G Sam
JF-Expert Member
- Apr 20, 2013
- 11,555
- 35,880
Hii nchi imejikuta kwa miaka mitano hii ni vurugu tupu. Yani kama kuna mtu alikufa 2014 halafu akafufuka 2020 kisha akahadithiwa yaliyotokea atastaajabu.
Imagine spika wa bunge alivyo amemuita mbunge aliyejiuzulu kwa hiari yake ili arudi bungeni. Mbunge alikabidhi kadi ya chama kilichomdhamini ubunge hadharani akapewa kadi ya chama kingine. Leo huyo mbunge anaitwa kuendelea na ubunge wake kwa kutumia kilekile chama alichokikimbia.
Aidha Rais ametoa ndege kwenda kuchukua dawa ambayo masikini hata haijathibitishwa kuwa ni dawa. Rais wa nchi anayetoa dawa hajui hata dozi iweje kwa matumizi. Mbaya zaidi waziri msomi anainywa hadharani! Kama ni sumu? Hivi mbona kama nchi tumefikia kuchanganyikiwa hivi?
Dah acheni abane tu vyombo vya habari maana hivi tunavyovishuhudia ni vituko vya aina yake. Tuna ombwe kubwa la uongozi!
Imagine spika wa bunge alivyo amemuita mbunge aliyejiuzulu kwa hiari yake ili arudi bungeni. Mbunge alikabidhi kadi ya chama kilichomdhamini ubunge hadharani akapewa kadi ya chama kingine. Leo huyo mbunge anaitwa kuendelea na ubunge wake kwa kutumia kilekile chama alichokikimbia.
Aidha Rais ametoa ndege kwenda kuchukua dawa ambayo masikini hata haijathibitishwa kuwa ni dawa. Rais wa nchi anayetoa dawa hajui hata dozi iweje kwa matumizi. Mbaya zaidi waziri msomi anainywa hadharani! Kama ni sumu? Hivi mbona kama nchi tumefikia kuchanganyikiwa hivi?
Dah acheni abane tu vyombo vya habari maana hivi tunavyovishuhudia ni vituko vya aina yake. Tuna ombwe kubwa la uongozi!