Hii ndio Tanzania ya kesho chini ya Uongozi wa Rais Magufuli. Je wewe unaiona kesho tofauti na hii?

FPT

JF-Expert Member
Mar 23, 2017
1,201
1,839
Tangu rais Magufuli aingie madarakani 2015 amekuwa akithibitisha kwamba maamuzi waliyofanya watanzania ya kumchagua kuwa kiongozi wao hawakukosea, ni maamuzi ya hekima naye hatuangushi. Pia, anaendelea kututhibitishia kuwa kesho ya Tanzania ni nzuri kuliko jana. Kesho ya Tanzania imejaa mambo mazuri ya kufurahisha ambayo kila mtanzania anatamani kuwa mbele ya wakati kuona kesho ya Tanzania kuna nini.

Kama utakubaliana nami nina uhakika unaiona kesho ya Tanzania kama ninayoiona mimi. Mimi naiona kesho ya Tanzania ikiwa ni sehemu ya watu kujifunza uongozi wa mfano na wa msimamo ambao Rais Magufuli anautumia katika kuletea nchi na wananchi wake maendeleo. Hii ndio kesho ya Tanzania ambayo rais wetu anataka iwe na naiona ikiwa hivyo.

Kesho ya Tanzania itakuwa ni hazina ya kudumu ya watanzania juu ya Amani, utu, umoja na mshikamano katika kuleta maendeleo. Kesho ambayo watanzania watakuwa waadilifu, watiifu na wazalendo kwa nchi yao inajengwa leo na rais Magufuli.

Kesho ambayo kutakuwa na siasa za kishindani na zisizofuata misingi ya ubaguzi wa rangi, dini, kabila na kanda. Hii ndio kesho ambayo rais wetu anataka iwe na tunaiona inavyokuwa kwa kasi na vyama vyenye misingi tajwa hapo juu tunaona vikipukutika na kupukutisha wanachama kama mti kipindi cha kiangazi.

Kesho ambayo huduma za kijamii kama elimu, maji, afya zitapatika kila sehemu katika nchi yetu na kwa gharama nafuu sana ndiyo inayotengenezwa na Rais Magufuli leo kwa damu na jasho ili itimie.
Kesho ambayo bajeti yetu itategemea wahisani kwa kiwango kidogo sana, uzalishaji kukua maradufu kutokana na kuwepo kwa wataalamu wengi kwa kila sekta, viwanda ndio kuwa nyenzo muhimu katika maendeleo yetu ndio naiona ikitengenezwa na rais Magufuli leo.

Kesho ambayo wafanyakazi watafurahi kwa ongezeko kubwa la mishahara, wakulima watafurahi kwa kuwepo kwa soko la uhakika la mazao yao,wavuvi, wafugaji nao hali kadhalika ndio itakuwa Tanzania.
Kesho ambayo mimi raia wa kawaida kabisa nitakuwa nasafiri kwa SGR ama ndege kwa gharama nafuu kabisa. Kesho ambayo miundombinu ya barabara, madaraja itakuwa kila sehemu nchini ndio ninayoiona.

Mimi naiona kesho ambayo kila mtanzania atakuwa na furaha sana na kuienzi jana ambayo ndio hii ya leo ambayo baadhi wanaidharau. Tuwe wamoja katika kuijenga kesho yetu kwa sababu tuna kiongozi ambayo yupo tayari kutuongoza kufika huko na kwa uweza wake Mungu tutafika. Hii ndio kesho ya Tanzania niionayo, je wewe waona kesho ya namna gani?
 
Umewahi kujiuliza hilo gepu la vipato lilopo kati ya watawala na watawaliwa litapunguzwa na nani wakati sheria zinazobadilika ni za kuongeza kodi tu kwa wafanyabiashara na wazalishaji?

Kuna wastaafu walitumikia nchi hii kwa mishahara mikubwa na wakajiuzia Mali za umma kwa bei ya kutupa., wakashirikiana na wawekezaji na wafanyabiashara kujilimbikizia Mali nyingi sana ,majumba,mashamba , viwanja ,mahisa mengi kwenye mabenki n.k. Watoto wao wengine ni wakubwa serikalini na mishahara mikubwa ,wake zao wana ma NGO makubwa n.k lakini cha ajabu Kabisa bado wanalipwa mamilioni ya walipa kodi bila kuwajibika wala kufanya kazi ya kuzalisha kwa ajili ya kujenga Taifa.
Hawa ni zaidi ya wanyonyaji na wakoloni.

