Mimi kwa kusema kweli huyu mchungaji wenu huwa namuona kama MZEE WA DILI tu hivi.
Huwa namuona kama vile yeye hufanya biashara ya kununua kesi toka kwa watu waoga waoga kisha yeye akatumie uzoefu wake alioupata akiwa karani wa mahakama baada ya miaka mingi ili atakapowachachafya wakubwa basi huitwa pembeni na kukatiwa fungu ambapo yule mwoga mwenye kesi yake naye Mtikila huwakatia ka 10 per senti.
Jambo hili linazungumzwa sana juu ya huyo mchungaji wenu. Na kama yumo ndani ya tume lolote basi sioni kama mambo yatakua tofauti sani.
Usije ukamdharau Mtikila hata kidogo, Ni mtu muhimu sana katika nchi hii. He is a real great thinker, ni mtu jasiri ambaye hajapata kutokea katika nchi hii. Alianza na wazo la kudai Tanganyika watu wote alicheka sana wakasema ni mwehu lakini leo tunaona umuhimu wake, akaja na hoja ya Mgombea binafsi kwa ujasiri alipeleka mahamani serikali ( Nani leo anaweza thubutu kuishitaki serikali) na akashinda kesi. Harakati za katiba mpya alizianza mapema mfumo wa vyama vingi ukianza akisema " Wapinzani hatuwezi tukashindana na CCM ikiwa vyombo vyote ni vyake Tume ya uchanguzi ya CCM, Mahakama ya CCM, Polisi wa CCM ni vigumu kushinda na kwa hiyo bila katiba hatutaweza kushindana" watu wakamzomea lakini leo ndicho tunachokutana nacho. kwakifupi huyu jamaa ni mtu muhimu sana wala si wakupuuzwa. mapungufu ni ya kila mtu maana hata JK mlimsifu sana mkasema jaguo la watu chaguo la mungu leo kiko wapi?
Ni kweli Mtikila ni mtu muhimu sana katika kuleta changamoto mbali zikiwemo hizi za kudai katiba mpya na kuruhusu wagombea binafsi, lakini wakati huo huo ni mtu ambaye imeshathibitishwa kwamba alienda kwa Rostam na kuchukua pesa za kujikimu.
Kwa maoni yangu huyu asiwemo kabisa katika hilo jopo maana anaweza kuleta kizungumkuti cha hali ya juu na hata kuvuruga utulivu/usikivu mkubwa unaotakiwa ndani ya jopo hilo katika kukusanya maoni toka kwa Watanzania wote. Na mafisadi wameshajua udhaifu wake mbele ya pesa basi wanaweza kabisa kumtumia ili kuharibu/kuvuruga vikao vya jopo hilo.