Hii mikoba jamani!

PSYCHOLOGY

Senior Member
Feb 10, 2011
177
14
Habari members JF...!
Naomba kujulishwa kwa yeyote alie ona ukweli wa hii mikoba ya akina mama/baba utakuta mtu/me au ke ameubeba mkoba utadhani anasafiri kumbe anaenda kazini tena atakuepo huko kazini kwake kwa masaa kumi au tisa.
Najiuliza hua inabeba nini?
Maana kuna hospitali moja hapa mjini alikuepo dada mmoja kila siku anakuja home mkoba wake umejaa mashuka nets mikate maziwa... Hivyo hivyo kwa baba mwingine. Mbali na mikoba ya laptop...
Si kwamba nawachukia...kama ni uzito wa mikoba wanabeba wenyewe.
Nawakilisha!
 
Kama ni wanaume wanabeba documents mbalimbali muhimu kama id, diary,notebooks na vitu vingine vinavyomsaidia kazini na kwa upande wa kina mama ni kama manukato,tissue papers (anything might happen) kanga mobile phones,pochi nk
 
...siku moja nlimshangaa dada mmoja ameingia kwenye dala dala ana mkoba wake mkubwa...mbaya zaidi akaniwekea kichwani kwangu...nikawa napenda nipate thawab za kumbebea mzigo wake.
Tena alikua dada wa kimjin mjin...sikujua kwanin amenibebesha!
 
...siku moja nlimshangaa dada mmoja ameingia kwenye dala dala ana mkoba wake mkubwa...mbaya zaidi akaniwekea kichwani kwangu...nikawa napenda nipate thawab za kumbebea mzigo wake.
Tena alikua dada wa kimjin mjin...sikujua kwanin amenibebesha!

Hujaeleweka maalim, yani alikuwekea kichwani na wewe ukakausha tu?
 
Mikoba inashughuli nyingi; usione imebebwa tu... Ooh!

Kwa mfano kwa kina mama ukiacha vitu muhimu kama vile Khanga, pamoja na zile kinga zao za mzunguko wa kila mwezi, utakuta pia kuna uturi, podari, sare za kazini... Wapo wanaobeba kwa nia njema kama vile viji zawadi vya watoto wakati wakitoka kazini au matembezini.... Usishangae kukuta ndani ya mkoba kumefichwa visheti, kaimati, sikirimu au ramba ramba na bagia.... Ukipekua sana utakuta tooth pick... vipande vya toilet paper na wakati mwingine hubeba biashara ndogondogo za kuuziana maofisini.

Wale wanaobeba vipodozi hawa wako wengi tu na ikifika wakati utashangaa kwani hata kama yuko ofisini hujisahau kabisa akidhani yuko chumbani kwake jinsi anavyojiremba na na kujipodoa inafurahisha anapokosa kioo cha kujiangalia utamuona akitumia kompyuta bila shaka... au atakuuliza vipi XP nipo poa eeh!?

Kuna mshairi mmoja ameandika haya:

Mkoba wa mkononi, kwa kina mama hadaa
ukimuona njiani, mbwembwezake ni balaa
Akiufungua ndani, wallahi utashangaa

Wale wendao kazini, yanini kuuchukua
Nauli imkononi, imevunyangwa sawia
Mkoba wa kazigani, mahangasha kujitia

Akijapita mahali, alivyoukumbatia
Utadhani muna mali, aogopa kuibiwa
Kumbe muna miambili, na wanja kujipodoa

Harusini kiwaona, kilamtu pekepeke
Ni aina kwa aina, kwa kila mtu na wake
Aringa na kujiona, ati ni mzuri wake

Ata kama ana begi, safari akimbilia
Na huku ana mashungi, mwilini yaning'inia
Ni lazima handbegi, nayo kijipachikia

Hebu siri nambieni, enyi mnaoibeba
Mikoba ya mkononi, kwa nini mna mahaba
Ijapo mwendasokoni,kununua ngogo miba

Ukweli nielezeni, wala msifiche kitu
Mkoba wa mkononi, ni lazima kila mtu
Uutundike kwapani, japo ndani hakuna kitu

Tamati sasa naona, Kalamu naweka chini
Kina mama wasichana,na mtie akilini
Kama hakuna la maana, mkoba wacha nyumbani.
 
Hujaeleweka maalim, yani alikuwekea kichwani na wewe ukakausha tu?
Hujanielewa wapi?
Nilketi kiti cha m2 mmoja..nae dada huyo kaingia na hilo koba lake...kwa kua kulikua na abiria wengi...nae hakuweza kulibeba uzuri...ndipo akaliegesha juu ya kichwa changu...nikatulia tuli!
Au ww hujawahi kupanda dala dala iliojaa?
 
Mikoba inashughuli nyingi; usione imebebwa tu... Ooh!

Kwa mfano kwa kina mama ukiacha vitu muhimu kama vile Khanga, pamoja na zile kinga zao za mzunguko wa kila mwezi, utakuta pia kuna uturi, podari, sare za kazini... Wapo wanaobeba kwa nia njema kama vile viji zawadi vya watoto wakati wakitoka kazini au matembezini.... Usishangae kukuta ndani ya mkoba kumefichwa visheti, kaimati, sikirimu au ramba ramba na bagia.... Ukipekua sana utakuta tooth pick... vipande vya toilet paper na wakati mwingine hubeba biashara ndogondogo za kuuziana maofisini.

Wale wanaobeba vipodozi hawa wako wengi tu na ikifika wakati utashangaa kwani hata kama yuko ofisini hujisahau kabisa akidhani yuko chumbani kwake jinsi anavyojiremba na na kujipodoa inafurahisha anapokosa kioo cha kujiangalia utamuona akitumia kompyuta bila shaka... au atakuuliza vipi XP nipo poa eeh!?

Kuna mshairi mmoja ameandika haya:

Mkoba wa mkononi, kwa kina mama hadaa
ukimuona njiani, mbwembwezake ni balaa
Akiufungua ndani, wallahi utashangaa

Wale wendao kazini, yanini kuuchukua
Nauli imkononi, imevunyangwa sawia
Mkoba wa kazigani, mahangasha kujitia

Akijapita mahali, alivyoukumbatia
Utadhani muna mali, aogopa kuibiwa
Kumbe muna miambili, na wanja kujipodoa

Harusini kiwaona, kilamtu pekepeke
Ni aina kwa aina, kwa kila mtu na wake
Aringa na kujiona, ati ni mzuri wake

Ata kama ana begi, safari akimbilia
Na huku ana mashungi, mwilini yaning'inia
Ni lazima handbegi, nayo kijipachikia

Hebu siri nambieni, enyi mnaoibeba
Mikoba ya mkononi, kwa nini mna mahaba
Ijapo mwendasokoni,kununua ngogo miba

Ukweli nielezeni, wala msifiche kitu
Mkoba wa mkononi, ni lazima kila mtu
Uutundike kwapani, japo ndani hakuna kitu

Tamati sasa naona, Kalamu naweka chini
Kina mama wasichana,na mtie akilini
Kama hakuna la maana, mkoba wacha nyumbani.
....nimecheka karibu mbavu kupasuka/kuvundika!!!!
Hee hee hee...nimependa hayo mashairi.
 

Similar Discussions

0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom