Hii haijatulia- Je wee waonaje?

Kana-Ka-Nsungu

JF-Expert Member
Oct 4, 2007
2,257
353
Mara nyingi najiskia kukereka ninapokutana na waswahili wenzangu ughaibuni alafu wanajidai wanaongea kiswahili kwa taabu, na most of the time kwenye mazungumzo yetu wanakuwa wakitumia kiingereza. Mke wangu sio mswahili na ninapoishi naweza kata hata wiki sijaongea kiswahili so ninapokutana na m bongo mwenzangu naona ni kama chance ya kuongea kinyumbani. Wengine ni watu niliokuwa nikiwajua toka home, tulikua tukiongea kiswahili toka enzi zile tukiwa bongo, lakini leo nikikutana nao ni mwendo wa kimombo tu! Na wengi nimewashinda kwa elimu, kiingereza nakijua lakini naona its not right kuabudu lugha ya wenzetu wakati tunaweza ku communicate kwa lugha yetu. Mbaya zaidi, wengi hawakijui kiingereza chenyewe vizuri, nikiwasikiliza tu kwenye maongezi yao nazidi kukereka kwa jinsi kilivyo broken. Je wee unaionaje hii? haijakutokea?
 
inaweza kuwa haijatulia, lakini wenzako ndio wanajifunza hivyo.......huwezi kujua lugha kama huongei mara kwa mara!!! kwani tatizo letu wabongo na kizungu ni nini?? ni kutokukiongea ndio maana hatukijui!! mie sioni tatizo kama mtu yupo ktk harakati za kujifunza. hayo mambo ya kuongea na kukaa na waswahili sana,ndio una kuta mtu yupo "kiwanja" miaka dahali lakini hata ng'eng'e la kuombea maji lina mpiga chenga!!
kaka waache wenzako nao wajifunze, maana wewe una mtu nyumbani unaeongea nae kizungu kila siku.........dont hate!!.
 
inaweza kuwa haijatulia, lakini wenzako ndio wanajifunza hivyo.......huwezi kujua lugha kama huongei mara kwa mara!!! kwani tatizo letu wabongo na kizungu ni nini?? ni kutokukiongea ndio maana hatukijui!! mie sioni tatizo kama mtu yupo ktk harakati za kujifunza. hayo mambo ya kuongea na kukaa na waswahili sana,ndio una kuta mtu yupo "kiwanja" miaka dahali lakini hata ng'eng'e la kuombea maji lina mpiga chenga!!
kaka waache wenzako nao wajifunze, maana wewe una mtu nyumbani unaeongea nae kizungu kila siku.........dont hate!!.

Km nimemuelewa vizuri bro Kana, ni kuwa hapondi hao jamaa kuongea Kiingereza, ila anasisitiza umuhimu wa kuienzi lugha yetu. Km ni suala la kujifunza, nafasi za kufanya hivyo ziko nyingi mno huko waliko kwani Kiingereza ndio mahali pake, na waongeao Kiswahili ni wachache mno ukilinganisha na waongeao Kiingereza.

Lkn kubwa zaidi ni wale waongeao Kiswahili kwa lafudhi ya Kiingereza. Je, huko nako ni kujifunza Kiingereza? Labda kuwe ni namna ya kujifunza kusahau Kiswahili. Ni utawala wa hisia tu ndio uwasumbuao hao.
 
Jamani wengi walioko mamtoni wanaspend most of their days na wazungu- mashuleni na makazini mainly. Sasa kweli ni lazima u practise kiingereza chako unapokutana na mbongo mwenzako? Let say kuna watalii wa kiingereza wanajua kiswahili cha kujifunza na wanaishi Dar- unadhani wanapokutana wataongea kiswahili?
 
Mara nyingi najiskia kukereka ninapokutana na waswahili wenzangu ughaibuni alafu wanajidai wanaongea kiswahili kwa taabu, na most of the time kwenye mazungumzo yetu wanakuwa wakitumia kiingereza. Mke wangu sio mswahili na ninapoishi naweza kata hata wiki sijaongea kiswahili so ninapokutana na m bongo mwenzangu naona ni kama chance ya kuongea kinyumbani. Wengine ni watu niliokuwa nikiwajua toka home, tulikua tukiongea kiswahili toka enzi zile tukiwa bongo, lakini leo nikikutana nao ni mwendo wa kimombo tu! Na wengi nimewashinda kwa elimu, kiingereza nakijua lakini naona its not right kuabudu lugha ya wenzetu wakati tunaweza ku communicate kwa lugha yetu. Mbaya zaidi, wengi hawakijui kiingereza chenyewe vizuri, nikiwasikiliza tu kwenye maongezi yao nazidi kukereka kwa jinsi kilivyo broken. Je wee unaionaje hii? haijakutokea?

