Hii Machine ya Ukweli zile ambazo tunapaswa kuwa nazo AU R8, Kaa Mbali kabisa

Mkuu hii gari ile ya mwaka 2018 ndio ilikuwa na nguvu sana yaani hata Huracan haiikamati
Ina nguvu sana nilikanyaga mafuta nikategemea labda nguvu ya kuondokea itageuka lakini wapi
Kwa kweli Audi zote ni nzuri sana au tuseme heshima kwa mjerumani kwa gari zake zote

Niliendesha ikiwa na 3 miles on the clock ingawa kuna wengine huwa wanasema eti kitu 0 km lakini ukweli hakuna hiyo kila moja lazima ijaribiwe kabla ya kukabidhiwa
Mimi mpenzi zaidi wa SUV na Q7 ndio chaguo la uhakika ikiwa na V12 ingine
Inakwenda kama gari ndogo
Vipi kuhusu Volkswagen Touareg V10
 
Vipi kuhusu Volkswagen Touareg V10

Tatizo kwanza ni diesel na kuifanya kuwa na muungurumo mkubwa mno
Kwa uendeshaji wake ni mzuri ila inakula mafuta balaa
Yaani ukilinganisha na suv zingine hiyo inaachwa mbali sana
Kwa mfano Audi 4.2 litre V8 TDI Q7 inamtoa jasho na ni economy kuzidi Touareg
Hawakuibadilisha sana kama gari zingine wanavyofanya kila mwaka ila ilitamba miaka kama minne nyuma basi
 
Beira boy na kiduku lilo ni watu maskini sana lakini ukisoma thread zao unaweza jua wanauwezo wa kuikopesha serikali ya awamu ya tano
 
Tatizo kwanza ni diesel na kuifanya kuwa na muungurumo mkubwa mno
Kwa uendeshaji wake ni mzuri ila inakula mafuta balaa
Yaani ukilinganisha na suv zingine hiyo inaachwa mbali sana
Kwa mfano Audi 4.2 litre V8 TDI Q7 inamtoa jasho na ni economy kuzidi Touareg
Hawakuibadilisha sana kama gari zingine wanavyofanya kila mwaka ila ilitamba miaka kama minne nyuma basi
Vipi kuhusu perfomance ya Mercedes Benz ML matoleo ya kuanzia 2015 na kuendelea.
 
Hizi ndo mashine ambazo huwa nazungumzia.nadhani ndo maana nafikia hatua nawaza hivi kweli ntaweza endesha gari ya Mjapani? Ikiwa Ulaya na Marekani wanaendelea kuzalisha Magari mazito ya maana? Sijui.

View attachment 1223584

Engije ya hii Machine Muscle Car ni V10
Ina Speed 350
Horse Power yake ni 562
Ukianza kukanyaga accelerator kutoka 0-60kmh inachukua sekunde 3.5

View attachment 1223587
View attachment 1223590

Hii gari hata ukinunua. Kwa Tanzania hutaweza enjoy. Unaweza jikuta nawe unaonekana kama unaendesha vyombo vya usafiri kama Altezza,Subaru and the like.

Wengi hata thamani yake wanaweza wasifahamu. Kibaya hutaweza enjoy maana hamna barabara ya kuweza drive that car. Hizi barabara zetu zilizowekwa matuta kama ya viazi na kuhalalishiwa mashimo yaliyowekwa lami. Gari itakuwa inagusa chini na wakati mwingine haipandi sehemu nyingine.

Ni kama siku ya kwanza nmekuja TZ toka nchi za Watu. Ilikuwa Usiku nikawa nashangaa kwa nini barabara ya airport haijawekwa lami. Imeshindiliwa tu mpaka nafika oysterbay nikawa sielewi.nikajiuliza ina maana nchi ni maskini kiasi hicho. Siki mbili baadaye nikaja pita ile njia na kigundua kuwa watanzania wanaita barabara ya lami.nliumia sana.

Nikifananisha na barabara za usa,uk,scandinavian countries nlisikitika sana.

