Hii kitu UPENDO kweli haichagui UMRI

Papa Mopao

JF-Expert Member
Oct 7, 2009
4,105
2,495
Kuna jamaa ana 30's kiumri, na mrembo binti wa umri kati ya miaka 16 mpaka 18 hivi, sasa jamaa anasema huyo msichana alipokuwa mdogo alikuwa akipenda sana kuwa naye karibu sana kiasi cha watu kumwambia si vizuri kuwa na uhusiano na mtoto mdogo kama huyo (wakati huo binti alikuwa bado mdogo kama darasa la tatu hivi au la nne)

Sasa jana kwenye sherehe ya mwaka mpya jamaa alinionesha jinsi huyo msichana anavyopenda kuwa naye karibu, kila alipo msichana anamfuata hata kama hajamwita na wanaongea kwa namna ya kiurafiki sana na msichana alikuwa huru sana mpaka nyamachoma anamletea jamaa kwa upendo kabisa.

Sasa alitoa swali, ninamnukuu "Hii ni nini? Ni UPENDO au nini? Maana toka zamani hisia hizi zilikuwepo na tukapoteana katikati hapo na leo tumekutana tena kwenye sherehe hisia ni zile zile kama za mwanzo na hii imekuwa tamu kupita ile ya mwanzo"

Na jamaa bado hajaoa na ana girl wake, na girl wake anajua hilo la huyo binti!
 
Huyo jamaa ni wewe........?

Mkuu Preta ha ha ha ha!

Hapana, siyo mimi...jamaa nimeongea naye leo asubuhi, nimekumbuka aliloniambia jana, sasa katika kufikiria ya kwake ndo nikalileta hii mada hapa!
 
Ni urafiki tu,ninavyojua mimi urafiki wa kawaida hudumu muda mrefu kuliko urafiki wa kimapenzi kati ya mwanaume na mwanamke ili mradi kuwe na mipaka tu!
 
Haya anyway ni upendo wa kawaida Kati ya kaka na dada mwambie amheshimu tuu binti wa watu
 
Sikiliza kijana, hakuna urafiki wa msichana na mvulana, lazima uta end in sex, ile nguvu ya neg and pos haipingiki, hiyo ni nature Mungu katuumba nayo, jinsi mwanamke na mwanaume wanapokuwa pamoja kwa muda mrefu na kuonana kila wakati wakiwa wenyewe faragha, lazima kunakitu itatokea
 
Sikiliza kijana, hakuna urafiki wa msichana na mvulana, lazima uta end in sex, ile nguvu ya neg and pos haipingiki, hiyo ni nature Mungu katuumba nayo, jinsi mwanamke na mwanaume wanapokuwa pamoja kwa muda mrefu na kuonana kila wakati wakiwa wenyewe faragha, lazima kunakitu itatokea

ndugu sijui unazungumzia urafiki gani. Kwani mimi kama mimi si kila rafiki yangu ni mpenzi wangu.ili muwe wapenzi inategemea akili zenu mmeziweka wapi
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom