Hii ndio aina ya wanaume wengi wa JF MMU, wanaune mko vizuri mno

Rasterman

JF-Expert Member
Feb 24, 2015
33,905
44,011
Habari za sasa wana JF MMU.

Nikiri kuwa ukifatilia stori za hapa na pale zinazopostiwa humu JFs utagundua kuwa wanaume wa humu wengi wamejaaliwa, wananemeka, wanabahati, wana mazali ya kufa mtu. Kwanza wanaume wa humu wana sifa zifuatazo

1. Wote ni mahandsome
2. Wote wana pesa, magari, majumba mazuri na mageto ya maana.
3. Kila mwanaume humu ana demu/mke mkali, mzuri, mrembo, mwenye shepu nzuri, sura kama malaika.
4. Wanaume wa humu hawanyanyaswi wala kusumbuliwa na wanawake.

5. Wengi hawatongozi ila wanatongozwa kutokana na mvuto walio nao wa sura au
Pesa.

6. Wengi wameshatembea na wanawake kuanzia 10 hadi 300. Hii ni baraka, zali la mentali.

7. Hawahongi.

stori nyingi za humu hazifanani na uhalisia huku kwenye jamii tunakoishi. Mademu wapo lakini siyo kama inavyooneshwa na kurahisishwa humu. Kuna mtu atakwambia amevuta mademu wote wa halmashauri fulani au wa ofisi fulani utadhani yeye ni mwanaume peke yake na wanawake wanamwangalia yeye tu. Wanaume tuache maigizo ya kujimwambafy inatupunguzia heshima sio sifa. Uongo haumusaidii kitu. Tutoe mastori ya kupendeza na kufurahisha lakini yawe na uhalisia.

Hata aliyelala guest bububu pale Buguruni za elfu 10 basi akija humu anasema alilala na demu mkali hotel fulani maarufu hapa Dar.

Hahahaaaa leo nimewaumbuaaa!!! Kama mbwai iwe mbwai tu.
 
Back
Top Bottom