barafu
JF-Expert Member
- Apr 28, 2013
- 6,726
- 32,818
Barabara zimeziba tofauti na week moja iliyopita mabapo mtaa wa Kongo na Msimbazi ilikuwa inapitika kwa urahisi.Hatari zaidi ni katika barabara ya Msimbazi ambapo machinga wengi wamemwaga bidhaa karibu na barabara za mabasi ya mwendo kasi na barabara za magari na hivyo kuleta hatari ya kutokea kwa ajali.Sasa Machinga wasio na vizimba wanatumia magari yaliyoegeshwa kama sehemu ya kutundukia bidhaa zao
Sasa mgambo wa jiji wamekosa kazi,kama Rais alivyowahi kuongea "Nikiwa Rais,Mgambo wakatafute kazi ya kufanya,sitakubali Machinga wasumbuliwe kwa kukimbizwa kimbizwa na mgambo".Japo wapo Machinga wanaoamini "neema" hii imekuja ili kuwaweka kando na Operation UKUTA.