Hii ndio Kozi nzuri ya kusoma chuo kikuu

mpatto

JF-Expert Member
Apr 28, 2017
766
1,027
Wana JF.

Basi, ikiwa zimebaki siku chache ili wanafunzi wa kidato cha sita waanze mitihani ya kumaliza elimu ya juu ya Sekondari, ni muhimu sasa kuwapa ushauri wakasome kozi ipi itakayowasaidia hapo baadaye.

Kipindi cha nyuma kidogo, watu walishauriwa kusoma masomo ya sayansi kwa sababu yalikuwa yana soko sana, yaani ajira zake zilikuwa zipo nyingi. Lakini tusidanganyane, kwa sasa hali ni tofauti, hata waliosoma Sayansi, bado wapo wengi tu mitaani hawajaajiriwa.

Kwa sasa naona kama wanaoajiriwa zaidi zaidi ni waalimu tena wa sayansi, au waalimu wale wa elimu maalum.

Sasa kutokana na kwamba si wote wanaopenda kuwa watumishi hasa katika fani ya ualimu wa elimu maalum, basi kwa hali iliyopo sasa ndugu zanguni ni hivi:

Nenda chuo, ukasome kozi ile unayoipenda, usifuate mkumbo wa kwamba kozi fulani ndio ina ajira, hilo kwa sikuhizi halipo. Bora ukasome kitu unachokipenda, ambacho unajua kabisa hata ukimaliza unaweza ukatoka na lolote la ziada linaloweza kukusaidia. Narudia tena, usichague kozi kishabiki. Mfano unachagua kishabiki, kozi ya Computer Security, lakini kumbe hata hobbie ya Linux huna, kisa tu uliambiwa ina mshahara mzuri utapopata ajira. Bora usome Bussiness Administration ambayo unajua una mpango wa kujiajiri mwenyewe hapo baadaye.

Mimi langu ni hilo tu ndugu zangu. Kama mtu una wazo tofauti basi unakaribishwa!!
 
1. Kilimo na mifugo. Usipoajiliwa utajiajili mwenyewe tena kwa mtaji kidogo sana. Wapo mtaani tena wana cheti tu wachache sana diploma. Kuna jamaa yangu ana diploma ya kilimo na mifugo alisoma Dodoma sijui ni chuo gani. Mpaka sasa hajaajiliwa hata zile nafasi tu za kutuma maombi hazijatoka!!! Lakini jamaa anapata sana kazi kwa wakulima na wafugaji ambako anaenda kutibu mifugo na kuwaelekeza matumizi ya pembejeo.

Alianza kwa kujitolea kupita nyumba hadi nyumba akitoa elimu bure. Wakamwelewa, siku hizi anapigiwa simu tu.....!!!

Wapo wanaotumia utaalam wa kilimo na mifugo kulima ama kufuga mifugo yao wenyewe.

2. Kasomee ardhi, hii sekta japokua imevamiwa na watu wengi lakini kila surveyor unaekutana nae atakwambia pamoja na wingi wetu lakini bado hatuwezi kukidhi mahitaji ya soko!!! Huku nako ajira zikikosekana, kujiajiri ni rahisi sana, wengi wana kampun za survey lakini hawana hata vifaa yani ni kukodi tu tena hawa masurveyor wapo wanaopata ajira serikalini na migodini wanazikataa ama wanaacha kwa madai kua madili ya mtaani yanalipa kuliko kamshahara ka milioni moja na nusu kwa mwezi!!!
 
1. Kilimo na mifugo. Usipoajiliwa utajiajili mwenyewe tena kwa mtaji kidogo sana. Wapo mtaani tena wana cheti tu wachache sana diploma. Kuna jamaa yangu ana diploma ya kilimo na mifugo alisoma Dodoma sijui ni chuo gani. Mpaka sasa hajaajiliwa hata zile nafasi tu za kutuma maombi hazijatoka!!! Lakini jamaa anapata sana kazi kwa wakulima na wafugaji ambako anaenda kutibu mifugo na kuwaelekeza matumizi ya pembejeo.

Alianza kwa kujitolea kupita nyumba hadi nyumba akitoa elimu bure. Wakamwelewa, siku hizi anapigiwa simu tu.....!!!

Wapo wanaotumia utaalam wa kilimo na mifugo kulima ama kufuga mifugo yao wenyewe.

2. Kasomee ardhi, hii sekta japokua imevamiwa na watu wengi lakini kila surveyor unaekutana nae atakwambia pamoja na wingi wetu lakini bado hatuwezi kukidhi mahitaji ya soko!!! Huku nako ajira zikikosekana, kujiajiri ni rahisi sana, wengi wana kampun za survey lakini hawana hata vifaa yani ni kukodi tu tena hawa masurveyor wapo wanaopata ajira serikalini na migodini wanazikataa ama wanaacha kwa madai kua madili ya mtaani yanalipa kuliko kamshahara ka milioni moja na nusu kwa mwezi!!!
Mkuu, ushauri mzuri huu kwa hawa madogo zetu form Six
 
Wana JF.

