niachiemimi
JF-Expert Member
- Feb 18, 2015
- 3,496
- 4,920
Ufugaji wa kuku ni changamoto sana. Mwanzoni kwenye vifaranga 130, vilikufa vikabaki 20. vifaranga vilikua vinajikunyata sana, kinyesi kinaganda kwenye mnyeo, vilikua havina nguvu za miguu lakini vilikua vinadumaa sana yaani nikikuonyesha kifaranga cha miezi miwili ni kidogo sana hutaamini.Kwahiyo vinakufa 15 out of 95??..Basi uko njema mkuu ! Kuna mikuku ilikua unaiwekea mayai 12 kinatoa kifaranga kimoja..siwehu huo! Na Kuna miez na miez ya kutotoa..mie toka corona umeanza had leo sijamwekea kuku yai tunakula tu coz Kuna baridi sana
Nikaenda kuiba mbinu kwa jamaa fulani ili bachi ijayo ya vifaranga, nipunguze vifo.
Nilipopata vifaranga wengine 90, nilihakikisha vinakaa sehemu safi na vyombo vya chakula na maji ni visafi. Nikanunua chakula kwenye kampuni fulani inatengeneza chakula cha kuku. Nikanunua mifuko mitatu ya chakula cha vifaranga kuku wa nyama.
Vifaranga sikuvitoa nje, vilikaa ndani kwa siku 10 lakini siku ya saba nikavipiga chanjo ya matone. Baada ya ya siku saba tena nikawapiga tena chanjo ya matone. Nilihakikisha chakula wanachokula ni kile special tu.
Kati ya vifaranga 90, kilikufa kimoja tu. Hivi sasa nikikuonyesha kifaranga cha mwezi mmoja, hutaamini. Nasubiri vikikamilisha mwezi ndio nianze kuwapa Pumba, unga wa dagaa na mabaki ya misosi yetu.