Kesho mzuri haitaleta na mtu mmoja kwani atakapoondoka ataacha vijana wengi wakiwa hawana ajira, wengi wakiwa hawana ,elimu ya maana , wengi wakiwa hawana uwezo kabisa wa kufanya biashara hata kwenda Burundi tu kununua vitenge.
Leo hii Dunia ni kama kijiji lakini kupata passport na visa kuna vikwazo vingi unategemea taifa la namna gani kama sio ndoto kama za wale magaidi wa Alshabab na Al kaida walivyokua wanapeana moyo huko porini kuwa wataitawala dunia kwa fikra zao.?

Unaweza kunionyesha mahali serikali imebana matumizi ya kununua magari ya kifahari na kupunguza misafara ya viongozi.
Leo hii hata mkuu wa wilaya ana msafara. Hujui magari yanatumia mafuta toka nje?

Huduma kama umeme ,maji, lini zitakua za bei nafuu wakati hata maji ya kisima binafsi yanalipiwa kodi ?
Umeme ungekua bei rahisi kama watu binafsi wangekua wanafursa ya kufunga panel zao za solar na kusambaziana umeme lakini sio huu wa Tanesco. Kinachofanyika ni kupumbaza watu akili. Kuna wanaoumia sana kwa kodi na gharama kubwa za umeme na maji ili wengine wapate kaunafuu kwa ajili ya kupiga kura kuwachagua mabeberu wa kuitafuna nchi lakini sio vinginevyo.

Bidhaa za viwandani zitakua vipi rahisi wakati umesema wafanyakazi watalipwa mishahara mikubwa na Wakulima watuza malighafi zao kwa bei kubwa ? Huo uzalishaji utakuaje wakati vipuri na machemical ya viwandani yananunuliwa kutoka nje?
Tuache kujenga nchi kwa dhana turudi kwenye uhalisia hata kama tutapunguza umaarufu wa mtu na Chama chake kuliko kufurahisha watu halafu miaka 20 ijayo watu wakajikuta ni maskini wa kutupwa hapa duniani.



Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mimi naiona kesho ambayo
Sasa wewe vipi.
Ni wewe unaiona Tanzania ya kusadikika au Magufuli ndivyo anavyoiona kama ulivyoanza kueleza hapo mwanzo!

Wewe ndie Magufuli, au mnao undugu?

Hiyo Tanzania yenu mpaka ipatikane, haki zetu mtakuwa mmetunyang'anya zote. Uhuru wetu mtakuwa mmepora. Hiyo Tanzania yenu itakuwa na faida gani kwetu kama raia tusiokuwa huru?
 
Hivi wewe ya leo tu umeshindwa kuyaona, ambayo ni ya hovyo kuwahi kutokea. Mtu aliyekuta mishahara inaongezwa kilamwaka yeye kashindwa, watu wanapandishwa madaraja yeye kashindwa, kakuta watu wanaajiriwa kila mwaka yeye kashindwa, kakuta wastaafu wanalipwa kwa wakati yeye kashindwa, thamani ya pesa dhidi ya dola kaikuta vipi kaifikisha wapi, bei ya mafuta, sekta binafsi kaikuta imeshamiri yeye kaiua, makusanyo ya kodi kaharibu, mzunguko wa fedha, mahusiano ya kimataifa na wawekezaji kaharibu yapo mengi sana ndugu, sasa hiyo kesho unayoizungumzia ni giza na shimo lenye kina kirefu sana kwa nchi hii naona unaota, mtu aliyeshindwa kumantain nchi alipoikuta ndio ataweza kuipeleka mbele hebu muogopeni Mungu.
 