Basi, ikiwa zimebaki siku chache ili wanafunzi wa kidato cha sita waanze mitihani ya kumaliza elimu ya juu ya Sekondari, ni muhimu sasa kuwapa ushauri wakasome kozi ipi itakayowasaidia hapo baadaye.

Kipindi cha nyuma kidogo, watu walishauriwa kusoma masomo ya sayansi kwa sababu yalikuwa yana soko sana, yaani ajira zake zilikuwa zipo nyingi. Lakini tusidanganyane, kwa sasa hali ni tofauti, hata waliosoma Sayansi, bado wapo wengi tu mitaani hawajaajiriwa.

Kwa sasa naona kama wanaoajiriwa zaidi zaidi ni waalimu tena wa sayansi, au waalimu wale wa elimu maalum.

Sasa kutokana na kwamba si wote wanaopenda kuwa watumishi hasa katika fani ya ualimu wa elimu maalum, basi kwa hali iliyopo sasa ndugu zanguni ni hivi:

Nenda chuo, ukasome kozi ile unayoipenda, usifuate mkumbo wa kwamba kozi fulani ndio ina ajira, hilo kwa sikuhizi halipo. Bora ukasome kitu unachokipenda, ambacho unajua kabisa hata ukimaliza unaweza ukatoka na lolote la ziada linaloweza kukusaidia. Narudia tena, usichague kozi kishabiki. Mfano unachagua kishabiki, kozi ya Computer Security, lakini kumbe hata hobbie ya Linux huna, kisa tu uliambiwa ina mshahara mzuri utapopata ajira. Bora usome Bussiness Administration ambayo unajua una mpango wa kujiajiri mwenyewe hapo baadaye.

Mimi langu ni hilo tu ndugu zangu. Kama mtu una wazo tofauti basi unakaribishwa!!
Dah bro umetuacha dillema
 
1. Kilimo na mifugo. Usipoajiliwa utajiajili mwenyewe tena kwa mtaji kidogo sana. Wapo mtaani tena wana cheti tu wachache sana diploma. Kuna jamaa yangu ana diploma ya kilimo na mifugo alisoma Dodoma sijui ni chuo gani. Mpaka sasa hajaajiliwa hata zile nafasi tu za kutuma maombi hazijatoka!!! Lakini jamaa anapata sana kazi kwa wakulima na wafugaji ambako anaenda kutibu mifugo na kuwaelekeza matumizi ya pembejeo.

Alianza kwa kujitolea kupita nyumba hadi nyumba akitoa elimu bure. Wakamwelewa, siku hizi anapigiwa simu tu.....!!!

Wapo wanaotumia utaalam wa kilimo na mifugo kulima ama kufuga mifugo yao wenyewe.

2. Kasomee ardhi, hii sekta japokua imevamiwa na watu wengi lakini kila surveyor unaekutana nae atakwambia pamoja na wingi wetu lakini bado hatuwezi kukidhi mahitaji ya soko!!! Huku nako ajira zikikosekana, kujiajiri ni rahisi sana, wengi wana kampun za survey lakini hawana hata vifaa yani ni kukodi tu tena hawa masurveyor wapo wanaopata ajira serikalini na migodini wanazikataa ama wanaacha kwa madai kua madili ya mtaani yanalipa kuliko kamshahara ka milioni moja na nusu kwa mwezi!!!
Shukran sana ila sas kozi ipi kwnye ardhi hapo inaeza kuwa best ukilinganisha na zingne kwa kutegemea na soko linahtaji nn?
 
Shukran sana ila sas kozi ipi kwnye ardhi hapo inaeza kuwa best ukilinganisha na zingne kwa kutegemea na soko linahtaji nn?
Kasome geomatics acha kushangaashangaa.
Iwe diploma iwe bachelor degree itakulipa tu
 
Shukran sana ila sas kozi ipi kwnye ardhi hapo inaeza kuwa best ukilinganisha na zingne kwa kutegemea na soko linahtaji nn?
Jomba, usiangalie sana habari ya "uhitaji wa soko" kwa sababu, soko la ajira hubadilika badilika!

Kwa mfano, kuna mwaka Petrolium Eng pamoja na Telecoms zilikuwa deal sana, wengi wakajiingiza kipindi kile, lakini ona kilichotokea!

Kwoo ushauri wangu ni kuwa, ni mara mia usomee kitu unachokipenda, kwa kuwa utakuwa more creative na kutengeneza pesa zako mwenyewe!!

Usisome kwa lengo la kunufaika na ajira hapo baadaye, soma ili unufaike na elimu!!

Siku hizi ajira ni ngumu sana, zingatia hilo kijana!!
 
IFAKARA HEALTH INSTITUTE 👍👍👍
Msikariri Vyuo kwa MAJINA
Bill Gates was here
 
Hivi principal pass ni kuanzia alama ngapi ktk grades za A,B,C,D,E?

Na je E ni principal pass?
Msaada wadau.
 
Ushauri uliotukuka kabisa, na wengi hufeli kwa kufuata mkumbo kwa kisingizio cha ajira na tatizo hilo huanzia katika uchaguzi wa combination mpk kozi, na matokeo yake ni majuto makubwa.
 
Back
Top Bottom