GENTAMYCINE
JF-Expert Member
- Jul 13, 2013
- 56,544
- 108,871
Mama mwenye Nyumba wangu simwelewi kwani kutokana na Vyuma Kukaza kwa sasa nimemwambia nitampa Kodi yake baada ya muda kama wa Wiki mbili zijazo hivyo awe tu mvumilivu Kwangu lakini kuna ‘ Kajitabia ‘ kamezuka hivi karibuni ambako kananitatiza.
Tokea juzi hadi leo kila nikimsalimia tu iwe ni asubuhi au usiku akishamaliza kuniitikia tu anaingia ndani na kuweka Wimbo wa Tshala Muana ule aliourudia wa Hayari Fredy Ndala Kasheba wa ‘ Dezo Dezo ‘ halafu kila ukifika ule mstari usemao ‘ unapenda dezo dezo……kodi ya Watu hulipi…..’ anaurudia rudia sana huku anasonya ‘ msonyo ‘ mrefu wa Tegeta Nyuki hadi Mbagala Kizuiani.
Natamani sana nimuulize Kulikoni kila nikimsalimia anauweka huo Wimbo lakini naogopa asije niongezea Kodi au hata kunidai kwa nguvu halafu akanijazia Inzi ( akanitangazia kwa Watu hapa ) ikawa noma Kwangu hivyo nimebaki tu kuumia kimoyo moyo.
Je hii adha naipata Mimi tu peke yangu kama Mpangaji au kuna Wapangaji wengine huko mliko nanyi pengine yanawakumba makubwa zaidi ya hayo ninayopata Mimi? Tafadhali na Wewe weka Wimbo ambao lazima tu Mwenye Nyumba wako ukiwa umemkwaza au umemuudhi hasa kwa kutomuwahishia Kodi yake huwa anakuwekea
Nawasilisha.
Tokea juzi hadi leo kila nikimsalimia tu iwe ni asubuhi au usiku akishamaliza kuniitikia tu anaingia ndani na kuweka Wimbo wa Tshala Muana ule aliourudia wa Hayari Fredy Ndala Kasheba wa ‘ Dezo Dezo ‘ halafu kila ukifika ule mstari usemao ‘ unapenda dezo dezo……kodi ya Watu hulipi…..’ anaurudia rudia sana huku anasonya ‘ msonyo ‘ mrefu wa Tegeta Nyuki hadi Mbagala Kizuiani.
Natamani sana nimuulize Kulikoni kila nikimsalimia anauweka huo Wimbo lakini naogopa asije niongezea Kodi au hata kunidai kwa nguvu halafu akanijazia Inzi ( akanitangazia kwa Watu hapa ) ikawa noma Kwangu hivyo nimebaki tu kuumia kimoyo moyo.
Je hii adha naipata Mimi tu peke yangu kama Mpangaji au kuna Wapangaji wengine huko mliko nanyi pengine yanawakumba makubwa zaidi ya hayo ninayopata Mimi? Tafadhali na Wewe weka Wimbo ambao lazima tu Mwenye Nyumba wako ukiwa umemkwaza au umemuudhi hasa kwa kutomuwahishia Kodi yake huwa anakuwekea
Nawasilisha.