Hii ingetokea Tanzania wangesamehewa na kupewa hata tuzo au wangepewa adhabu zaidi?

GENTAMYCINE

JF-Expert Member
Jul 13, 2013
56,516
108,791
Wafungwa nane ( 8 ) waliokuwa katika Chumba kimoja katika Gereza moja huko Mjini Texas nchini Marekani waliamua kuvunja hicho chumba chao ili kuweza kumuokoa Askari Magareza aliyeanguka ghafla na kutapatapa ambaye pia alikuwa akiwalinda wao na kufanikiwa kumbeba hadi katika Hospitali ya Gereza hilo ili akapatiwe matibabu.

Naomba sasa kuuliza hivi kwa mfano " kibongo bongo " na tunavyojijua wenyewe hili tukio lingefanywa na Wafungwa wetu hapa wangesamehewa pengine hata kupewa tuzo kwa kitendo chao cha Kijasiri au ndiyo kwanza wangeongezewa adhabu pengine kwa kuvunja ile cell yao na kumbeba Askari Magereza aliyekuwa akiwalinda?

Karibuni " mtiririke ".
 
Kwanza hao wafungwa wenyewe wasingeweza kumpeleka huko hospital, kitu wangeweza fanya kwanza ni kummalizia kwanza na kutokomea
 
Back
Top Bottom