Hii inatangaza utalii au inaonesha ni jinsi gani Tanzania ilivyo lawless?

Hofstede

JF-Expert Member
Jul 15, 2007
3,577
1,107
Richard Angel Matembelea Tanzania nia kuja na documentary fupi kuhusu some parts of Tanzania. Hadza or Hadzabe people: Wanaishi mapangoni, hawana nyumba wanaishi katika karne ya stone age. Je Tanzania inawatumia watu hawa kama kivutio cha utalii? au ni kukosa sera madhubuti za kuwastaarabisha?. Whatch the documentary via link below and think

[video]http://video.msnbc.msn.com/rock-center/46286427/#46286427[/video]

 
Last edited by a moderator:
Mkuu nadhani hawa watu wamelinda utamaduni wao. Na hilo ni jambo la kujivunia hivyo basi wanaweza kutumika kama sehemu ya kuonyesha utamaduni kwa kabila hilo ikiwa sehemu ya Tanzania.
Makabila kama hayo yapo mengi duniani na huwa kuna documentary inaonyeshwa kwenye channel ya National Geographic huwa ina cover makabila kama haya. Kuna jamaa humu avatar yake inaonyesha mwanamume akiwa hana nguo na ameficha nyeti zake kwa kitu kama fimbo hivi; hilo kabila ni kama hawa wahadzabe na wanapatikana huko papua new guinea. Tudumishe mila zetu ila siyo tuwe vivutio vya watalii. Watalii wavutiwe na tembo na twiga ila waje kujifinza utamaduni wetu!
 
Usisahau hata kule afrika kusini pamoja na kupiga hatua kubwa kwa maendeleo zaidi yetu ,lakini bado wanao watu kama hawa na filamu mfululizo za hawa ma -bushmens wa kalahali ni maarufu na zinapendwa dunani kote.

Ebu itafute mojawapo ya hizo Gods must be crazy afu utaelewa maana yake.na kwa taarifa tu ni kwamba kule man'ora wanakopatikana hawa watindiga wao wamekuwa ni boost kubwa kwa uchumi wa eneo husika tokana na utalii.
 
Mkuu, kama location yangu inavyoonesha niko Mangola ambako kuna idadi kubwa tu ya waHadza. Nimefanya kazi pia katika kuangalia namna ya kuwasaidia na kuboresha hali yao ya maisha.
Niseme kuwa si kweli kwamba kuna hitajia la 'kuwastaarabisha'. Wanao ustaafabu wao hata kama unaonekana kuwa primitive. Katika huku kutaka kujifanya tunawastaarabisha ndio yunavyozidi kufanya hali ya maisha yao kuwa ngumu. Ingawa sikubaliani na hali ya wao kufanywa 'kivutio', ningekufahamisha kuwa ziara za kuwatembelea waHadza ni moja ya components katika iteneraries za tour companies nyingi zinazoleta wageni huku Eyasi.
Ningeeleza zaidi ila nipo mobile.
 
Back
Top Bottom