Hii inayoitwa Demokrasia USA, Ulaya ni Ujinga mtupu, sitaki tuelekee huko!

Barbarosa

JF-Expert Member
Apr 16, 2015
22,584
27,782
Nimekuwa mfwatiliaji mzuri sana wa Siasa za USA na bara la Ulaya kwa kiasi fulani na nilichojifunza sicho nilichokitegemea, kwamba hii wanayoiita Demokrasia USA na Ulaya ni usanii mtupu, na inawabomoa Wazungu kuliko kuwajenga, ukiangalia sehemu kubwa sana ni kukomoana, ni kwamba kwa kuwa fulani hapendwi au hakubaliki na kundi fulani basi wanatumia media na Wanasheria kumuharibia!

Mifano iko mingi kwa mfano Dominik Strauss Khan aliyekuwa Raisi wa Benki ya Dunia alitaka kugombea Uraisi nchini Ufaransa na alikuwa na nafasi kubwa sana ya kupita mpaka siku moja alivyoambiwa alimbaka mfagizi wa Hoteli New York akashitakiwa kesi ikaanza kusikilizwa jambo lililomuondoa moja kwa moja kwenye Uraisi, leo hii inajulikana Msichana alidanganya lkn mission accomplished!

Sasa hivi Trump, wanamuingilia kila mahali kwa kumsingizia kila kitu sasa hivi wamehamia kwa Mwanasheria Mkuu wake kwa kuwa ma neo-liberal na maglobalist hawamtaki Jeff Sessions ambaye ni m-conservative na yuko against abortion, Ushoga, Utransgender n.k. basi wameamua kumsingizia kwamba ana uhusiano na nchi ya Urusi na kwamba anahatarisha Usalama wa USA, wakati Hillary Clinton, Obama, Bushes wote walikuwa na Mahusiano ya moja kwa moja na Saudi Royal familly na hata Osama bin Laden alitokea Saudi Royal familly, lkn kimya, sasa hapo watatumia Wanasheria na kumshinikiza Session mpaka ataziujulu, akishajiuzulu tu kesi inaisha!

Tukija Ufaransa sasa hivi kuna uchaguzi mgombea anayeongoza kura za maoni na kupendwa na Wafaransa Francois Fillon tayari ameshafunguliwa kesi Mahakamani kwamba alishiriki sijui kwenye rushwa, sasa ukiangalia huyu Fillon hapendi Udikteta wa EU na pia hapendi Globalisation na ushoga, na lengo ni kumuondoa kwenye kinyang'anyiro cha uraisi kwa kumbambikizia kesi!

Hivyo nilichojifunza mwisho wa siku ni hii Demokrasia ya Ulaya na USA ni usanii tu, na ipo kwa ajili ya manufaa ya kundi fulani na wale wote ambao hawako kwenye hili kundi au wana mawazo tofauti na hili kundi basi wataaandamwa na media, Wanasheria na kufilisiwa au hata kufungwa lkn wale wahalifu hasa ambao wanaoingiza nchi vitani bila ya sababu ya maana isipokuwa sababu binafsi kama akina Bushes, Obama, Clinton husikii wakishitakiwa!
Binafsi napenda Demokrasia lkn tutafute aina nyingine na siyo hii ya USA na Ulaya, ni usanii na witch hunting tu ...


Paid demonstrators wakitaka Jeff Sessions ajiuzulu!
sessions23-640x480.



C58ZNVIVMAAfZlK.jpg:large


 
Ndugu yangu dunia hii inatawaliwa na waovu. Mwenye haki hana sehemu katika dunia hii.
Nitoke kwenye mada, kulikuwa na kampuni ya ujenzi na mtu mmoja mwenye haki ambaye alikuwa operator wa machine alikataa wazo la wizi wa mafuta kwenye mitambo. Sasa wakati wakichota kifusi wakafanya hila mpaka wakamuua kwa kumwangushia kifusi na kuonekana kuwa ni ajali. Mwenye haki kuishi katika ulimwengu huu ni kazi sana.
 
1 Reactions
Reply
Back
Top Bottom