Hii inasikitisha kwa wasomi wa Shinyanga??!

jonb09

New Member
Sep 27, 2009
3
0
Ndugu wana JF!

Ninasikitishwa sana na hali ya kielimu ya mkoa wa Shinyanga kuanzia ngazi ya chini. Kwa kweli mkoa huu umekuwa nyuma kielimu, mfano ukiangalia kuanzia ngazi ya msingi na kuendelea. Pia ukiangalia hata shule zetu za kata ni za kubabaisha.
Mara nyingi tumekuwa tukiilaum serikali kwa kutokujali elimu (Hili lina ukweli wake), lakini hata sisi kama wasomi tunayo nafasi ya kutoa mikakati ambayo kwa namna moja ama nyingine itasaidia kuukoa huu mkoa wetu. Kupata mawazo ya ya jinsi ya kusolve tatizo ni zaidi ya nusu ktk kusolve tatizo..


Kila mara utasikia Shinyanga, Shinyanga imeshika mkia! Why? Why Shinyanga Shinyanga kila wakati? No!! Enough is Enough! mi binafsi nimechoka kusikia hii kauli !

Kwa wale wasomi kutoka mkoa wa Shinyanga, popote mlipo duniani, ni wakati wenu wa kutoa mawazo yenu ili tuweze kuondokana na hii hali..

Kwa kuanzia naomba wale walio facebook, wajiunge SHINYANGA WASOMI COMMUNITY. Email ya Community ni obheja2010@gmail.com.

"Shinyanga!.. Raise education to the peak"... 2010

Mtu yeyote mwenye mapenzi na mkoa wa Shinyanga anakaribishwa kujiunga ili atoe mchango wake wa mawazo.

Na kama kuna mtu anaweza akafungua community ya Shinyanga mahala pengine afanye hivyo haraka hali si nzuri mkoani kwetu. Na kama atafungua basi tuziunganishe hizi communities za Wasomi wa Shinyanga..

Jon..
 
Sasa kila mtu akija hapa kwenye forums na kuhamasisha watu wa kijijini kwake wachangie maendeleo tutakuwa tunajadili kweli?

Ni wazo zuri kuchangia kuleta maendeleo sehemu husika, lakini hapa ni kwa manufaa ya jamii nzima, otherwise iwe shida ya dharula, kama ile harambee ya mzee mwanakijiji kuhusu waliopatwa na maafa ya mafuriko! nawakilisha.
 
jonb09, hizi nyuzi zako ziko 2 na zinafana, omba moja itolewe kwa manufaa ya wachangiaji basi
 
Sasa kila mtu akija hapa kwenye forums na kuhamasisha watu wa kijijini kwake wachangie maendeleo tutakuwa tunajadili kweli?

Ni wazo zuri kuchangia kuleta maendeleo sehemu husika, lakini hapa ni kwa manufaa ya jamii nzima, otherwise iwe shida ya dharula, kama ile harambee ya mzee mwanakijiji kuhusu waliopatwa na maafa ya mafuriko! nawakilisha.


Mtoa hoja ana maana nzuri.. Maendeleo ya taifa yanaanzia chini kwenda juu, na si juu kuja chini.
 
Back
Top Bottom