Hii mitandao ya simu imeshatugeuza shamba la bibi!

Mu7

JF-Expert Member
Jun 15, 2013
1,549
1,804
HIvi sisi wateja wa huduma za simu ni nani mtetezi wetu? Kila siku haya makampuni yanatupandishia bei za huduma zao wanavyojisikia na hakuna wa kuwadhibiti!

Mwezi Januari nakumbuka TCRA walitoa ahadi kwa wananchi kuwa wamesikia kilio chetu kuhusu ughali wa gharama za mitandao ya simu na kuitaja tarehe 28 Februari kuwa siku ya kutangaza muarobaini wa tatizo hilo. Mpaka leo tarehe 2 Machi kimyaaaaaaa. Kama hawapo. Mambo kama haya huondoa imani kwa vyombo vyetu.

Sasa kama mtetezi wetu ndio hivyo hatusikii sauti yake, tunafanyaje? Dawa ni kuanza kususia makampuni haya ya kinyonyaji na kuhamia yenye nafuu.

TIGO ndio wamezidi kabisa. Bando la internet walilozoea kuniuzia kwa Tsh. 10,000 GB 7 kwa mwezi, leo wananiuzia GB 2.5 kwa bei hiyo hiyo ya Tshs 10,000 kweli? Inauma na haivumiliki.

Huu ni uhuni na wizi wa wazi kabisa. Huduma yao haijawa bora hivyo kiasi cha kupanda thamani kiasi hicho na kushusha thamani ya pesa yangu mteja.


Screenshot_20210302-065937.jpg
 
Kwani Feb 28 Waziri hakutoa tena tamko? Kama internet haipo na manufaa ni bora mtu usijiunge na kifurushi umiza.
 
Mitandao inaamini mawasiliano ni hitaji muhimu kwa binadamu kwa sasa hasa INTANETI hivyo wanatumia mwanya huo kutengeneza faida katika makampuni yao.

Thamani ya shilingi naona inazidi kudidimia kwenye tanuru la moto, haiwezekani shilingi 5000 kwenye suala la mawasiliano hasa INTANETI iwe sawa na Tsh 50 ya kununulia pipi kifua.

Hizi gharama tafsiri yake ni kuwa huwenda zina baraka kutoka kwa mamlaka zinazosimamia uendeshaji wa mitandao.
 
Waafrika badala ya kutafuta suluhisho tunalalamika lalamika Kama mbuzi aliyempoteza mamaye
Hizo ni changamoto kwa wateja lakini ni fursa kwako angalia mbele tafuta suluhisho
Mwaka 2008 nilipanga foleni kuanzia asubui saa 2 asubui hadi saa 10 jioni kulipa ada pale nmb clock tower arusha lakini Sasa hivi haya Mambo hakuna tena kwanini? Kwa sababu watu wameona fursa na kuleta mabadiliko acha kulalamika tumia fursa hiyo
 
Waafrika badala ya kutafuta suluhisho tunalalamika lalamika Kama mbuzi aliyempoteza mamaye
Hizo ni changamoto kwa wateja lakini ni fursa kwako angalia mbele tafuta suluhisho
Mwaka 2008 nilipanga foleni kuanzia asubui saa 2 asubui hadi saa 10 jioni kulipa ada pale nmb clock tower arusha lakini Sasa hivi haya Mambo hakuna tena kwanini? Kwa sababu watu wameona fursa na kuleta mabadiliko acha kulalamika tumia fursa hiyo
Unasikitisha sana wewe kiumbe mwenye fikira za kijasiriamali kila kona mwili wako.

Kupanda kwa gharama za mawasiliano unataka kuibadili kuwa fursa kivipi? Fursa ni hadi pale utakapoanzisha kampuni yako ya mawasiliano na kushusha bei ya gharama za mawasiliano ili upate faida.

FURSA limekuwa neno dhaifu linalozungumzika kirahisi kwa kila mwenye changamoto za maendeleo.
 
Waafrika badala ya kutafuta suluhisho tunalalamika lalamika Kama mbuzi aliyempoteza mamaye
Hizo ni changamoto kwa wateja lakini ni fursa kwako angalia mbele tafuta suluhisho
Mwaka 2008 nilipanga foleni kuanzia asubui saa 2 asubui hadi saa 10 jioni kulipa ada pale nmb clock tower arusha lakini Sasa hivi haya Mambo hakuna tena kwanini? Kwa sababu watu wameona fursa na kuleta mabadiliko acha kulalamika tumia fursa hiyo
hebu elezea hiyo fursa mzee baba
 
Hawawezi kupandisha bei za vifurushi bila sababu.. itakua wameongezewa kodi au gharama za uendeshaji zimepanda au vyote kwa pamoja.. nahisi serikali imejificha nyuma ya hili. Wakiicha mitandao ikitupiwa lawama na wananchi
 
HIvi sisi wateja wa huduma za simu ni nani mtetezi wetu? Kila siku haya makampuni yanatupandishia bei za huduma zao wanavyojisikia na hakuna wa kuwadhibiti!

