Hii nchi ni hatari tuendako kama hivi ndivyo vigezo vya kupata ajira serikalini

faokipe

JF-Expert Member
Jan 20, 2015
1,017
1,172
Niende kwenye nada moja kwa moja ,nimemaliza kidato Cha sita mwaka 2019 nikapata nafasi ya kwenda chuo kikuu, mkopo sikupewa (nilikosa) kutokana na changamoto ya kipato kwenye familia nikawa Sina namna ya kuendelea na masomo ya elimu ya juu.

Juzi hapa likatoka tangazo la nafasi za kazi polisi nimeomba nkapeleka na Cheti Hadi Cha mafunzo ya JKT tunaambiwa tutaitwa kwenye usaili !!

Siku ya siku tukaitwa kupima afya kwenye usaili tunaambiwa wanaohitajika kwenye kazi ya polisi Ni form four wenye daraja la nne na form six daraja la tatu

Kwa hivyo vigezo nikatupwa nje ya usaili maana form form Nina division two na form six pia Nina division two!

Hapa najiuliza Ina maana kusoma kwangu huku hakunisaidii chochote

2: Jeshi la polisi linahitaji watu wasio na elimu kubwa?

Wakuu naomba kuwasiliana
 
Division 2 form six sio elimu kubwa dogo ufaulu wa daraja la pili mtihani wa kumaliza sekondari
 
Division 2 form six sio elimu kubwa dogo ufaulu wa daraja la pili mtihani wa kumaliza sekondari
Mimi sijasema Ni elimu kubwa ,na ndio maana nlitaka kuendelea na elimu ya chuo Ila uwezo umekua mdogo!!swali la kujiuliza Kama Kama div.two nimeachwa lakini mwenye div three anapata nafasi Ni wapi tunakoenda Kama nchi yenye watu weredi
 
Kama hakuna wa kukusimamia huwez pata. Ulizia mwaka juzi hapo twalipo utaambiwa kilichofanyika. Walitaka madokta 600 tu kilichotokea pale mm siombi kaz Kama hiz ikiwa sina refa kitengo
 
Niende kwenye nada moja kwa moja ,nimemaliza kidato Cha sita mwaka 2019 nikapata nafasi ya kwenda chuo kikuu ,mkopo sikupewa (nilikosa) kutokana na changamoto ya kipato kwenye familia nikawa Sina namna ya kuendelea na masomo ya elimu ya juu!!juzi hapa likatoka tangazo la nafasi za kazi polisi nimeomba nkapeleka na Cheti Hadi Cha mafunzo ya JKT tunaambiwa tutaitwa kwenye usaili !! Siku ya siku tukaitwa kupima afya kwenye usaili tunaambiwa wanaohitajika kwenye kazi ya polisi Ni form four wenye daraja la nne na form six daraja la tatu
Kwa hivyo vigezo nikatupwa nje ya usaili maana form form Nina division two na form six pia Nina division two!!hapa najiuliza Ina maana kusoma kwangu huku hakunisaidii chochote
2: jeshi la polisi linahitaji watu wasio na elimu kubwa??wakuu naomba kuwasiliana
Acha kulalalamika tafuta mtaji jiajili
 
hizo wala sio sababu za kukukatalia sababu kuu ya kukukatalia ni kwamba ulitaka kuingia bila connection (hela) jiongeze mkuu

nafasi zina wenyewe izo
 
Kama hakuna wa kukusimamia huwez pata. Ulizia mwaka juzi hapo twalipo utaambiwa kilichofanyika. Walitaka madokta 600 tu kilichotokea pale mm siombi kaz Kama hiz ikiwa sina refa kitengo
Lakini wew omba tu inawez ikawa ngekewa ila jitahid kumkarr hata mmoja katka hao wa usaili mvizie akitoka mfatilie hadi kwake. Nenda na maongez kiutu uzima siku ya pili (koneksheni tayari)
 
Ndio, jeshi la polisi linahitaji vilaza, maana watu mnaojitambua hamtakubali kupelekeshwa, ndio maana wanachukua hao mazezeta wayatumikisha kuzuia maandamano, nchi hii kuwa mjinga ni mtaji kwa wengine, ndio maana wanaogopa wajanja msiingie huko.
 
Back
Top Bottom