Hii ndio tofauti niliyoiona kati ya Rais Samia na Hayati Dkt. Magufuli hadi sasa

Lord denning

JF-Expert Member
Jun 3, 2015
13,227
26,048
Amani iwe nanyi wanabodi

Leo nimeona nishare na nyie tofauti ndogo niliyoiona kati ya JPM na Samia Hadi sasa

1. Samia anafanya kazi kubwa sana ila haja invest kwenye mapambio ya kusifu na kuabudu.

Kielelezo cha haya ni takwimu kubwa zinazombeba zinazoendelea kutolewa hadi sasa kuhusu Tanzania kuipiku Kenya kuingiza bidhaa Uganda. Kama wote mmeona juzi bank kuu ya Uganda imetoa Takwimu kuwa kwa sasa Tanzania inaongoza kwa kuingiza bidhaa Uganda ikiipiku Kenya. Kama takwimu hizi zingetolewa kipindi cha JPM hadi sasa Msemaji wa Serikali angekuwa ameshaita press conference kulisema, Mataga nao wangekuwa wameshatengeneza picha kibao na zinasambaa kwenye mitandao, huku Gerson Msigwa nae akiwa anapost kwenye page yake na vijembe kibao.

Kwa upande mwingine Musiba na Magazeti yake wangekuwa wameshaandika nakala kibao kwenye magazeti yao na kumsifia JPM Kama JPM na wala sio CCM wala serikali. Bila kusahau vipindi vya TBC na Channel kuongelea hili Kwa kirefu zaidi.

2. Kuna kazi kubwa inafanywa kwenye miradi Ila Samia hapendi kuchukua sifa yeye Kama yeye bali kwa Serikali kwa ujumla.

Mfano wa haya ni kama ifuatavyo.
Jana Mkoa wa Dar es Salaam wamesaini mikataba kupitia tarula na wakandandari kujenga na kukarabati barabara za Maeneo ya Jiji la Dar es Salaam.

Ingekuwa kipindi cha JPM mikataba hii ingesainiwa Ikulu huku kukiwa na live coverage na mbele ya JPM peke yake. Ili siku ya mwisho sifa zirudi kwake kuwa yeye ndo ametoa hizo hela huku Paul Makonda akitoa sifa kem kem na kumfananisha JPM na Mtume au Nabii.
Ila chini ya Samia, Mkataba huu umesainiwa na Mkuu wa Mkoa tena bila hata Live coverage. Samia anataka kuonesha serikali inafanya kazi ila JPM alikuwa anataka kuonesha kuwa yeye ndo anafanya kazi. Kusaidiwa kwa Mkataba huu ni matunda yalioanza kuonekana na tozo ya miamala ambayo pesa zake ndo zinaenda kujenga hizi barabara kupitia Tarula Ila hatuoni majigambo haya kwa Samia.

Mwisho wa mfano kwenye hili jambo la pili ni Bandari ya Tanzania kupokea meli kubwa sana iliyoingiza mizigo ambayo asilimia 65 inaenda nchi za jirani. Ingekuwa kipindi cha JPM jambo hili pia lingefanywa kwa live coverage na sifa zote zingemrudia JPM kuonesha idadi ya mizigo kwenda nje kupitia Bandari yetu imeongezeka. Ila kwa Samia wala hili tukio halikuwa na live coverage na hakukuwa na mapambio ya kusifu na kuabudu kwake Samia Kama amekuwa Nani au mwokozi.

Mwisho napenda kusema kwa uchunguzi wangu mdogo, Samia anafanya mambo makubwa sana ila kimya kimya huku akiwa hataki sifa zirudi kwake binafsi tofauti na Mtangulizi wake ambae hata kwa madogo aliyokuwa akifanya sifa alitaka zirudi kwake binafsi. Anaendelea kutoa hela Bwawa la Nyerere na ujenzi unaendelea, anaendelea kutoa hela kwa wakandarasi wa barabara na reli na zinajengwa sana Kama inavyoonekana kule Mji wa Serikali Mtumba na Pia Kwenye reli ya umeme ila huyu mama hataki na hapendi sifa kwake binafsi bali kwa Chama chake na serikali yake.

Hongera Rais Samia.
 
Back
Top Bottom