View attachment 1223600

Anyway msiwe bored na aina ya maisha yangu.maana hapa ningezungumzia Vyombo vya Usafiri vyaToyota ndo mngenielewa zaidi. But mimi nimeona nanyi wenzangu muweze enjoy Gari ndo maana nimewaletea kitu AUDI R8 machine ya Ukweli. Gari zenye Misuli.

Ndo maana huwa nashangaa kuna watu wanasema wanashindana kwa kutumia vitu vya kusafiria toka Japan. Siku mjaribu kushindana na gari sports za ukweli toka kwa wazungu.ndo mtaona raha ya ligi za barabarani.

Ndo maana mimi gari zangu ni RANGE ROVER, MERCEDES BENZ,BMW,FORD RANGER NA GMC. SASA NATAKA AUDI.

Hii machine si Ghali sana ni USD 240,000 Sawa na Tsh 500,000,000. Nakushauri kama wewe ni mtanzania mnyonge,mlalahoi na mwananchi. Hata ukipewa bure kataa. Waambie wakupe Chombo cha kukusafirisha tu toka Japan. Huwezi ihudumia hii machine. Na pia huwezi iendesha huko uswahilini sinza,kijitonyama na sijui wapi.
Sasa Kiduku. Hii gari Bongo unaendeshea wapi? Angalau gari kama AU A8L ya mwaka huu au mwaka jana. Mfano ya mwaka huu engine yake ina 563HP V8 pia twin turbo na yenyewe from 0 to 60mph ni 3 seconds na points.
 
ila ukweli upo kuna gari na kuna usafiri!! hapo nimecheka. wakati mtu na vits yake anatesa mpaka kaliua hadi manyovu na namikupa tandahimba acha kabisa!!
 
Kiduku kumbe hujui wenzio wakisema 0 - 60 wanamaanisha 60mph ≈ 100kmph

Hiyo 3.5 seconds ni 0 to 100kmph
 
Mkuu Benz nilikuwa nalo nikaliuza najua ni gari la uhakika
Ila nilikuwa nazungumzia Haya ambayo ni mapya kabisa na kuyaendesha
Mjerumani kwa gari zake zote yuko juu sana
hujakosea anything jerumani utapaenda. ila uwe vizuri kiasi maana na wese zinabugia ila spea mkataba hakuna kanjanja hapo!
 
Hapo ndo shida ndugu yangu. Hii gari kwa TZ hamna barabara za kuitumia. Mpaka siku tukianza kutengeneza barabara za lami ndo hii machine uta enjoy.

Sasa Kiduku. Hii gari Bongo unaendeshea wapi? Angalau gari kama AU A8L ya mwaka huu au mwaka jana. Mfano ya mwaka huu engine yake ina 563HP V8 pia twin turbo na yenyewe from 0 to 60mph ni 3 seconds na points.
 
Hapo ndo shida ndugu yangu. Hii gari kwa TZ hamna barabara za kuitumia. Mpaka siku tukianza kutengeneza barabara za lami ndo hii machine uta enjoy.
Kiduku Lilo nunua yatch ya kifahari uje upate raha baharini. Huku hakuna traffic, tochi,matuta wala njia mbovu.

Unatembea speed utakayo Dar kwenda Zanzibar ni masaa 3 wewe chukua yatch yenye engine za Volvo Penta dakika 45 unakuwa upo Zanzibar.
 
Kuna mfalme anaitwa Porshe Panorama ya mwaka 2017 huyu nadhani apewi promo ila amekamilika kila idara.

Huyo hapo mkuu yuko mbele anatanua
IMG_1039.JPG
 
Mzee baba bora wewe utupe live experience achana na huyu mjomba aliyekua anaomba ushauri amehamia tabata anatafuta wapi atapata garage ya kutengeneza gx 110(grande mark 2) yake.

Ule uzi wake wa juzi alipiga picha mitaa ya Vingunguti akielekea Barakuda
 
Back
Top Bottom