AGITATOR
JF-Expert Member
- Apr 7, 2019
- 4,897
- 6,089
Bigup Sana. Watanzania wanamwelewa Sana jembe lao. Kiu ya kila mtanzania ni kuona nchi hii inakuwa Heaven on earth, nchi ya mfano duniani. Viongozi wenye maono, uzalendo wa kweli kwa watanzania ni kutoka CCM pekee. Hao wengine, kila mtu analake moyoni, kila mtu ataka awe yeye. Wajiuze wenyewe kwa mabeberu aisee, sio mama Tanzania.Habari za leo watanzania wenzangu, Natumai mu wazima wa afya njema.
Leo nitatoa orodha ya watanzania watakao mpigia kura Magufuli siku ya oktoba 28. Naomba ufuatane na mimi ili upate kuelewa vizuri kama hujui. Basi yafuatayo ndio makundi ya watu hao.
1. Watu wenye akili timamu, wanaojua kutafakari na kupambanua mambo. Hawa lazima wampigie kura Magufuli.
2. Watu wanaopenda kuona haki zikitendeka mahakamani, makazini na maeneo mbalimbali. Hawa lazima watampigia kura.
3. Watu wanyonge wanaojua akiwepo Magufuli ataweza kuondoa unyonge wao. Hapa kuna makundi mbalimbali. Hawa lazima watampigia kura.
4. Watu wanaopenda maendeleo na wanapenda kufanya kazi kwa bidii. Hawa lazima watampigia kura.
5. Watu wasiopenda ufisadi na mafisadi. Watu wasiopenda kusikia watu wanaiba pesa zetu huko mabandarini, TRA, na kwenye mataasisi yetu mbalimbali. Hawa lazima watampigia kura.
6. Watu wasiopenda rushwa. Hapa kuna makundi mbalimbali kuna wasiopenda kutoa rushwa na wasiopenda kupokea rushwa. Nina asilimia mia hawa lazima watampigia kura.
7. Wacha Mungu wote hawa lazima watampigia kura zote. Aliwaongoza kwenye maombi kipindi cha korona. Wala hakuruhusu makanisa yafungwe. Alisisitiza waendelee kumwomba Mungu na kufanya kazi.
8. Watu wasio wavivu na wanaopenda kufanya kazi kwa bidii kwa kiingereza tunasema non lazy people. Hawa lazima watampigia kura hawategemei serikali iwalishe wao wanajua kujituma kwaajili ya kufanya uzalishaji ndani ya taifa ni wajibu wa raia na sio kulala tu ukitegemea serikali ukuletee chakula.
9. Watu wanaopenda maadili mazuri kazini. Hawa lazima watampigia kura Magufuli.
10. Wanaopenda Tanzania iwe kama ulaya. Ukienda ulaya utaona jinsi mawasiliano yalivyo raisishwa. Kuna mabarabara ya juu, matren ya umeme na umeme wa uhakika. Hawa lazima watampigia kura Magufuli. Watu wanaopenda kuona wagonjwa wote hata viongozi wanatibiwa hapahapa Tanzania kwenye hospitali zetu.
11. Watu wanaopenda serikali inayowajibika kwaajili ya wananchi wake. Hawa lazima watampigia kura Magufuli.
12. Watu wanaopenda kuona haki ikitendekw kila maeneo. Hapa kuna wakinanamama, akina baba, vijana, n. k
13. Watu wanaopenda kuona serikali inayo ajiri kwa kufuata uwezo wa mtu na elimu aliyo nayo. Na sio kuajiri ovyoovyo hata kama mtu hana elimu wa uwezo wa kufanya kazi hiyo au kuajiri kwa kufuata undugu.. Kundi la watu hawa lazima limpigie kura Magufuli maana ndio mkombozi wao.
14. Watu wanaopenda rasilimali zetu zisiibiwe na mabeberu. Tanzania ni nchi yenye rasilimali za kutosha madini kila mkoa na wilaya. Tukiwa na Rais asiye na msimamo kwa mabeberu. Mabeberu wataiba madini na gesi yetu yote. Hivyo kinda lisilopenda haya kutokea nina asilimia Mia lazima limpigie kura Magufuli.
15. Watu wasiopenda kuonewa na mtu yeyote. Na wanajua kwamba wakimfuata Magufuli atawasaidia kukamata wale wanao waonea. Kundi hili nina asilimia mia lazima limpigie kura Magufuli.
Nimemaliza wakuu.
Na Ellyskywilly