Hii ikoje wadau

isack raphael

Senior Member
Oct 26, 2013
139
30
Tangu mwaka 2009 nilikua naomba kujiunga JKT nikia na cheti cha sekondar na nilikuwa na umri kati ya 18 hadi 23 kulingana na vigezo vya JKT ila nilikosa.
Kwasababu napenda kupita JKT niliamua niende chuo nipate angalau cheti,nikafanikiwa kupatata cheti mwaka 2011 na mwaka 2012 nikaapply tena JKT nikiwa na umri wa miaka 24 na profession yangu lakini bado sikufanikiwa...
Nilikuwa na wazo la kuendelea na diploma ila ada ni tatizo hadi sasa nipo tu kijiweni nasugua gaga,nimeona tangazo la kujiunga na JKT ila vigezo nimevikosa hasa kuhusu umri.

Wadau naomba mnipe mwongozo nini nifanye ili nipate chansi ya kutumikia jeshi...kwasababu napenda sana kuwa katika nafasi flani ya jeshi letu la tanzania.

Nawasilisha
 
likuepukalo lina kheri na wewe...muombe Mwenyezi Mungu akujaalie upate kile anachoona yeye kuwa unastahili na kitakufaa...
 
Back
Top Bottom