democrasia na Siasa hapa Tanzania.

Jinga jingine hili lisilo jitambua.
 
Bado. Yaani hadi 2015 titaweka akili sawa. Bado tupo wengi ambao hatujawahi kulala na njaa. Huko tuendako yatafika tu. Sasa hivi tunasisitiza uzungu na kugomea extended family, tukilalia chai na mkate na kisha kukosa mkate tutaelewa. Bado baba, tuliza boli. Na unajua dola imeanza kuimarika upyaaa!?
You can't be serious King'asti ... hivi kuna kunyooka zaidi ya hapa tulipofikia!?
 
Last edited by a moderator:
Utafiti Mzuri! Pamoja na changamoto zote tunazopata, bado kuna tatizo kubwa sana kwa watanzania ni kutokuwa na mwamko wa kupiga kura. Kura ndio maamuzi ya mwisho kama unataka mabadiliko. ACHA kushabikia tu mtaani na mikutanoni, PIGIA KURA CHADEMA!

M4C inaendelea na itaendelea kuwafikia watu mijini na vijijini,elimu ya uraia imewafikia na inaendelea kuwafikia,kufika 2015 watu watakua wameelewa na hatimae SHETANI CCM litang'oka.Viva CDM,VIVA M4C Peopleeeeeees....... Power!!
 
Msijidanganye cdm hz takwimu mnapaswa kuzitafakari kwa kina kwani ingawa chama kinaungwa mkono na watanzania wengi lkn chama kama chama bd hakija kuwa, nasema hvy kwa nn? Lazima mlinganishe toka mwaka 1992-2013 ki uchumi chama kikowapi kimepiga hatua gani , idadi ya wanachama halali na waaminifu imeongezeka kiasi gani! Uwezo wa kutengeneza fursa za kiuchumi ki chama imefikia wapi? Ofisi za kueleweks kuanzia Taifa mpaka ngazi ya chama zipo?uongozi endelevu kuanzia Taifa mpaka chini upo?. Nasema hvy maana natambuwa kuwa cdm hakijatekeleza hy ambayo ndi yanayoosha kama chama kimekuwa. Kilichopo sasa ni kuwa cdm kina washabiki tuu ambao ni dkk mojo tuu wanaweza kugeuka na kikiacha chama kama kikombe kilichomaliza kunywewa maji yaani tupu. Jiimalisheni ktk hayo vinginevyo ni sawa na kundi kama la waigizaji tuu ktk democrasia na Siasa hapa Tanzania.

Endelea kujidanganya kwa vi takwimu uchwara vilivyokaa ki uharo uharo zaidi.2015 sio mbali mtaisoma number tu.
 
8 Reactions
Reply
Back
Top Bottom