Mwezi Januari nakumbuka TCRA walitoa ahadi kwa wananchi kuwa wamesikia kilio chetu kuhusu ughali wa gharama za mitandao ya simu na kuitaja tarehe 28 Februari kuwa siku ya kutangaza muarobaini wa tatizo hilo. Mpaka leo tarehe 2 Machi kimyaaaaaaa. Kama hawapo. Mambo kama haya huondoa imani kwa vyombo vyetu.

Sasa kama mtetezi wetu ndio hivyo hatusikii sauti yake, tunafanyaje? Dawa ni kuanza kususia makampuni haya ya kinyonyaji na kuhamia yenye nafuu.

TIGO ndio wamezidi kabisa. Bando la internet walilozoea kuniuzia kwa Tsh. 10,000 GB 7 kwa mwezi, leo wananiuzia GB 2.5 kwa bei hiyo hiyo ya Tshs 10,000 kweli? Inauma na haivumiliki.

Huu ni uhuni na wizi wa wazi kabisa. Huduma yao haijawa bora hivyo kiasi cha kupanda thamani kiasi hicho na kushusha thamani ya pesa yangu mteja.


Ukiona hvyo ujue serikali wanahusika moja kwa moja ndiyo maana wote wanapandisha kwa pamoja
 
Waafrika badala ya kutafuta suluhisho tunalalamika lalamika Kama mbuzi aliyempoteza mamaye
Hizo ni changamoto kwa wateja lakini ni fursa kwako angalia mbele tafuta suluhisho
Mwaka 2008 nilipanga foleni kuanzia asubui saa 2 asubui hadi saa 10 jioni kulipa ada pale nmb clock tower arusha lakini Sasa hivi haya Mambo hakuna tena kwanini? Kwa sababu watu wameona fursa na kuleta mabadiliko acha kulalamika tumia fursa hiyo
Motivesheno spika
 
hebu elezea hiyo fursa mzee baba
Ukishakuwa na fikra za kulia lia hauwezi kuona fursa. Kama unaona kupiga simu ni gharama mfuate huyo ndugu yako mkaongee ana kwa ana.
Watu watumie gharama kununua mitambo ya kuunganisha mawasiliano alafu wewe mpuuzi mmoja uje kulia lia gharama ni kubwa? Umeshajiuliza watu wametumia rasilimali kiasi gani kufanikisha Jambo hilo?
Nenda lab fanya tafiti vumbua mbinu yako ya kuwasiliana alafu punguza bei au fanya bure kabisa
Uholanzi inaishi juu ya maji, kuna nchi kila siku barafu imetanda juu ya nchi hao watu Kama wasingekuwa wabunifu na kutafuta suluhu ya matatizo yao wangekua hai kweli? Achane kulia lia tafuteni suluhu Kama hamna ongeza kipato chako kukidhi mahitaji yako.
 
Ukishakuwa na fikra za kulia lia hauwezi kuona fursa. Kama unaona kupiga simu ni gharama mfuate huyo ndugu yako mkaongee ana kwa ana.
Watu watumie gharama kununua mitambo ya kuunganisha mawasiliano alafu wewe mpuuzi mmoja uje kulia lia gharama ni kubwa? Umeshajiuliza watu wametumia rasilimali kiasi gani kufanikisha Jambo hilo?
Nenda lab fanya tafiti vumbua mbinu yako ya kuwasiliana alafu punguza bei au fanya bure kabisa
Uholanzi inaishi juu ya maji, kuna nchi kila siku barafu imetanda juu ya nchi hao watu Kama wasingekuwa wabunifu na kutafuta suluhu ya matatizo yao wangekua hai kweli? Achane kulia lia tafuteni suluhu Kama hamna ongeza kipato chako kukidhi mahitaji yako.
wewe una matatizo bila shaka, wakati unaoa ulituma washenga wakabargain bei ya mahari kwa wakwe zako mbona hukusema ukamuoe dada yako bure!?
 
Hawawezi kupandisha bei za vifurushi bila sababu.. itakua wameongezewa kodi au gharama za uendeshaji zimepanda au vyote kwa pamoja.. nahisi serikali imejificha nyuma ya hili. Wakiicha mitandao ikitupiwa lawama na wananchi
Huu ndo ukweli na ndo maana waziri husika amekaaa kimyaaa asijue lakufanyaa!
 
Msidanganywe na haya matamko ya mawaziri nyie wadanganyika, haya makampuni ya simu yana kitu kinaitwa 'cartel' lengo ni kumshawish/ kumrubuni mtu anaetaka kuharibu maslahi yao. Kumbukeni january makamba, na huyu waziri itakuwa hivyohivyo.
 
6 Reactions
Reply
Back
Top Bottom