Hii hali ya sasa inatisha sana!!!

Abbasfarudume

JF-Expert Member
Feb 14, 2017
1,625
1,323
Wakuu nina maana yangu kusema hivyo, kuwa hali ya sasa hivi inatisha haswa kwenye nyumba hizi za kulala wageni al maarufu guest house ukienda sehemu sio ujichukulie tu mradi guest haswa hizi zilizo uswazi ndani ndani au za uchochoroni ni hatari sana, unashangaa katikati ya usingizi mida mibovu mnaweza kuvamiwa hata na majambazi usiku wa manane wakajua mna hela nakadhalika mkapigwa na kuteswa hata umauti unaweza mtu kukufika kisa tu ushetani na tamaa zao za mali ikichangiwa na ugumu wa maisha, sawa siwakatazi kulala guest house lkn bora mchague sehemu ilio na uhakika wa usalama na roho yako na mali zako hali imekuwa tafrani kwa usawa huu tulio nao na ukizingatia sikukuu ya eid fitri iko njiani waharifu wanatafuta hela kwa njia mbali mbali.... Napenda kuwakilisha kwenu wakuu.!
 
Sawa, ila inasikitisha kuona baadhi ya polisi wasio waadilifu wakijihusisha/ wakishirikiana wahalifu.
 
Ugumu wa maisha ndio kipimo cha akili! Wanadamu wapo radhi kutumia mbinu yeyote hata kuua ili-mradi wafanikishe mambo yao tu! Ahsante kwa taarifa mkuu!
 
kabisa..hiyo hali ipo maeneo gani mkuu
Sehemu nyingi tu za Uswaz mkuu... Keko, tabata, kimara, kinyerezi, kibangu, msewe, mburahati manzese, tandika, kipunguni, kivule, msongola, kitunda, gongolamboto, majohe, urongoni, mwananyamala, mbagala, karakata, kiwalani, vingunguti, kigogo, chang'ombe temeke mtoni kichangani, hadi kwa azizi ally mkuu.
 
Sehemu nyingi tu za Uswaz mkuu... Keko, tabata, kimara, kinyerezi, kibangu, msewe, mburahati manzese, tandika, kipunguni, kivule, msongola, kitunda, gongolamboto, majohe, urongoni, mwananyamala, mbagala, karakata, kiwalani, vingunguti, kigogo, chang'ombe temeke mtoni kichangani, hadi kwa azizi ally mkuu.
poa kumbe ni huko Dar..huku kwingine hali ni tofauti
 
Sehemu nyingi tu za Uswaz mkuu... Keko, tabata, kimara, kinyerezi, kibangu, msewe, mburahati manzese, tandika, kipunguni, kivule, msongola, kitunda, gongolamboto, majohe, urongoni, mwananyamala, mbagala, karakata, kiwalani, vingunguti, kigogo, chang'ombe temeke mtoni kichangani, hadi kwa azizi ally mkuu.


Duuuuuuh

Aiseeeeeh, majina tu yalivyo yanatisha Je, maeneo hayo yakoje!?

Weka picha kwa kuongeza vielelezo.
 
Mkuu umenikumbusha leo asubuhi nikiwa town nimekaa nje ya office yangu kwa nje ni sehemu ambayo yeyote anaweza kukaa,sasa kuna jamaa alikaa kwa pembeni kidogo sasa mi nikiwaza yangu ya kichwani mara jamaa huyu hapa kanisogelea mkononi ana mfuko wa rambo akiniambia brother mi mji huu mgeni naomba kama simu yako ina credit nisaidie niongee na jamaa yangu kanielekeza nimkute mtaa huu,wakati anasubiri jamaa yake asogee alipokuwa zikaanza story mara akiniambia huyo jamaa aliyempigia ni boss wake wa zamani amemuomba amsaidie nauli arudi alikotoka na kilichomkuta ni kwamba katokea Arusha kuja Dar kuchukua mzigo wa viatu vya watoto target yake aviuze msimu wa sikukuu ukifika ila mwenyeji wake kamuibia hela 2,300,000/=,simu vitambulisho pamoja na viatu hotel aliyoshukia,nikamuuliza ilikuwaje mwenyeji wako akiache chumba chake aje kulala na wewe guest?hakuwa na jibu zaidi kujiuma uma tu.jibu nililipata aliponiambia kwamba tukio limemtokea Manzese nikaunganisha dots na the way alivyokuwa akijieleza nikamstukia kwamba huyu lazima kakutana na wale dada'poa wa Lambo Motel au wa Savannah Bar wakamuingiza mjini,wale nawajua ukijichanganya wanaweza kuondoka mpaka na kichwa chako ukiwa hujui.
 
Wakuu nina maana yangu kusema hivyo, kuwa hali ya sasa hivi inatisha haswa kwenye nyumba hizi za kulala wageni al maarufu guest house ukienda sehemu sio ujichukulie tu mradi guest haswa hizi zilizo uswazi ndani ndani au za uchochoroni ni hatari sana, unashangaa katikati ya usingizi mida mibovu mnaweza kuvamiwa hata na majambazi usiku wa manane wakajua mna hela nakadhalika mkapigwa na kuteswa hata umauti unaweza mtu kukufika kisa tu ushetani na tamaa zao za mali ikichangiwa na ugumu wa maisha, sawa siwakatazi kulala guest house lkn bora mchague sehemu ilio na uhakika wa usalama na roho yako na mali zako hali imekuwa tafrani kwa usawa huu tulio nao na ukizingatia sikukuu ya eid fitri iko njiani waharifu wanatafuta hela kwa njia mbali mbali.... Napenda kuwakilisha kwenu wakuu.!
Ohoooo unaona sasa mjini shule
poa kumbe ni huko Dar..huku kwingine hali ni tofauti
 
Sehemu nyingi tu za Uswaz mkuu... Keko, tabata, kimara, kinyerezi, kibangu, msewe, mburahati manzese, tandika, kipunguni, kivule, msongola, kitunda, gongolamboto, majohe, urongoni, mwananyamala, mbagala, karakata, kiwalani, vingunguti, kigogo, chang'ombe temeke mtoni kichangani, hadi kwa azizi ally mkuu.
Sasa mkuu utashukaje na basi Ubungo halafu ukalale tandika, mburahati, majohe, kigogo au kivule...??? Kwann ukajifiche mbali kote huko?? Nimegundua mambo mawili:-

1. Ili uende sehemu nyng ulizotaja, labda ulitoka na mke wa mtu, so ukajificha mbali. Kwa sababu Kivule sio karibu mkuu. Ndo mnaoandika kwny kitabu cha guest: Mahali ulipotoka = Dar, Unapokwenda =Dar, sasa si bora ukalale kwenu tu..!!

2. Labda useme umetaja tu maeneo ya uswazi, ila hakuna tukio kma hilo lilotokea huko kma muuliza swali alivyotaka.
 
3 Reactions
Reply
Back
Top Bottom