Makirita Amani
JF-Expert Member
- Jun 6, 2012
- 1,781
- 3,074
- Thread starter
- #41
Siyo kwamba ukipata madhara kwa chanjo basi serikali inakutelekeza."Kuondoa huo mkanganyiko na kuzuia wenye tamaa na nia mbaya wasitumie upenyo huo kukwamisha zoezi la chanjo, serikali inataka mtu aridhie na akubali kama akipata madhara hatailaumu au kuishitaki kwa hilo."
Sasa hapo mkuu vp ambao ikitokea kweli wakapata madhara yenye kusababishwa na hizo chanjo?
Hapana, utasaidiwa kabisa na ndiyo maana hata ukishapata chanjo, unaendelea kufuatiliwa na unapewa namba za kuripoti pale unapopata changamoto.
Kinachozuiwa hapo ni watu wasitumie huu mwanya kujinufaisha kifedhaz uende ukafungue kesi ya kudai mabilioni ya fedha kwa kusema chanjo imekuletea madhara.