Hivi wewe ya leo tu umeshindwa kuyaona, ambayo ni ya hovyo kuwahi kutokea. Mtu aliyekuta mishahara inaongezwa kilamwaka yeye kashindwa, watu wanapandishwa madaraja yeye kashindwa, kakuta watu wanaajiriwa kila mwaka yeye kashindwa, kakuta wastaafu wanalipwa kwa wakati yeye kashindwa, thamani ya pesa dhidi ya dola kaikuta vipi kaifikisha wapi, bei ya mafuta, sekta binafsi kaikuta imeshamiri yeye kaiua, makusanyo ya kodi kaharibu, mzunguko wa fedha, mahusiano ya kimataifa na wawekezaji kaharibu yapo mengi sana ndugu, sasa hiyo kesho unayoizungumzia ni giza na shimo lenye kina kirefu sana kwa nchi hii naona unaota, mtu aliyeshindwa kumantain nchi alipoikuta ndio ataweza kuipeleka mbele hebu muogopeni Mungu.
Wanapenda kusifia vitu abstract, na vilivyo giza wananchi wanaishi kwa tabu , wao hawaoni, hiyo SGR wareno wameondoka , makontracta wengine hawajalipwa zaidi ya miezi sita, bajeti za wizara haziendi, pesa hamna, ni bajeti ya waziri tuu inapewa, mwaka wa mkosi umeanza mvua ya kutosha hamna, kama ethiopia atakomaa , na ukipiga picha watu hawana chakula , wewe mxhochezi, sijui wanasema maendeleo gani hawa watu, lakini ni kawaida hata hitler alikuwa na mashabiki wake
 


Tangu rais Magufuli aingie madarakani 2015 amekuwa akithibitisha kwamba maamuzi waliyofanya watanzania ya kumchagua kuwa kiongozi wao hawakukosea, ni maamuzi ya hekima naye hatuangushi. Pia, anaendelea kututhibitishia kuwa kesho ya Tanzania ni nzuri kuliko jana. Kesho ya Tanzania imejaa mambo mazuri ya kufurahisha ambayo kila mtanzania anatamani kuwa mbele ya wakati kuona kesho ya Tanzania kuna nini.

Kama utakubaliana nami nina uhakika unaiona kesho ya Tanzania kama ninayoiona mimi. Mimi naiona kesho ya Tanzania ikiwa ni sehemu ya watu kujifunza uongozi wa mfano na wa msimamo ambao Rais Magufuli anautumia katika kuletea nchi na wananchi wake maendeleo. Hii ndio kesho ya Tanzania ambayo rais wetu anataka iwe na naiona ikiwa hivyo.

Kesho ya Tanzania itakuwa ni hazina ya kudumu ya watanzania juu ya Amani, utu, umoja na mshikamano katika kuleta maendeleo. Kesho ambayo watanzania watakuwa waadilifu, watiifu na wazalendo kwa nchi yao inajengwa leo na rais Magufuli.

Kesho ambayo kutakuwa na siasa za kishindani na zisizofuata misingi ya ubaguzi wa rangi, dini, kabila na kanda. Hii ndio kesho ambayo rais wetu anataka iwe na tunaiona inavyokuwa kwa kasi na vyama vyenye misingi tajwa hapo juu tunaona vikipukutika na kupukutisha wanachama kama mti kipindi cha kiangazi.

Kesho ambayo huduma za kijamii kama elimu, maji, afya zitapatika kila sehemu katika nchi yetu na kwa gharama nafuu sana ndiyo inayotengenezwa na Rais Magufuli leo kwa damu na jasho ili itimie.
Kesho ambayo bajeti yetu itategemea wahisani kwa kiwango kidogo sana, uzalishaji kukua maradufu kutokana na kuwepo kwa wataalamu wengi kwa kila sekta, viwanda ndio kuwa nyenzo muhimu katika maendeleo yetu ndio naiona ikitengenezwa na rais Magufuli leo.

Kesho ambayo wafanyakazi watafurahi kwa ongezeko kubwa la mishahara, wakulima watafurahi kwa kuwepo kwa soko la uhakika la mazao yao,wavuvi, wafugaji nao hali kadhalika ndio itakuwa Tanzania.
Kesho ambayo mimi raia wa kawaida kabisa nitakuwa nasafiri kwa SGR ama ndege kwa gharama nafuu kabisa. Kesho ambayo miundombinu ya barabara, madaraja itakuwa kila sehemu nchini ndio ninayoiona.

Mimi naiona kesho ambayo kila mtanzania atakuwa na furaha sana na kuienzi jana ambayo ndio hii ya leo ambayo baadhi wanaidharau. Tuwe wamoja katika kuijenga kesho yetu kwa sababu tuna kiongozi ambayo yupo tayari kutuongoza kufika huko na kwa uweza wake Mungu tutafika. Hii ndio kesho ya Tanzania niionayo, je wewe waona kesho ya namna gani?
 
