#COVID19 Hii hapa ni nafasi yako ya kuibadili dunia, itumie

"Kuondoa huo mkanganyiko na kuzuia wenye tamaa na nia mbaya wasitumie upenyo huo kukwamisha zoezi la chanjo, serikali inataka mtu aridhie na akubali kama akipata madhara hatailaumu au kuishitaki kwa hilo."

Sasa hapo mkuu vp ambao ikitokea kweli wakapata madhara yenye kusababishwa na hizo chanjo?
Siyo kwamba ukipata madhara kwa chanjo basi serikali inakutelekeza.
Hapana, utasaidiwa kabisa na ndiyo maana hata ukishapata chanjo, unaendelea kufuatiliwa na unapewa namba za kuripoti pale unapopata changamoto.
Kinachozuiwa hapo ni watu wasitumie huu mwanya kujinufaisha kifedhaz uende ukafungue kesi ya kudai mabilioni ya fedha kwa kusema chanjo imekuletea madhara.
 
Siyo kwamba ukipata madhara kwa chanjo basi serikali inakutelekeza.
Hapana, utasaidiwa kabisa na ndiyo maana hata ukishapata chanjo, unaendelea kufuatiliwa na unapewa namba za kuripoti pale unapopata changamoto.
Kinachozuiwa hapo ni watu wasitumie huu mwanya kujinufaisha kifedhaz uende ukafungue kesi ya kudai mabilioni ya fedha kwa kusema chanjo imekuletea madhara.
Sawa ila hapo sasa watakaopata madhara kweli ya chanjo wamenyimwa haki ya kushitaki.
 
Literature za yote hayo ziko wazi mkuu, kama unapenda kujisomea nakuwekea link hapa ujisomee.
Lengo la mimi kuandaa darasa hili fupi ni kueleza hilo kwa lugha ya darasa la tano, ili kila mmoja aelewe na kufanya maamuzi sahihi.
1. Pfizer and BioNTech Conclude Phase 3 Study of COVID-19 Vaccine Candidate, Meeting All Primary Efficacy Endpoints | pfpfizeruscom

2. Different COVID-19 Vaccines
Mimi mwenyewe ni darasa la saba tu mkuu ndio maana nikaomba ujapo kwa uchache uelezee hilo suala kwa lugha ya darasa la 7 japo nami nipate chochote kitu maana hiyo lugha nyengine ni mtihani kwangu.

Kwa uchache tu.
 
Mkuu,
Tabia ya kuchagua kusikia kile tu unachotaka kusikia wewe, itakukosesha mengi mazuri kwenye maisha.
usiwe mgando (fixed) dunia inakwenda kasi, mambo yanabadilika.
Kuchanja wewe ni swala la muda tu, hivyo usishupaze sana shingo, utachanja.
Sichanji.
 
Mimi mwenyewe ni darasa la saba tu mkuu ndio maana nikaomba ujapo kwa uchache uelezee hilo suala kwa lugha ya darasa la 7 japo nami nipate chochote kitu maana hiyo lugha nyengine ni mtihani kwangu.

Kwa uchache tu.
Kwa uchache ni hayo niliyoeleza hapo juu, yanatosha kabisa mtu kufanya maamuzi sahihi kwenye hili.
Karibu.
 
Rafiki yangu mpendwa je umeelewa ulichokiandika au umeandika tu kukamilisha mstari!!!
Inakuaje watu wafuatilie jambo lisilo na ufanisi wa 100%, je wewe unaweza kufanya kazi unayolipwa mshahara wa kukidhi mlo tu, je ukiumwa utaomba msaada kwa ndugu?
Mkuu, kama umefanikiwa kusoma darasa nililoweka hapa, hata baada ya bidhaa kuingia sokoni, lazima iendelee kufuatiliwa.
Mfano kwenye hili la chanjo, lazima iendelee kufuatiliwa je mtu akipata kinga ya chanjo anakaa nayo kwa muda mrefu kiasi gani? Je kuna uhitaji wa kuendelea kuchoma tena ili kuboost kinga? yote hayo yanajulikana kwa tafiti zinazokuwa zinaendelea. hivyo ndivyo sayansi inavyofanya kazi na ndiyo maana tumeweza kupiga hatua kwenye maeneo mengi, kwa tafiti na kuangalia kile ambacho kinaweza kuwa improved zaidi.
 
Kwanini serikali iseme haiko answerable na consequences baada ya chajo?

Kwanini waliochanjwa wawe na same degree of exposure kama ambao hawajachanjwa?

Kwanini watu wahimizwe kuendelea kuvaa mabarakoa sijui na ku sanitize baada ya chanjo kama ambao hawajachanjwa?
hayo maswali yalishajibiwa, fatilia acha uvivu wa kiseng*
 
Chanjo hizi zinazotumika sasa ni zile zilizoanza fanyiwa tafiti wakati ule covid 19 inagundulika Wuhan na kwingineko duniani, tumeshuhudia wadudu hawa wakibadika na kuja kwa adhari na madhara zaidi ya yale ya awali,

Mfano Delta na sasa Lamda je bado tuamini chanjo hii ni msaada tosha ama ni sehemu ya majaribio?
 
Back
Top Bottom