Hii imekaaje rev mtikila kushirikishwa kwenye kukusanya maoni ya katiba mpya?

mzambia

JF-Expert Member
Dec 31, 2010
885
60
Jamani wana jf nimesikia tetesi kuwa mch. Mtikila amemuandikia jk barua akiomba kuwemo kwenye tume ya kukusanya maoni kutoka kwa wananchi. Sijui imekaaje hii

naomba michango wana jf the great thinkers kwamba je anasitahili?
 
Mimi kwa kusema kweli huyu mchungaji wenu huwa namuona kama MZEE WA DILI tu hivi.

Huwa namuona kama vile yeye hufanya biashara ya kununua kesi toka kwa watu waoga waoga kisha yeye akatumie uzoefu wake alioupata akiwa karani wa mahakama baada ya miaka mingi ili atakapowachachafya wakubwa basi huitwa pembeni na kukatiwa fungu ambapo yule mwoga mwenye kesi yake naye Mtikila huwakatia ka 10 per senti.

Jambo hili linazungumzwa sana juu ya huyo mchungaji wenu. Na kama yumo ndani ya tume lolote basi sioni kama mambo yatakua tofauti sani.
 
Mimi kwa kusema kweli huyu mchungaji wenu huwa namuona kama MZEE WA DILI tu hivi.

Huwa namuona kama vile yeye hufanya biashara ya kununua kesi toka kwa watu waoga waoga kisha yeye akatumie uzoefu wake alioupata akiwa karani wa mahakama baada ya miaka mingi ili atakapowachachafya wakubwa basi huitwa pembeni na kukatiwa fungu ambapo yule mwoga mwenye kesi yake naye Mtikila huwakatia ka 10 per senti.

Jambo hili linazungumzwa sana juu ya huyo mchungaji wenu. Na kama yumo ndani ya tume lolote basi sioni kama mambo yatakua tofauti sani.

unaweza ukawa mtunzi mzuri sana wa hadithi, you know imagination is freely, evidence is costly,! people who dare to find evidence are actually exercising their free will power of adding value to human life in this planet! people who imagine tend to have day dream!, doing dirty-natural thing in secret places. Haiwezekani mtu ukaa na ku-magine

Unaweza ukawa ni mtoto, lakini kwa wanazungumzia mageuzi na kuleta changes hapa nchini Mtikila huwezi kumsahau wala kuzngumza utumbo, if we are finding faults, Think big!
 
Usije ukamdharau Mtikila hata kidogo, Ni mtu muhimu sana katika nchi hii. He is a real great thinker, ni mtu jasiri ambaye hajapata kutokea katika nchi hii. Alianza na wazo la kudai Tanganyika watu wote alicheka sana wakasema ni mwehu lakini leo tunaona umuhimu wake, akaja na hoja ya Mgombea binafsi kwa ujasiri alipeleka mahamani serikali ( Nani leo anaweza thubutu kuishitaki serikali) na akashinda kesi. Harakati za katiba mpya alizianza mapema mfumo wa vyama vingi ukianza akisema " Wapinzani hatuwezi tukashindana na CCM ikiwa vyombo vyote ni vyake Tume ya uchanguzi ya CCM, Mahakama ya CCM, Polisi wa CCM ni vigumu kushinda na kwa hiyo bila katiba hatutaweza kushindana" watu wakamzomea lakini leo ndicho tunachokutana nacho. kwakifupi huyu jamaa ni mtu muhimu sana wala si wakupuuzwa. mapungufu ni ya kila mtu maana hata JK mlimsifu sana mkasema jaguo la watu chaguo la mungu leo kiko wapi?
 
Ni kweli Mtikila ni mtu muhimu sana katika kuleta changamoto mbali zikiwemo hizi za kudai katiba mpya na kuruhusu wagombea binafsi, lakini wakati huo huo ni mtu ambaye imeshathibitishwa kwamba alienda kwa Rostam na kuchukua pesa za kujikimu.

Kwa maoni yangu huyu asiwemo kabisa katika hilo jopo maana anaweza kuleta kizungumkuti cha hali ya juu na hata kuvuruga utulivu/usikivu mkubwa unaotakiwa ndani ya jopo hilo katika kukusanya maoni toka kwa Watanzania wote. Na mafisadi wameshajua udhaifu wake mbele ya pesa basi wanaweza kabisa kumtumia ili kuharibu/kuvuruga vikao vya jopo hilo.
 
