Sky Eclat
JF-Expert Member
- Oct 17, 2012
- 57,597
- 215,270
Chakaza nimecheka sana leo. Ninasikia kule shingoni kwenye mirija ya kupitisha damu kwenda kichwani watu wako tayari na visu vilivyonolewa.Awali hakuwa anaiogopa 2020 kwani alikuwa na uhakika CCM watampitisha na uchaguzi mkuu atatumia Polisi na NEC ya ma DED kulazimisha ushindi.
Sasa huko CCM moto, Membe anakuja kininja tena akiwa na support kubwa kutoka kwa wakongwe wa chama ambao "wakuja" Bashiru kawamwagia "petrol" ya matusi na kuchomoa wire wa betri.
Huku nje nako NEC nayo sio ya kutegemea sana maana hili suala la kuwaondoa maDED kusimamia litafanya uchaguzi kuwa mgumu na wizi utumie nguvu zaidi ili hali macho ya wababe ulimwenguni yana mwangalia kwa makini.
Lazima abadilike tuu, tusishangae siku akitamka shikamoo jukwaani.