Tangu rais Magufuli aingie madarakani 2015 amekuwa akithibitisha kwamba maamuzi waliyofanya watanzania ya kumchagua kuwa kiongozi wao hawakukosea, ni maamuzi ya hekima naye hatuangushi. Pia, anaendelea kututhibitishia kuwa kesho ya Tanzania ni nzuri kuliko jana. Kesho ya Tanzania imejaa mambo mazuri ya kufurahisha ambayo kila mtanzania anatamani kuwa mbele ya wakati kuona kesho ya Tanzania kuna nini.

Kama utakubaliana nami nina uhakika unaiona kesho ya Tanzania kama ninayoiona mimi. Mimi naiona kesho ya Tanzania ikiwa ni sehemu ya watu kujifunza uongozi wa mfano na wa msimamo ambao Rais Magufuli anautumia katika kuletea nchi na wananchi wake maendeleo. Hii ndio kesho ya Tanzania ambayo rais wetu anataka iwe na naiona ikiwa hivyo.

Kesho ya Tanzania itakuwa ni hazina ya kudumu ya watanzania juu ya Amani, utu, umoja na mshikamano katika kuleta maendeleo. Kesho ambayo watanzania watakuwa waadilifu, watiifu na wazalendo kwa nchi yao inajengwa leo na rais Magufuli.

Kesho ambayo kutakuwa na siasa za kishindani na zisizofuata misingi ya ubaguzi wa rangi, dini, kabila na kanda. Hii ndio kesho ambayo rais wetu anataka iwe na tunaiona inavyokuwa kwa kasi na vyama vyenye misingi tajwa hapo juu tunaona vikipukutika na kupukutisha wanachama kama mti kipindi cha kiangazi.

Kesho ambayo huduma za kijamii kama elimu, maji, afya zitapatika kila sehemu katika nchi yetu na kwa gharama nafuu sana ndiyo inayotengenezwa na Rais Magufuli leo kwa damu na jasho ili itimie.
Kesho ambayo bajeti yetu itategemea wahisani kwa kiwango kidogo sana, uzalishaji kukua maradufu kutokana na kuwepo kwa wataalamu wengi kwa kila sekta, viwanda ndio kuwa nyenzo muhimu katika maendeleo yetu ndio naiona ikitengenezwa na rais Magufuli leo.

Kesho ambayo wafanyakazi watafurahi kwa ongezeko kubwa la mishahara, wakulima watafurahi kwa kuwepo kwa soko la uhakika la mazao yao,wavuvi, wafugaji nao hali kadhalika ndio itakuwa Tanzania.
Kesho ambayo mimi raia wa kawaida kabisa nitakuwa nasafiri kwa SGR ama ndege kwa gharama nafuu kabisa. Kesho ambayo miundombinu ya barabara, madaraja itakuwa kila sehemu nchini ndio ninayoiona.

Mimi naiona kesho ambayo kila mtanzania atakuwa na furaha sana na kuienzi jana ambayo ndio hii ya leo ambayo baadhi wanaidharau. Tuwe wamoja katika kuijenga kesho yetu kwa sababu tuna kiongozi ambayo yupo tayari kutuongoza kufika huko na kwa uweza wake Mungu tutafika. Hii ndio kesho ya Tanzania niionayo, je wewe waona kesho ya namna gani?
Bia za bure za makonda zimewaathiri sana
 
Jiwe ni kiongozi wa hovyo kupata kutokea katika nchi yetu tangu tupate uhuru. Ni mbaguzi, mbinafsi, amayeendekeza ukanda, ukabila na udini. Ni mchonganishi na anayependa kuona wananchi wakiishi katika umaskini uliokithiri ili wapate kumtukuza na kumpigia magoti. Ni mshamba na limbukeni anayetaka wengine wasisifiwe hata kama wanafanya mambo makubwa na yenye tija kwa nchi yetu. Ni dikteta asiyezingatia utawala wa sheria na haki. Ni mpenda sifa asiyeona mbali kama mfalme Juha. Ana kila sifa inayomhusu mtu muovu.
 
Tunamshukuru Rais na Makonda kwa kuiwezesha TZ kufuzu afcon19
 
1% wanasifia
2% wanashauri
97% wanapinga

Hii inaonyesha mtu hana mvuto na ushawishi kwa anaowaongoza,mleta mada jitathmin unavyovisifia.
 
Back
Top Bottom