Aaaaa, jamani. labda kama ulivyosema "wengi hawakijui kiingereza chenyewe vizuri", si inawezekana kuwa wanafanya mazoezi ili wakielewe vizuri.
 
Hii ni Hulka yetu sisi wabongo. Mimi nimekutana nayo kwa wabongo wengi ambao lugha kuu huku(Kijerumani, spanish, French, scandinavian n.k) Ukikutana nao wanajua ni Mtz na mnaanza kusalimiana vizuri hapo baadae utadhani ni aliondoka Tanzania wakati wa ukoloni. Yaani kwake kuzungumza hiyo lugha ya wazungu badala ya kiswahili anajisikia fahari sana.

Ukweli ni kwamba kila mtu akikutana na mtu wa kwao anazungumza lugha yao hata hawa wazungu wanapenda kikwao wakutanapo, isipokuwa sisi tu tunapenda lugha zao kuliko zetu pale tunapokutana huku umatumbini.

Mtu huyo huyo mkute anamtongoza mtoto wa kikenya ambaye anazungumza kiswahili, atakuwa anaongea kiswahili utadhani ndio kwanza karudi kutoka bongo anavyoongea vizuri, Je nini sababu?????
 
Aaaaa, jamani. labda kama ulivyosema "wengi hawakijui kiingereza chenyewe vizuri", si inawezekana kuwa wanafanya mazoezi ili wakielewe vizuri.

Zomba soma post yangu ya mwisho kabla ya hii kwanza. Halafu watu mnakazania hii point ya kujifunza lakini ukweli ni kwamba most of the time inakuwa ni ubishoo tu na show off kwamba 'nami nakiweza'. Utawasikia wakijidai kuongea kama kina 50 cents and the likes- whats up nigg..? You know wa im sayin? I cant do this sh.t?? Utumbo mtupu!
 
Lakini hata wewe kiswaahili kinakwenda upande maana hapa umetuchanganyia siku hizi wanaita kiswaglishi ebu ona "na most of the time kwenye mazungumzo..", "tunaweza ku communicate" na "so ninapokutana na m bongo mwenzangu naona ni kama chance"
 
Lakini hata wewe kiswaahili kinakwenda upande maana hapa umetuchanganyia siku hizi wanaita kiswaglishi ebu ona "na most of the time kwenye mazungumzo..", "tunaweza ku communicate" na "so ninapokutana na m bongo mwenzangu naona ni kama chance"

Sina tatizo na watu wanaochomekea vijineno vya kizungu kidogo kama hivyo, ninachoongelea hapa ni mtu kuongea kimombo pasee! as if hajui hata neno moja la kiswahili.
 
Ona mwingine eti naye anaponda kuchanganya kingereza "Jamani wengi walioko mamtoni wanaspend most of their days na wazungu- mashuleni na makazini mainly. Sasa kweli ni lazima u practise kiingereza chako unapokutana na mbongo mwenzako? Let say kuna watalii wa kiingereza wanajua kiswahili cha kujifunza na wanaishi Dar- unadhani wanapokutana wataongea kiswahili?"
 
Unajua kama umehamua kuzungumza kiswahili kiwe ni kiswahili ili tujue, kuchanganya kama ulivyofanya wengine uwa wanakereeka, na hii imekuwa kama mtindo. Mtu haongei kiswahili kikanyoka, atachomeka kingereza mbaka unashindwa kujua ni lugha gani inaongelewa
 
Wee tishe unaonekana u mgumu kuelewa, walimu wako wana/ walistahili mshahara wa ziada. You are missing the point here- ninachosema hapa ni matumizi ya lugha ya kiingereza baina ya waswahili na sio kuchanganya lugha hizi mbili, kiswanglish kimekua ni kitu cha kawaida sana siku hizi kila mahali.Tatizo langu ni pale watu wanaposusa kabisa kutumia kiswahili na kuongea kiingereza tu as if hawana lugha yao au hawakifahamu.
 
Jamani titi la mama li tamu hata likiwa la mbwa! Kama kuna asiyejua utamu wa titi la mama na kulinyonya kila apatapo fursa, basi huyo ni wa kusikitikiwa tu!
Hapa kuna makundi mawili: la wale wasiopenda kutumia lugha yao ya taifa na wale wanaoitumia lakini wanaitukana kwa kuiongea visivyo au kuichanganya changanya na lugha zingine wanazodhania kuwa ni za hadhi zaidi kuliko "titi la mama yao"!
Nawapa pole, lakini tujue kuwa tatizo ni udhalili wa kiutamaduni, mtu kuhusudu (ni sahihi?) na kuabudu cha wengine na mbaya zaidi kuamini kuwa chake kina ila ya ubora!
 
Back
Top Bottom