Usije ukamdharau Mtikila hata kidogo, Ni mtu muhimu sana katika nchi hii. He is a real great thinker, ni mtu jasiri ambaye hajapata kutokea katika nchi hii. Alianza na wazo la kudai Tanganyika watu wote alicheka sana wakasema ni mwehu lakini leo tunaona umuhimu wake, akaja na hoja ya Mgombea binafsi kwa ujasiri alipeleka mahamani serikali ( Nani leo anaweza thubutu kuishitaki serikali) na akashinda kesi. Harakati za katiba mpya alizianza mapema mfumo wa vyama vingi ukianza akisema " Wapinzani hatuwezi tukashindana na CCM ikiwa vyombo vyote ni vyake Tume ya uchanguzi ya CCM, Mahakama ya CCM, Polisi wa CCM ni vigumu kushinda na kwa hiyo bila katiba hatutaweza kushindana" watu wakamzomea lakini leo ndicho tunachokutana nacho. kwakifupi huyu jamaa ni mtu muhimu sana wala si wakupuuzwa. mapungufu ni ya kila mtu maana hata JK mlimsifu sana mkasema jaguo la watu chaguo la mungu leo kiko wapi?

Pamoja na umuhimu huo mnaoona kwa padri Mtikila sasa hili la kumuandikia raisi barua kuomba kuteuliwa nalo limekaeje sasa?
 
Ni kweli Mtikila ni mtu muhimu sana katika kuleta changamoto mbali zikiwemo hizi za kudai katiba mpya na kuruhusu wagombea binafsi, lakini wakati huo huo ni mtu ambaye imeshathibitishwa kwamba alienda kwa Rostam na kuchukua pesa za kujikimu.

Kwa maoni yangu huyu asiwemo kabisa katika hilo jopo maana anaweza kuleta kizungumkuti cha hali ya juu na hata kuvuruga utulivu/usikivu mkubwa unaotakiwa ndani ya jopo hilo katika kukusanya maoni toka kwa Watanzania wote. Na mafisadi wameshajua udhaifu wake mbele ya pesa basi wanaweza kabisa kumtumia ili kuharibu/kuvuruga vikao vya jopo hilo.

Kaka Waberoya upo mpaka hapo? Huyo ndiye shujaa wako padri Mtikila au tumpeleke hivo hivo kwenye tume itajulikanaga mbele kwa mbele?
 
mtikila hafai kabisa ni msanii tu kama mkwere, hakukanusha tuhuma za uswahiba wake na fisadi papa no2 baada ya mkweqe rostam azizi mpaka akawa anapewa pesa za kujikim, anaomba kazi kwa mkwere? Na njaa njaa zake lazima tu ataharibu mambo.
 
Mtikila ni jasiri sana katika kutafuta maslahi yake binafsi ...........kumbuka kilicho tokea Tarime mpaka aka pigwa na jiwe kichwani baadaye alipo ona ccm hawampi pesa yake na uchaguzi umesha fika akaanza kutoa siri zote jinsi walivyo kubaliaana na ccm ili kuidondosha CDM kwa propaganda za uongo......Huyu ni msanii tu.

Unakumbuka alivyo wa umiza wahindi na sera yake ya magabachori........walipigwa mawe pale jangwani wa hindi wawatu mpaka walijuta lakini alipo takiwa kunyang'anywa numba aliyo kuwa amepanga ya NHC wahindi wakachanga pesa na kumnunulia akakaa kimya mpaka leo hakutoa single yake ya magabachori.........huyu ni mcheza diri ingawa kweli huyu jamaa ana akili sana

Mmesahau alipo hamia CUF na akagombea ubunge ludewa alipo kosa aka rudi na matusi ya nguoni akiwa tukana viongozi wa CUF hadi akafukuzwa na kurudi tena DP baada ya kuona CUF hakuna dili ya fedha tena.........kwenye hili atuachie akae pembeni ila tuna mshukuru kwa kuamsha watanzania juu ya kupigania haki zao pamoja na kwamba yeye alikuwa mcheza dili tu.........
 
Mtikila mzee wa dili tu. Zile siasa zake za GARBACHOLI dhana ambayo alitisha nayo wahindi mpaka leo anaendelea kuvuta tu mifungu kila duka la kihindi anakopita.

Wale WALALAHOI aliodai kuwatetea mpaka leo hii watu bado hamjiulizi tu kwa nini Mtikila wenu huyo hajawahi kuwawakilisha hata siku moja wala hata kwenye ngazi ya KATIBU KATA achilia mbali katika ngazi za UDIWANI au UBUNGE. Siku zote Chama chake ni ndani ya brief-case tu.

Mtikila kwa KUCHEZA MICHONGO YA HELA duu!
 
Back
Top Bottom